MUNGU MKUU 50


 SCENE 50: -

MAHAKAMANI: -

SIKU YA HUKUMU: -

(Watu wamekusanyika pamoja kwa ajili ya kusikiliza hatma ya kesi inayomkabili Miriam)

Hakimu: (anaingia)

Watu: (wanasimama ishara ya heshima)

Hakimu: (anaketi)

Watu: (wanaketi)

Miriam: (ameshafika na anaonekana ana wasiwasi sana)

Mwansheria: unatetemeka sana…hiyo sio nzuri kwa ujauzito wako

Miriam: (machozi yanamlenga) nini faida ya kuwa na ujauzito huku leo hukumu inatoka kuwa nimeua na nitanyongwa mpaka kufa?

Mwanasheria: tulia Miriam tafadhali niamini mimi basi kama sio mimi muamini Mungu basi

Miriam: (anaangalia nyuma anawaona ndugu zake, baba yake, mama yake, mama yake mlezi pamoja na baba yake mlezi, rafiki yake kipenzi, mchumba wake, bibi na babu wake pamoja na mama yake mkubwa na Zaidi dada yake wa kufikia) imagine hawa wote baada ya leo sitawaona tena… (machozi yanamtoka)

Mwansheria: tulia Miriam nakuomba...

Mwendesha mashtaka: leo ndo ile siku ambayo tumekutana hapa kusikiliza hukumu baada ya kukusanya ushahidi kutoka pande zote (anamuinamia hakimu) kwa heshima naomba mheshimiwa uendelee

Hakimu: (anaangalia karatasi yake) mahakama hii imekuta

Ariana: (anatabasamu) ni wakati sasa Miriam umekwisha…yuko wapi huyo Mungu wako mbona hatumuoni?

Hakimu: mahakama imekuta

Miriam: (amejiinamia Analia sana)

Jeremy: (anatetemeka)

Vanessa: eeh Mungu huu ni wakati sasa Mungu simama mwenyewe rafiki yangu hajaua

Miriam: nimekwi…

Sauti: (kutoka nyuma) subiri

(Watu wanageuka)

Mtu: (anakuja kwa kasi kubwa sana)

Watu: (minong’ono)

(La haula!!! Mtu mwenyewe sio mwingine ni Colton yule yule iliyosemekana ameuliwa na Miriam)

Ariana: (kwa mshangao) Colton???

Miriam: Colton…?

Jeremy: (anatabasamu) thank you man!!!

Mwansheria 2: (anatoa macho) mzimu…

Vincent: (anatabasamu)

Miriam: (kwa mwanasheria) muujiza…

Mwanasheria: kuna mambo mengi sana utasikia kaa kwa utulivu

Miriam: MUNGU MKUU… (Analia kwa furaha) iam safe now

Colton: (anaendea kizimba)

Mwendesha mashtaka: umefufuka?

Hakimu: umetokea wapi?

Colton: sikufa na wala sikuzikwa… (kwa Miriam) Miriam mdogo wangu kipenzi nisamehe

Miriam: (anashangaa)

Ariana: (anatoa macho)

Miriam: mimi mdogo wako?

Colton: ndio Miriam mimi ni mtoto wa bwana Vincent nilizaliwa mimi ndo ukazaliwa wewe…
Miriam: (anashangaa)

Colton: kwa bahati mbaya nilijua hivi karibuni kweli hii dunia ndogo sana…baba yangu na mama yako walikuwa mahawara baba yangu alikuwa ni mume wa mtu…wakati wapo kwenye mahusiano mama yako alibeba mimba ambayo matunda yake ni wewe Miriam

Miriam: (anashangaa)

Colton: sikujua mpaka baada ya kukufanyia unyama mdogo wangu (Analia) nisamehe mdogo wangu ni ujinga tu…ni mapenzi tu na ujana ndo ulikuwa unanisumbua mpaka nikakubali huo ujinga

Ken: (anashangaa) Colton kaka yake Miriam kivipi?

Mwansheria 1: embu tusimulie maana hata hatuelewi naamini hakuna anayeelewa wewe ni kaka wa Miriam kivipi ulijua lini saa ngapi…ulijua kabla au baada ya kujua kuwa una mdogo anayeitwa Miriam?

Colton: ilikuwa baada ya kufanya haya

Mwanasheria 1: mlifanyaje mpaka polisi wakaamini kuwa umekufa?

Colton: tulipanga vizuri kabisa na Ariana

Keddy: (anashangaa) Ariana???

Colton: Ariana hakuwahi kumpenda Miriam tangu siku ya kwanza anamuona...aliniambia kuwa Miriam alimuibia kila kitu tangu siku ya kwanza amefika…Miriam ni mtoto wa kufikia wa wazazi wa Ariana…mara ya kwanza hakujua maana wazazi wale walimpenda kama mtoto waliyemzaa…hicho hakikumpendeza Ariana hata kidogo…wivu ukajenga chuki na kila siku ulizidi wakati Miriam akiwa bado mdogo sana alimchukua na kwenda kumficha porini ili wanyama wakali wamtafune ila Mungu alikuwa upande wa Miriam alipatikana

Watu: (wanashangaa)

Colton: walipokuwa wakubwa Miriam akiwa na umri wa miaka 18 mchumba alikuja nyumbani kwa lengo la kumchumbia Ariana ila kwa bahati sijui mbaya sijui nzuri mchumba akampenda Miriam kama mnavyojua penzi kikohozi mchumba akamwambia ukweli Miriam juu ya hisia zake kwa moyo mzito Miriam alikubali wakaanza mahusiano na bwana yule

(Watu wanasikiliza kwa makini)

Colton: mahusiano yale yalijulikana kwa Ariana alichukia sana akamteka Miriam na kumtesa sana

Ken: (anashangaa) kumbe adui alikuwa ndani kwangu

Colton: Miriam alipatikana kwa msaada wa mpenzi wake ambae sasa ni mchumba na baba wa mtoto wake aliye tumboni kwake…Ariana hakuridhika akanituma niende nyumbani nijifanye ni mchumba wake lakini pia hawara wa Miriam…nilikubali

Keddy: (anashangaa) kumbe mipango yote alikuwa anayafanya Ariana?

Colton: nikajifanya bwana wake nikamuharibia Miriam kwa wakwe zake yaani wazazi wa mchumba wake…hilo lilipita alipoona ameshindwa kabisa Ariana aliijifanya amepatana na Miriam akiwa na mpango mwingine kichwani mwake

Watu: Mungu wangu

Colton: mpango wa mimi kujifanya nimeuliwa na Miriam ni kweli ile damu ni rangi tu…nguo zake tulikuja kuziiba na nikazipaka damu yangu…nikisaidiwa na baadhi ya maaskari

Askari 1: (anaangalia chini)

Colton: baada ya tukio la kuiba nguo nilichoka nikaona nirudi nyumbani kwa baba yangu maana nilikuwa nimekimbia nyumbani kwa sababu ya ujinga wangu…(Analia)

Watu: (wanasikitika)

Miriam: (Analia)

Jeremy: MUNGU MKUU sana acha niziimbe sifa zake God did it my love…

Ariana: (amekaa kimya huku anaangalia chini kwa aibu)

Miriam: (anamgeukia Jeremy)

Jeremy: Jesus did it my love

Mwanasheria 1: tuambie ulijuaje kuwa Miriam ni dada yako na ulifanyaje baada ya hapo…

Colton: okay nitasimulia kisa kizima naombeni muda kidogo

FLASHBACK

Post a Comment

0 Comments