MUNGU MKUU 16

 


SCENE 16: -

(Asubuhi ya siku nyingine Miriam yupo chumbani kwake anaonekana ana maumivu Fulani kwani anaugulia sana na Analia sana, Mary anasikia kilio hicho kwa mbali)

Mary: mwanangu Analia nini tena jamani? (Anaingia chumbani kwa Miriam) Miriam…mwanangu nini mama?

Miriam :( anashika tumbo lake) naumwa tumbo ma mdogo

Mary: limeanza tena…(anaguna)hata mimi nilipokuwa msichana nilikuwa naumwa sana tumbo pole sana mwanangu

Miriam: asante

Mary: ngoja nikamuite mama yako (anatoka)

(Baada ya muda Mary na keddy wanakuja)

Keddy: mwanangu nini tena?

Miriam: naumwa tumbo la hedhi mama

Keddy: pole…ngoja nikuletee dawa angalau litulie kidogo

Miriam :( anaitikia kwa kichwa akimaanisha kukubali)

Keddy :( anatoka anaelekea sebuleni)

(Kengele ya mlangoni inalia)

Keddy: nani tena? (Anaenda kuufungua mlango) oh Jeremy baba karibu

Jeremy: Asante… (Anaingia)

Keddy: Ariana bado kalala Nina uhakika umekuja kumuona yeye…si ndio baba

Jeremy :( hajibu kitu anabaki anatabasamu)

Keddy: karibu uketi nikamuite mchumba wako

Jeremy: hapana mama usimsumbue kwani mama siruhusiwi kuja kuwasalimia hata nyie?

Keddy: unaruhusiwa baba…anyway ngoja nikampe shemeji yako dawa anaumwa tumbo

Jeremy :(anasema moyoni) nimekuja kumuona Miriam na sio Ariana, mpenzi wangu alinipigia simu akaniambia anaumwa sana sikuweza kuvumilia nikaona nije tu nimuone…hapa natakiwa kutafuta kisingizio nimuone Miriam wangu, sijui nisemeje(anawaza)

Keddy :( anapiga hatua)

Jeremy: mama naweza kumuona Shem…

Keddy: sawa ngoja nimwambie akae vizuri

Jeremy: Asante mama... (Anamfuata nyuma)

Keddy :( anatabasamu) wewe nae nimekuambia ukae hapa nimuone Kama amekaa vizuri ndo uje

Jeremy :( anacheka) haina sawa mama

Keddy :( anaingia chumbani kwa Miriam) ebu kaa vizuri shemeji yako anakuja

Miriam :( anatabasamu kisha anajisemea moyoni) amekuja yaani hana uvumilivu huyu… (Kisha anajiweka vizuri)

Mary :( anamuangalia Miriam usoni) mbona kama umefurahi Fulani kusikia shemeji yako anataka kukuona?

Miirriam: hamna kitu ma mdogo jamani…kwanini nifurahi?

Keddy :( anamuita Jeremy)

Keddy: Jeremy?

Jeremy: naam mama

Keddy: haya njoo

Jeremy :( haraka anaingia ndani)

(Miriam na Jeremy wanatabasamiana mara baada ya kuonana)

Jeremy: shemeji…

Miriam: abee…shikamoo?

Jeremy: marahaba shemeji yangu…unaendeleaje?

Miriam: vizuri kidogo

Keddy :( anampa dawa na maji) haya kunywa

Miriam :( anapokea) asante mama (anazinywa)

Keddy:mi narudi kulala…shemeji yako huyu hapa

Miriam: sawa mama

Keddy :( anatoka)

Mary :( anagundua kitu) mpo sawa kweli nyie

Miriam: ndio ma mdogo kwanini unasema hivyo?

Mary: sijui nawaonaje tu Kama vile kuna kitu Fulani

Jeremy: hamna kitu ma mdogo

Mary: (anaguna kidogo) haya bwana ila shauri yenu… (Anatoka)

Jeremy :( anambusu Miriam shavuni) pole mke wangu…umeanza usiku?

Miriam: ndio nimeanza usiku yaani sijalala sidhani Kama nitaenda chuo leo

Jeremy :( anatoa chocolate mfukoni) nimekuletea chocolate

Miriam: Asante… (Anapokea)

Mary :( amejibanza anawaangalia) Mungu wangu hawa watoto wana mahusiano na ndo maana Jeremy kaja watakuwa wamepigiana simu…Miriam anamsaliti Ariana nah ii sio nzuri… (anasikitika sana)

Miriam: sasa nani kakuambia uje? Inamaana sitakiwi kukuambia kitu nikikuambia unakuja…si unajua mahusiano yetu ni siri? Ukifanya hivyo tena watatugundua mapema sana

Jeremy: samahani sitafanya tena lakini Miriam unajua kabisa jinsi ninavyokupenda yaani nimeamka nataka kujiandaa niende ofisini kila kitu kinagoma…nimekuona hivi sasa mambo yataenda

Miriam: Jeremy…

Jeremy: nivumilie...Nafanya hivi kwasababu nakupenda sana Miriam si unajua kuwa nakupenda sana

Miriam: nami nakupenda Sana, tunachotakiwa kufanya ni kuwa makini ikijulikana itakuwa kesi kubwa sana

Jeremy :( anambusu tena shavuni) usijali nitakuwa makini baby

Ariana :( anafungua mlango ghafla)

(Wanashtuka)

Ariana: vipi? mbona mmeshtuka? oh Jeremy…vipi umekuja nyumbani mapema hivi? una shida gani?

Jeremy :( anashikwa kigugumizi) nimekuja kuwasalimia

Ariana: saa moja?

Jeremy :( anajichekesha) yeah saa moja nilikuwa naenda ofisini

Ariana: hujavaa kiofisi

Jeremy: ah sometimes huwa naenda hivi

Ariana: okay… (Kwa Miriam) dogo vipi?

Miriam: poa shikamoo dada

Ariana: marahaba (huku anaondoka) anyways natoka ma mdogo ameniambia unaumwa ndo nikaona nije nikuone pole (anaondoka)

Miriam :( kwa Jeremy) kwani hujamwambia dada kuwa humtaki tena?

Jeremy: Nilimwambia ILA hakukubali ingawa aliniambia kuwa atawaambia wazazi wenu ila nilimuona kabisa hajalipokea vizuri

Miriam: sasa itakuwaje? Mimi sina mamlaka kuwa na wewe kama hujaachana na Ariana

Jeremy: Miriam, nitakuja na wazazi wangu tuombe radhi tutauvunja uchumba kati yangu na yeye…nakupenda na nitakuoa wewe…hata wazazi wangu wanajua kuwa nakupenda wewe

Miriam: dah…najua itakuwa vigumu sana kwa wazazi kukubali penzi letu

Jeremy: watakubali kuwa na mani mke wangu… (Anaibusu mikono na Miriam)

Miriam: sawa Nina Imani kuwa kila kitu kitakuwa sawa

Jeremy: ofcourse baby… (Anambusu kwenye paji la uso)

(Wanakumbatiana huku kila mmoja wao anaonekana amezama kwenye dimbwi la mahaba mazito)

Mary: (bado anawachungulia kwa mbali) Mungu wangu hawa watoto

Post a Comment

1 Comments