SCENE 20: -
(Asubuhi mpya iliyojaa matumaini
mapya Kwa viumbe vyote, Jeremy yupo ofisini kwake akiwa anafanya shughuli
mbalimbali yeye na wafanyakazi wake, wakati huo anaendelea na kazi zao, simu ya
Jeremy inaita kwa kuwa iko mbali nae anaomba msaada wa kuletewa simu hiyo)
Jeremy:
embu Anita nipe simu ila angalia nani anapiga?
Anita:
my lady
Jeremy:
wewe…ikimbize haraka hiyo simu
Anita
:( anaiwahisha) boss kwani my lady ni
nani?
Jeremy
:( anatabasamu huku anaichukua simu
kutoka kwa anita) wifi yako...Haya kaendelee na kazi zako
Anita
:( anaondoka)
Jeremy
:( anapokea simu) my lady nilijua tu
kuwa utanipigia mara baada ya kukuta missed calls
Miriam:
kwanini ulikuwa unapiga kwa mfululizo?
Jeremy:
jamani kwani wewe hujui kwanini nafanya hivyo? Si nakupenda?
Miriam:
tufanyeje sasa…maana Mimi nakupenda pia...Tena Sana ila naipenda sana familia
yangu nampenda dada yangu na mama na baba yangu wakisikia huu utakuwa usaliti...
Jeremy
:( anatoka nje) No baby hakuna mtu
anayeweza kulazimisha moyo umpende mtu ambae haumtaki…Mimi nakupenda wewe hata
iweje siwezi kumpenda Ariana maana yeye sio chaguo langu
Miriam:
kiukweli Mimi sijui cha kufanya Zaidi Jeremy
Jeremy:
ufuate moyo wako...Hayo mengine tutakuja kujua mbele ya safari tu jamani Miriam
Miriam:
kwakweli sijui nipo dilemma…ma mdogo ananiambia ukweli kuwa kumchukua mchumba
wa dada yangu sio vizuri lakini moyo wangu hautaki kusikia kabisa moyo wangu
hautaki kuelewa kuwa sio vizuri kumchukua mchumba wa dada yangu
Jeremy:
kwasababu sio vibaya kupenda Miriam
Miriam:
ila ni vibaya kuisaliti familia yako...
Jeremy:
tutawaambia…na kumbuka sio kwamba nilipanga kuwa nikifika kwenye nyumba ya
mchumba ambae wazazi wangu wamenitafutia nitampenda mdogo wa mchumba wangu
huyo…hapana ilikuja tu bila mimi mwenyewe kujua wala kutambua…wala kutarajia
Miriam
:( anashusha pumzi) kwahiyo
tufanyeje?
Jeremy:
tupendane…ukiwa tayari Kwa ndoa maana Mimi nipo tayari wakati wowote
Miriam
:( anaguna)
Jeremy:
ukiwa tayari basi tutawaambia wazazi wetu
Miriam:
sikutegemea Kama ningekupenda Jeremy…nilifata tu kutaka kutimiza ombi la baba
yako la kusema kuwa unaweza kujiua…na pia nilifata ushauri wa Vanessa ningejua
hata nisingejaribu kukaa karibu na wewe
Jeremy:
Mungu alitupangia tu kuwa pamoja na wala sio wanadamu...Nakupenda Miriam naomba
usiogope kunipenda mpenzi wangu
Miriam:
okay tupendane mpenzi wangu ila sasa siku Ariana akijua itakuwa msala…
Jeremy:
tutajiandaa kwa hilo...Tutakuwa pamoja wakati hili linatokea
Miriam:
usinidanganye…nakuomba
Jeremy:
hapana…sikudanganyi mpenzi wangu
Miriam:
okay
Jeremy:
Asante Kwa kunielewa…by the way uko wapi?
Miriam:
bado nipo nyumbani…
Jeremy:
Leo huendi chuo?
Miriam:
Leo Nina vipindi saa tano mpaka saa Saba
Jeremy:
nitakupitia tukale lunch pamoja…
Miriam:
okay
Jeremy:
lakini natamani nije nikuchukue nikupeleke chuo ila nimebanana kweli nitapata
muda mchana
Miriam:
usijali baba atanipeleka
Jeremy:
au nikununulie gari?
Miriam:
hapana ukininunulia gari nitaulizwa Sana nyumbani
Jeremy:
nakununulia gari natafuta na dereva mwanamke anakuwa anakupitia kila ukitaka
kuzunguka labda sokoni, chuoni, supermarket kwa marafiki na kadhalika
Miriam
:( anacheka) hata usijisumbue
Jeremy:
please sipendi ukipita njiani Kwa miguu…wanaume watakutamani una umbo na una
sura nzuri watakuona
Miriam
:( anacheka) umeanza wivu wako sasa
Jeremy
:( anacheka pia) lazima niwe na
wivu…wewe mke bwana
Miriam
:( anacheka) ngoja nikate simu naona
mama anakuja
Jeremy:
I love you
Miriam:
I love you too… (Anakata simu haraka)
(Upande
wa Jeremy anarudi ofisini akiwa ana furaha Zaidi)
Anita
:( anamtania) wacha we wifi
amekufurahisha nini
Jeremy:(anatabasamu) acha tu
mwenzangu(anacheka)embu kafanye kazi
acha umbea
Anita:(anaondoka huku anacheka)
Jeremy:(anabaki anaangalia picha ya Miriam kwenye
simu yake, anatabasamu mwenyewe)

0 Comments