SCENE
56: -
BAADA
YA MIEZI MITATU: -
HARUSI
YA MARY NA VINCENT: -
(Miriam
anamuandaa mama yake kwa ajili ya ndoa itakayofanyika muda mchache baadae)
Mary: oh,
Mungu wangu
Miriam:
umependeza sana…(anatabasamu) mama yangu wewe ni mrembo sana
Mary: (amependeza
sana) jamani Miriam (anatabasamu)
Miriam:
mama
Mary:
mmmh…
Miriam:
una furaha?
Mary:
sana mwanangu kuna mtu ambae aliota kuolewa na mwanaume Fulani nae akamuoa
akaacha kufurahi kweli?
Miriam:
ulikuwa unaota kuolewa na baba?
Mary; (anakaa
kimya kidogo) Vincent ni mwanaume wa ujana wangu…alikuwa ni mume wa mtu
wakati tunakupata wewe, aliniacha na kwenda kwa familia yake na mimi nyumbani
nikafukuzwa sikuwa na msaada mwingine Zaidi ya kukuweka mlango kwa baba na mama
Ariana…nina furaha wazazi wale walikulea kwa upendo na kukupa kila kitu
ulichohitaji…(anatabasamu) nimekaa miaka 20 bila kumuangukia mwanaume
yeyote maana nilikuwa nampenda sana Vincent –ila sio kwamba sikuwa na mahusiano
ila tu muda wote huo nilkuwa nampenda sana Vincent
Miriam;
oh mama
Mary:
sikuwahi kujua kama Mungu atafanya muujiza wa kunileta karibu na Vincent na
baada ya masaa machache naingia kanisani kwenda kuungana na mwanamume
niliyempenda maisha yangu yote
Miriam:
utapenda kuzaa?
Mary:
hapana Miriam nimeshazeeka sana
Miriam:
miaka 37?
Mary:
ndio
Miriam:
mama watu wanazaa mpaka miaka 41 mpaka miaka 45 mama—usiwe mchoyo mama mi
nataka mdogo wangu
Mary: (anamshika
bega mwanae) haya hayo tumuachie Mungu
Mama Mary:
(anakuja) nyie bado mnapiga stori muda umeisha
Mary:
mama
Miriam:
bibi hujaenda tu kanisani
(simu
ya Miriam inaita)
Miriam:
baba Glory anapiga…ataanza kunigombeza
Mama Mary:
wanaume ndivyo walivyo shoga yangu…
Miriam:
(anapokea) shikamoo baba glory
Jeremy: marahaba
mama Glory !!!mpo wapi jamani?
Miriam:
tunakuja…tupo saluni bado kwani mmeshaanza?
Jeremy:
hapana tutaanzaje huku bibi harusi hajafika?
Miriam:
ngoja nimnyonyeshe Glorify nakuja
Jeremy:
msichelewe mama Glory…
Miriam:
hatuchelewi
(wanakata
smu)
Mama Mary:
ulikuwa unaogopa bure mbona hajakugombeza
Miriam:
sipendi kumuudhi maana akichukia muziki wake sio wa kitoto
Mary:
naelewa mama
Miriam:
nampenda baba Glory
Mama Mary:
hata yeye anakupenda sana…yaani napenda mnavyoheshimiana na hicho ndo
kitawawaongoza na kutunza mahusiano yenu
Mary:
kweli kabisa
Miriam:
jamani tusiongee sana…twendeni
(wanatoka
wanapanda gari lililopambwa vizuri)
Mary: (ameshika
ua kubwa)
Miriam:
(anamchukua mwanae na kumnyonyesha) hivi Vanessa yuko wapi?
Mama Mary:
katangulia kanisani
Miriam:
oh
(Safari
ya kwenda kanisani)
Mary: (anashusha
pumzi)
Miriam:
usiwaze mama utakuwa sawa
Mary:
najua kila kitu kitaenda vizuri
Miriam:
(anacheka)
(Baada
ya mwendo wa muda mrefu kidogo wanafika kanisani)
Mary:
kuna watu wengi sana
Miriam:
unaishi na watu vizuri sana…karibu mama twende ukaungane na mpenzi wa moyo wako
Mary:
ndio mwanangu
(wanashuka)
Miriam:
(anatangulia kama kusafisha njia kabla ya bibi harusi kuingia)
Keddy: (anatabasamu
anapomuona Miriam)
Jeremy:
(anampokea na pamoja wanaelekea altareni)
Vincent:
(anasubiri kwa hamu kubwa) sikutarajia kama Mary atakuwa mke wangu
maisha bwana…ni fumbo zito sana
Colton:
(anatabasamu wakati anamsubiri Vanessa)
Vanessa:
(anakuja)
Colton:
(anampokea mpenzi wake)
Mary: (amesimama
tayari kabisa kwa ajili ya kuingia kanisani)
(Wapiga
picha wako tayari kabisa kumpiga picha bibi harusi)
Mary: (anapiga
hatua huku anatabasamu)
(watu
wamesimama kumkaribisha kwa shangwe nyingi)
Miriam:
oh (kwa Jeremy) mama yangu amependeza sana jamani
Jeremy:
ni mrembo kama wewe
Miriam: oh,
honey asante kwa kunipamba
Jeremy:
usijali (anamuangalia usoni kisha anatabasamu)
Mary: (anafika
altareni anashikwa mkono na Vincent kisha kwa pamoja wanamuangalia mchungaji)
Keddy:
hongera sana Mary…hatimaye na wewe umepata wa kwako…wa maisha
Mary: (anatokwa
machozi ya furaha)
Vincent:
(anatabasamu)
Miriam:
wazazi wangu
Jeremy:
najua
Mchungaji:
(anaanza ibada kwa kukaribishwa waumini kisha anafanya mahubiri kidogo)
sasa tunaingia ibada ya ndoa takatifu
Mary: (anamshika
mkono mume wake mtarajiwa)
Mchungaji:
(anaanza ibada na mwisho anawatangaza kuwa mume na mke) sasa
mmekuwa mwili mmoja sasa ni mke na mume
(watu
wanawapongeza kwa hatua hiyo kubwa)

0 Comments