MUNGU MKUU 45


 

SCENE 45: -

RUMANDE ALIPO MIRIAM: -

(Jioni ya siku nyingine, Miriam yupo rumande pamoja na wafungwa wengine. Upole na unyenyekevu wake unampa marafiki wapya sehemu hiyo, pamoja na kuwa na marafiki wapya bado moyo wake unaumia sana kwa hali anayopitia)

Miriam: (Analia sana)

Rafiki: usilie umeshalia sana jamani kwanini usiache kulia?

Miriam: naogopa…naogopa matokeo ya haya yote

Rafiki: umeniambia kuwa hukuua Mungu anakujua na atakupigania

Miriam: sijui rafiki yangu

Rafiki: usilie yaani tangu umekuja wewe ni kulia tu

Miriam: (anafuta machozi)

Rafiki: embu tuachane na hayo…yule kaka mrefu aliyekuja kukuona na anakuja sana ee ni nani yako?

Miriam: (anatabasamu kidogo) ni mpenzi wangu actually ni mchumba wangu yeye ndo chanzo cha haya yote…ndo maana nafikiria kuachana nae

Rafiki: jamani kwanini?  kaka wa watu alivyo mzuri jamani mashallah

Miriam: kwanza najua nitakufa tu hapa hukumu ikitoka nitakufa ni bora nimuachishe tumaini la kuoana na mimi

Rafiki: sio vizuri

Afande: (anakuja walipo kina Miriam) Miriam njoo kuna mgeni wako

Rafiki: amekuja tena…yaani anajitahidi kuja

Miriam: (anaamka na kumfuata afande baada ya hatua chache anafika alipo Jeremy) Jeremy

Jeremy: baby

(Wanakaa)

Jeremy: unaendeleaje?

Miriam: salama shikamoo

Jeremy: marahaba

Miriam: bora umekuja nina jambo nataka kukuambia

Jeremy: una mimba yangu? Baby najua utakuwa na mimba yangu nafanya juu chini utoke ili tufunge ndoa tumlee mtoto wetu

Miriam: sina mimba…

Jeremy: lakini nilikuwa nina uhakika baada ya siku ile

Miriam: mimi ndo najua by the way najutia kile kitendo

Jeremy: kwanini?

Miriam: tulizini

Jeremy: ila si tuna mpango wa kuoana?

Miriam: huo mpango umeisha

Jeremy: hata sikuelewi Miriam

Miriam: mimi na wewe basi

Jeremy: you can’t be serious Miriam…

Miriam: kwa bahati mbaya nipo very serious

Jeremy: nimekukosea nini Miriam

Miriam: nadhani ndoa yako na Ariana inabidi iwe

Jeremy: simpendi Ariana and you know it

Miriam: jilazimishe

Jeremy: Miriam umesahau mapenzi yetu, ahadi zetu hata mipango yetu mpenzi wangu embu niambie nakosea wapi nitajirekebisha ila tafadhali naomba usiniache

Miriam: mimi ni mfu nasubiri tu siku ya hukumu na baada ya hapo sitakuwepo tena Jeremy

Jeremy: we are doing our very best mimi na mwanasheria wako tunafanya kila kitu

Miriam: (machozi yanamlenga) nielewe Jeremy bora uumie uzoee kuliko kuniona nimekufa utaumia sana

Jeremy: usiniache tafadhali Miriam wangu nipo chini ya miguu yako ni wewe pekee ninayekupenda kwa dhati kabisa naomba usiniache Miriam

Miriam: (Analia) ila nitakuacha hivi karibuni Jeremy

Jeremy: Mungu wetu hatoruhusu nakuomba sana nipe nafasi mpenzi please (anamshika mkono)

Miriam: (Analia) Jeremy naomba uende nyumbani na usirudi tena

Jeremy: Miriam that is not fair…

Miriam: iam so sorry (ananyanyuka)

Jeremy: Miriam…

Miriam: (anaondoka)

Jeremy: Miriam…Miriam usinifanyie hivyo tafadhali

Miriam: (anaingia rumande)

Jeremy: (anabaki anasikitika sana)

Post a Comment

0 Comments