SCENE
46: -
KWENYE
JUMBA BOVU LA KINA ARIANA: -
(Majira
ya saa moja usiku giza totoro limetanda juu ya nchi, Ariana amesimama kwenye
jumba ambalo aliwahi kumtekea Miriam, anaonekana kuna kitu au mtu anamsubiri
kwa hamu. Baada ya kusubiri kwa muda mrefu hatimaye mtu yule anafika)
Mtu:
boss nimefika
Ariana:
nakuona (anatabasamu) Colton za kwako? Asante kwa kunisaidia kwenye hili
Colton:
usijali
Ariana:
tumefanya mambo mengi sana kuhakikisha Miriam anahukumiwa kufa…
Colton:
sawa sawa boss
Ariana:
unajua nimetembea na hakimu ili atoe hukumu nayotaka mimi
Colton:
Duh wewe noma sana…uko vizuri lakini huoni ni dhambi unajichumia
Ariana:
(kwa kejeli) wanasema Mungu ni wa huruma husamehe dhambi
Colton:
acha kumkejeli Mungu
Ariana: hata
mimi atanisamehe tu…ila nimekukubali sana umeiba nguo za Miriam kwa maumivu
makubwa ukatoa damu yako na kuzipaka baada ya kufanya hivyo ukazirudisha ili
uwe ushahidi aisee nimekupenda bure
Colton:
nilikuwa nafata maagizo yako
Ariana:
safi sana wewe kweli ni rafiki mwema yaani umesimama na mimi kwenye shida na
raha…
Colton:
nimefanya ulichotaka ingawa mara ya kwanza sikuona kama itakuja kunitesa
hivi…mtoto wa watu atanyongwa kwa kosa ambalo sio lake na wala mimi sijafa
Ariana:
(anacheka kidogo) huyo mtoto unayesema sijui unamuona huruma ni mtoto
aliyenitesa mimi kwa asilimia mia…amechukua kila nilichokuwa nacho…namchukia
sana
Colton:
ungemuadhibu kivingine
Ariana: usinifundishe
(anafyonza) huyu Malaya amenitesa mimi hata huyo Mungu wenu anajua
Colton:
acha kumkejeli Mungu Ariana
Ariana:
aende zake
Colton:
Mungu hakejeliwi
Ariana:
aende zake huko
Colton:
(anatikisa kichwa) Mungu wangu hakejeliwi nimefanya kosa kubwa sana
kuungana na wewe kumpoteza Miriam sasa yupo jela anasubiri hukumu
Ariana:
na atanyongwa… (anacheka) maana kila kitu nimekipika na kikaiva
kinasubiri kiipuliwe kiliwe (anacheka) Miriam akishakufa Jeremy atakuwa
wangu na familia yangu itakuwa yangu peke yangu
Colton:
sawa hongera…naomba uniache niende nikapate chakula kisha nipumzike…sijisikii
vizuri
Ariana:
hauendi popote baba
Colton:
ukimaanisha?
Ariana:
kwamba kitu pekee ambacho sijafanya ni ushahidi wa mwili wako…
Colton:
unataka kufanyaje Ariana...?
Ariana:
kukuua
Colton:
(anatoa macho kama mjusi kabanwa na mlango)
Ariana:
(anatoa bastola kutoka kwenye mkoba wake)
Colton: Ariana
naomba usiniue tafadhali maana nimefanya kila ulichoniambia tena kwa uaminifu
mkubwa sana
Ariana:
najua hata mimi naona vibaya sana kukua ila unadhani nitafanyaje? Nataka Miriam
afe sasa hatakufa kama wewe upo hai mtakutana ahela
Colton: Ariana
please…
Ariana:
iam so sorry my dear friend (anafyatua risasi moja)
Colton:
(inamfikia kifuani Analia kwa uchungu kisha anaanguka chini)
Ariana:
(anaweka bastola kwenye mkoba kisha kwa kiwewe anakimbia)
BAADA
YA DAKIKA TAKRIBANI THELATHINI
Colton:
(ananyanyua mkono kwa maumivu makubwa sana) aah nina bahati sana (anachukua
simu na kumpigia mtu Fulani)
(Simu
inaita)
Sauti:
enhe...nambie
Colton:
kama uliota ni kweli amejaribu kuniua…nakushukuru sana kwa kuniandaa
Sauti:
usijali...toka hapo sasa…kwani yeye yuko wapi?
Colton:
ameondoka nahisi… ila nina maumivu
Sauti:
ni uoga tu sidhani kama imefika popote…nimekuvalisha hii bullet proof
Colton:
ulijuaje atanipiaga maeneo ya kifuani?
Sauti:
hata mimi nashangaa…nilijuaje…anyways toka hapo njoo moja kwa moja tulipopanga,
pole lakini kwa maswaibu uliyopata
Colton:
sawa, usijali
(wanakata
simu)
Colton:
(kwa kuugulia ananyanyuka na kuondoka mahali hapo)
0 Comments