SCENE 8: -
(Miriam anafika chuoni anatembea
taratibu kuelekea darasani, wakati anaendelea kutembea anasikia honi ya gari
nyuma yake haraka anageuka kuangalia ni nani)
Miriam
:( anageuka) nani?
Jeremy:
Mimi (anasogeza gari karibu na Miriam
kisha anashusha kioo)
Miriam:
oh…shemeji
Jeremy:
Jeremy…
Miriam
:( anatabasamu)
Jeremy:
za toka siku ile?
Miriam:
nzuri tu…
Jeremy:
njoo ukae nikusindikizie mpaka darasani
Miriam:
nimefika shemeji...
Jeremy:
nakuomba sana Miriam
Miriam:(anaingia kwenye gari) haya…umefurahi?
Jeremy:(anatabasamu) nimefurahi sana…
Miriam:(anacheka)
Jeremy:(anaanza kuendesha gari) wewe ni mrembo
sana…una umri gani ulisema?
Miriam:
miaka 18…
Jeremy:
umesoma harakaharaka sana upo chuo na una umri mdogo sana
Miriam:
nilianza shule mdogo sana
Jeremy:
naomba namba yako kabla ya yote usije ukashuka bila kunipa namba yako (anatoa simu yake aina ya iphone 14 na kumpa Miriam
aandike namba yake) naomba namba yako please
Miriam:
sasa mimi namba yako ya nini?
Jeremy:
naomba… (anaacha kuendesha gari)
nakuomba…Miriam
Miriam:(anacheka na kubadilisha mada) dada
amekupenda kweli na amesema kuwa utafaa kuwa mumewe
Jeremy:(anamuangalia usoni bila kusema kitu)
Miriam:
hivi una umri gani shemeji samahani lakini shem…
Jeremy:
bila samahani…nakuzidi miaka 12 kwahiyo nina miaka 30
Miriam:
mnalingana na dada
Jeremy:mi
nataka kukuoa wewe
Miriam:
wewe shem hata usiongee hivyo hata kimasihala
Jeremy:
kwanini?
Miriam:
wewe ni mchumba wa dada yangu na naomba ubaki hivyo…
Jeremy:(anacheka) nakutania tu Miriam
Miriam:
najua unanitania… (anaangalia alipoweka
mkono wake anaona gazeti lenye picha ya Jeremy mbele ya gazeti hilo) na
mimi mpelelezi…na hii picha inafanya nini kwenye hili gazeti
Jeremy:
soma si unajua kusoma?
Miriam:
wewe Mohamed Dewji?
Jeremy:(anacheka)
Miriam:
upcoming young business icon of the year
Jeremy:(anacheka) yes…
Miriam:
wewe ni mfanyabiashara eeh…
Jeremy:
nina hotel Dar es Salaam, Mwanza na Arusha…nina supermarket Dodoma na nina
filling station kama tatu hapa Dar
Miriam:
wow…hongera
Jeremy:
asante na zinafanya vizuri…kinachokosekana maishani mwangu ni mwanamke tena
simaanishi mwanamke tu…natafuta true love
Miriam:(anacheka) si umempata dada yangu
Jeremy:(anacheka) ninaishi peke yangu na mwisho
wa siku nikaona nimwambie baba anitafutie mchumba ila katika hilo nikaona ua
lililonipendeza sana na ninataka nilichume
Miriam:
kwahiyo kwa lugha nyingine hutaki tena kumuoa dada yangu?
Jeremy:
kwa bahati mbaya…ndio…
Miriam:
kwanini…ulikuja nyumbani…
Jeremy:
hapo ilikuwa kabla ya kuona ua langu
Miriam:
yaani wanaume
Jeremy:
hapana usituchukulie hivyo...
Miriam:
sasa unadhani dada yangu atajisikiaje akijua kuwa wewe humtaki na yeye anakupenda
sana...tangu mmeondoka amekuwa akiongea sana kuhusu wewe yaani anakupenda sana
shemeji kwanini unafanya hivyo…?
Jeremy:
iam sorry…okay tumeongea sana na ninajua kuwa unahitaji kwenda darasani…naomba
namba yako
Miriam:
ya nini huku unasema una ua lako? kama ni hivyo naomba uwaambie wazazi wangu
kuwa hutamuoa dada yangu ili waache kupanga hii harusi…
Jeremy:
nitafanya hivyo…
Miriam:(anajikuta anamuonea huruma dada yake)
shemeji jamani usifanye hivyo tutachekwa maana mlipokuja tu wazazi wetu
wakaanza kuwaambia watu ya kwamba dada Ariana anatarajia kufunga ndoa
Jeremy:
but I don’t love her na ndoa yetu haitakuwa na Amani maana hakuna upendo baina
yetu
Miriam:
utampenda tu…
Jeremy:
hamna…embu naomba simu yako
Miriam:(anatoa simu aina ya iphone 6 PLUS) ya
nini?
Jeremy:(anaichukua na kuweka namba yake)
Miriam:
simu yangu haina salio
Jeremy:
itakuja tu
Miriam:(anatabasamu)
Jeremy:(anajaribu kujipigia na haraka namba ya Miriam
inaingia kwenye simu yake) asante Miriam
Miriam:
sawa…
Jeremy:(anatoa pesa kama elfu hamsini) chukua
hii utanunua vocha
Miriam:
mbona nyingi?
Jeremy:
ya kawaida bwana…najua una mahitaji mengi kama vocha na sio kila kitu
utamwambia baba na mama…
Miriam:
asante lakini…ubarikiwe
Jeremy:
usijali…
Miriam:mi
naenda sasa
Jeremy:
naomba nikupigie simu baada ya masomo tuonane
Miriam:(anaguna) sidhani kama nitaweza
Jeremy:
usijali…tunaenda kunywa tu soda halafu nakurudisha nyumbani
Miriam:
baba huwa anakuja kunichukua na kunileta chuoni
Jeremy:
ah…hiyo ni mbaya…kwahiyo tufanyaje?
Miriam:
hata sijui…
Jeremy:
okay nenda nitajua cha kufanya siwezi kukosa cha kufanya ili nionane na wewe
Miriam:
lakini kwanini unataka kuniona?
Jeremy:
basi tu…
Miriam:(anashuka kwenye gari na kwenda darasani)
Jeremy: I love you Miriam
nakupenda sana…nimepata mtu wa kukaa nae my life partner…I love you najua
itakuwa ngumu sana kwetu ila tutapata tu njia my love… (anawasha gari na kuondoka zake)
1 Comments
Miriam na ariana into conflict😅🙌
ReplyDelete