MUNGU MKUU 19

 


SCENE 19: -

(Jioni ya siku Kama tatu zimepita mara baada ya Miriam kuvunja uhusiano wake na Jeremy, Jeremy anabisha hodi kwenye malango ya nyumba ya kina Miriam)

Jeremy :( anabisha hodi)

Miriam :( anamfungulia anatoa macho kama mjusi kabanwa na mlango mara baada ya kumuona Jeremy) He!! Wewe nae…mbona umekuja?

Jeremy: nakupigia simu hupokei sijakuona tangu siku ile nimekushusha chuoni kila nikija wewe haupo umeshaondoka simu zangu unakata ulidhani Mimi ningefanyaje?

Miriam: huo ni utoto Jeremy kwanini umekuja mpaka nyumbani au mmekuja kuongelea mahari

Jeremy :( anacheka) mahari yako

Miriam: acha utani wako tumeshazungumza na tayari tumeshavunja uhusiano wetu sasa unanipigia simu ya nini?

Ken :( anakuja) kuna nini Miriam mbona umeganda mlangoni mama

Miriam :( anajaribu kumsukuma Jeremy ili aondoke)

Jeremy :( analeta ubishi)

Miriam: hamna kitu baba

Ken: nani alikuwa anabisha hodi?

Jeremy :( anajitokeza) shikamoo baba

Ken: oh, baba marahaba mwanangu karibu ndani

Jeremy :( anamuangalia Miriam huku anatabasamu)

Ken: karibu Sana…

Jeremy: Asante Sana baba…shikamoo

Ken: marahaba hujambo? (Kwa Miriam) mama embu njoo umletee shemeji yako hata kahawa…au juisi

Jeremy :( anatabasamu)

Miriam :( anaenda jikoni)

Ken: enhe…baba karibu mmetususa Sana jamani kwani tuliwakosea wapi sie?

Jeremy: hapana majukumu mzee wangu

Ken: wazazi wako hawajambo?

Jeremy: wote wazima baba sijui nyie hapa

Ken: ah tupo tu ila Miriam ndo kidogo madonda ya tumbo yamemuibukia…

Jeremy :( anashtuka) eeh Mungu wangu

Ken: ila anaendelea vizuri si unaona mpaka anatembea…alikuwa anaumwa Sana

Jeremy: oh God… (Anajisemea moyoni) ndo maana labda hakuwa ananipokelea simu yangu na chuoni nilikuwa simuoni kumbe alikuwa anaumwa jamani mtoto jasiri huyu…

Miriam :( anarudi akiwa na glasi mbili za juisi) karibuni (anazitenga kwa heshima)

Jeremy: samahani chooni ni wapi?

Ken: Miriam embu muonyeshe shemeji yako chooni

Miriam: naomba unifuate… (Anamuongoza njia)

Jeremy :( wanapofika mbali upeo wa macho ya watu, anambana ukutani) mbona hukuniambia kuwa unaumwa Miriam…badilisha nguo twende hospitali sasa hivi

Miriam: kwanza unaniumiza, naomba usogee mbali…lakini pili nimeshapelekwa hospitalini kwahiyo sihitaji kwenda hospitalini tena…

Jeremy: sawa tuvunge umeshinda…kwanini hukuniambia kuwa unaumwa?

Miriam: nikwambie ili iweje? Mimi ni shemeji yako

Jeremy :( anamkazia macho) inamaana unataka kuniambia kuwa umesahau wakati tuliokuwa nao pamoja wakati mzuri…beach, migahawani

Miriam: yamepita na wala sitaki kukumbuka maana itanipa shida tu mimi…usisahau kuwa wewe ni mchumba wa dada yangu… (Anaona mama yake anakuja) mama huyo...Haya shemeji chooni ni humu

Jeremy:(anageuka anaona ni kweli ni mama yao Ariana na Miriam) okay asante Miriam (kwa mama) shikamoo mama

Keddy: marahaba baba hujambo?

Jeremy: sijambo… (Anaingia chooni)

Miriam :( anaondoka)

Keddy :( anapita na kuondoka zake)

Jeremy: (anafungua mlango wa chooni na kutoka) Miriam…

Miriam :( anamgeukia) jamani si uniache…

Jeremy: my lady usinifanyie hivyo….

Miriam: jamani fanya tu kuniacha bwana unajua unanitesa Sana bwana ee

Jeremy: wewe ndo unanitesa Sana bwana, kwani bado unajisikia vibaya Sana? Naomba basi nikupeleke hospitali

Miriam: usiniletee matatizo...Bwana naomba uniache tu

(Wanakutana na Mary njiani)

Mary: vipi nyie mbona mnafatana nyuma kama kumbikumbi?

Miriam: shemeji ametoka chooni

Mary: ndo umempeleka kwani yeye amekuwa mtoto anahitaji kusindikizwa?

Miriam:  alikuwa hapajui

Mary :( Kwa Miriam) huyo ni shemeji yako sijui unaelewa hilo?

Miriam: ndio naelewa na sitasahau kuwa ni shemeji yangu

Jeremy :( anajisemea moyoni) dah huyo maza ananiharibia kweli na swaga zake za ushemeji hapa mi nahangaika huyu mrembo anielewe kuwa yeye kwangu ndo wa muhimu huyu maza anazingua dah...

Mary: nendeni sebuleni walipo wengine sio vizuri kujibanza

Miriam:(anaenda sebuleni)

Jeremy:(anamfuata nyuma)

Mary:(anamshika mkono Jeremy) acha kumletea matatizo mwenzio sawa ee

Jeremy: kivipi ma mdogo…

Mary: najua una mahusiano nae…wewe hujui hiyo itamletea shida…mtoto mwenyewe… (ananyamaza ghafla)

Jeremy: mtoto mwenyewe nini ma mdogo…

Mary: anaaminika sana kwa wazazi wake kwahiyo usije ukamharibia mwenzio uaminifu wazazi wake wakaona kama hana adabu

Jeremy: nashukuru umejua kuwa nampenda Miriam, ma mdogo ni kweli nampenda sana Miriam yaani Miriam ndo mwanamke wa maisha yangu

Mary: wewe mtoto acha kabisa huo ujinga acha kabisa na umuoe huyu uliyemchumbia mwanzo

Jeremy: siwezi…nitaoa ninayemtaka…samahani kwa kukujibu vibaya ila nitamuoa ninayemtaka na huyo ni Miriam (anaondoka na kuelekea sebuleni)

Mary:(anajisemea moyoni) huyu kijana atamletea mwanangu shida jamani si amuache? watoto bwana wakiwa wadogo wanasumbua wakiwa wakubwa ndo usiseme sasa hapo Ken na mkewe wakijua kuwa Miriam anamuibia mume mtoto wao sijui itakuwaje (anaguna kisha anaenda kuendelea na kazi zake)

(Huku sebuleni)

Jeremy: jamani naomba niwaage mi naenda

Ken: haya baba karibu… (kwa Miriam) we Miriam mtoe shemeji yako

Miriam:(anatii kisha anatoka nje yeye pamoja na Jeremy)

Jeremy:my lady…I love you so much

Miriam: Jeremy...sijui nikwambieje ila hatuna ruhusa ya kupendana…

Jeremy: kwani hao ni Mungu? wakikufukuza nitakujengea nyumba nzuri nitakuoa haki ya Mungu sikudanganyi

Miriam: hapana familia ni muhimu kuliko hivyo vyote

Jeremy: jamani Miriam usinifanyie hivyo

Miriam: nenda tu nyumbani (anarudi zake ndani)

Post a Comment

0 Comments