MUNGU MKUU 57


 

SCENE 57: -

BAADA YA WIKI MOJA: -

HOSPITALI YA WENYE CHANGAMOTO YA AFYA YA AKILI: -

(Miriam na Vanessa wanafika katika hospitali ya vichaa kwa lengo la kumuona Ariana aliyekuwepo hapo kwa mwaka mzima)

Miriam: (kwa nesi wa zamu) habari dada?

Nesi: safi karibu

Miriam: asante

Nesi: enhe…

Miriam: nimekuja kumuona dada yangu

Nesi: anaitwa nani?

Miriam: Ariana Kennedy

Nesi: sawa nifuateni…

(wanamfuata)

Nesi: (anawaongoza njia mpaka katika bustani nzuri iliyopo nje kidogo ya wodi hizo) yule pale anapenda kukaa peke yake hapendi kuongea na mtu yeyote…karibuni

Miriam: asante (kwa Vanessa) twende wifi

Vanessa: twende

(wanamfuata mpaka alipo)

Miriam: (kwa sauti ya utulivu) dada?

Ariana: (anageuka anawaangalia kwa huruma huku afya yake inaonekana kuzorota sana na amekonda sana)

Miriam: dada yangu

Ariana: (kimya)

Miriam: shikamoo dada

Ariana: (anaitikia kwa kichwa)

Vanessa: shikamoo dada

Ariana: (anaitikia kwa kichwa)

Miriam: tumekuja kukuona

Ariana: (kimya)

Miriam: baada ya miezi miwili Colton na Vanessa watafunga ndoa…

Ariana: (kimya)

Miriam: mama na baba yangu tayari wameshafunga ndoa wameenda Sweden kwa ajili ya fungate

Ariana: (kimya)

Miriam: dada bado umenikasirikia?

Ariana: (kwa huzuni huku machozi yanamtoka) hapana nimejikasirikia mwenyewe

Miriam: (kwa huzuni kidogo) dada

Ariana: MUNGU MKUU na ukuu wake nilikuwa ninauona kwako kwa kila tukio baya nililokuwa nakufanyia

Miriam: (anasikitika) lakini bado sikukubali ona alivyoniadhibu

Vanessa: (anashangaa) kwani wewe ni mzima sio kichaa?

Ariana: (machozi yanamtoka) hapana mimi sio kichaa wala nini naogopa kwenda jela (Analia sana)

Vanessa: dada Ariana

Ariana: mimi ni mtu mbaya ona watu wote wazuri sasa hivi mna maisha mazuri mimi naishi kwa uoga sijui kwanini…nilimdhihaki Mungu wangu nikakataa kuuona ukuu wake ona ninavyohangaika mimi jamani

Miriam: hapana dada usiseme hivyo na pia huendi jela dada Ariana

Ariana: (anafuta machozi) kivipi?

Miriam: umekuja utetezi unaosema kuwa ukifanya kila kitu ukiwa una tatizo…la (anashusha sauti kidogo) la kiakili hivyo watakusamehe na mimi nimefuta

Ariana: (kimya kidogo) ndo maana Mungu alikuwa anakupigania una roho nzuri sana nilikutesa sana Miriam

Miriam: najua ila yamepita natamani umjue Mungu na ukuu wake

Ariana: (anatabasamu) nilikataa kukukubali kama mdogo wangu na tatizo langu lilianzia hapo

Miriam: usijali dada hayo yameisha…kesho majira kama haya utakuwa unarudi nyumbani kuna mambo mawili matatu utafata kama utaratibu na baada ya hapo kila kitu kitaisha

Vanessa:  natumaini umejifunza

Ariana: ndio…mdogo wangu Vanessa nimejifunza kuwa Mungu ni mkuu na ni yeye ndo mwenye mamlaka ya dunia hii…nilifanya kosa kubwa sana kumkejeli

Miriam: umekiri kosa na umejitahidi kumkaribisha maishani mwako yeye ni mwenye huruma atakaribia maishani mwako

Ariana: enhe nambie mabadiliko yoyote huko?

Miriam: Colton na Vanessa watafunga ndoa

Ariana: habari njema sana hiyo na mimi ningetulia na mimi ningekuwa kwenye mstari wa kuolewa ila kwasababu ya roho yangu mbaya na mipango mingi isiyo kuwa na faida nipo hapa sina mbele wala nyuma

Miriam: Mungu wetu ni Mkuu na njia zake hazichunguziki hata kwa macho gani usijali Mungu amekuwekea wa kwako wewe mkaribie kaa nae na mkumbushane nae atakupatia kila hitaji la moyo wako

Ariana: amina mdogo wangu naamini itakuwa hivyo…kwa mara nyingine Miriam nisamehe

Miriam: nimeshakusamehe wewe ni dada yangu na ninakupenda sana

Ariana: pamoja na kwamba nilikutesa Miriam?

Miriam: hata hivyo still wewe ni shoga yangu (anatabasamu)

Ariana: oh Miriam… (anamkumbatia)

Miriam: (anamkumbatia pia)

Vanessa: (anatabasamu)

Ariana: njoo wifi yetu

Vanessa: (anaungana nao)

Ariana: asanteni kwa kuja yaani imenipa Amani nilikuwa sina Amani nilikuwa nalia tu

Miriam: ulikuwa umekata tamaa?

Ariana: kabisa

Miriam: hairuhusiwi kukata tamaa hata iweje…wanasema hata kama usiku ni mzito vipi ni lazima pakuche maana yake hata iweje kwamba unapitia shida nyingi Mungu anakupa tumaini ya kwamba patapambazuka na hayo matatizo yataisha tu dada yangu ni mwaka umekuwa kwenye matatizo sasa pamepambazuka na yote hiyo sifa na utukufu mrudishie yeye sifa na utukufu kwa UKUU wake na kwamba amefanya makuu

Vanessa: Miriam alikuwa dada yao Mussa na Haruni na unajua sifa ya Miriam?

Ariana: mimi sijui

Miriam: hata mimi…

Vanessa: Miriam alikuwa ni mwana sifa…nakuona na wewe unavyompa Mungu sifa zake

Miriam: ni kwasababu nimeuona mkono wake na matendo yanayodhihirisha kuwa yeye ni MKUU…oh Namapenda Mungu wangu sijui nimrudishie nini kwa mambo makuu aliyonitendea

Vanessa: kwakweli hata utoe nini hautaweza kumrudishia Mungu…hatuna budi kuendelea kusema UKUU wake kwa vizazi na vizazi

Ariana: hakika…(anatabasamu) na mimi nitakuwepo kwenye harusi ya Colton na Vanessa 

Miriam: bila shaka kabisa

Vanessa: kwa uwezo wa Mungu wetu nitaka kuona watu wakifurahi sana siku ya harusi yangu

Miriam: na itakuwa hivyo dear wifi

(wanacheka)

Ariana: (anatabasamu na anaonekana ana tumaini jipya)

Post a Comment

0 Comments