MUNGU MKUU 60 (MWISHO)


 

SCENE 60: -

LONDON UINGEREZA: -

FUNGATE LA MIRIAM NA JEREMY (HONEYMOON)

(hali ya ubaridi Fulani mtulivu umetambaa katika jiji maarufu duniani pande hizo za kwa malikia Elizabeth, Miriam amesimama peke yake huku anaonekana kufurahi mandhari na hali ya hewa ya jiji hilo)

Miriam: oh, nimepapenda sana huku…ni pazuri Sanaa

Jeremy: (anakuja kwa nyuma yake na kumkumbatia) baby

Miriam: baby

Jeremy: (anampaa kinywaji)

Miriam: baby unajua kuwa mimi sinywi pombe

Jeremy: unajua hata mimi sipendi nawala sinywi pombe hii ni shampeni na walaa haina kilevi

Miriam: kama ile tuliyokunywa kwenye sherehe ya harusi yetu?

Jeremy: yes, my love

Miriam: (anapokea) asante sana baba G

Jeremy: usijali mpenzi wangu…mke wangu

Miriam: (anacheka kisha anakunywa kidogo) mmh tamu

Jeremy: najua ni tamu sana… (anacheka kisha anamkumbatia) tupange kupata mdogo wake G maana G tulimpata kwa bahati mbaya…

Miriam: jamani mume wangu mtoto wetu ndo kwanza ana miezi sita

Jeremy: najua mke wanagu ila sasa haitakuwa bahati mbaya itakuwa ni ndani ya ndoa haitakuwa kama kipindi kile

Miriam: (anacheka) najua ilikuwa tulizidiwa sana siku hiyo (anacheka) huwezi kuamini nilikuwa nawaza labda utaniacha

Jeremy: siwezi…na nisingeweza…tangu siku ile nimekuona mara ya kwanza nilijisemea kuwa nitafanyakila kitu ili uwe mke wangu (anacheka) kuna mara nyingine nilikuwa nafunga kuombea huu uhusiano uishie kwenye ndoa

Miriam: hata mimi nilikuwa nafunga…nilijua tu kuwa MUNGU wetu sio kiziwi atatufikisha ona sasa ametufikisha

Jeremy: kabisa…

Miriam: nakupenda Jeremy

Jeremy: hunizidi… naahidi kuwa nitakupenda sana mpaka basi…(anamkumbatia) G kalala tumtafute mdogo wake

Miriam: mume wangu tuenjoi kwanza hali ya hewa ya mji huu…kwanza utanipeleka kwenye jumba la kifalme?

Jeremy: nitakupeleka mke wangu, nitakupeleka na Mexico kwa wale waigizaji unaowapenda kisha tutaenda New York kisha Canada na kama utapenda kwendaa China na Dubai nitakupeleka

Miriam: asante sana mume wangu...namuwaza sana dada yangu

Jeremy: sh... sh... usimuwaze mtu yeyote tafadhali huu ni wakati wetu mpenzi

Miriam: (anazungusha mikono yake mabegani kwa mumewe) sawa ila usiseme mtoto wetu G ni wa kimakosa…mume wangu mtoto wetu ni matunda ya penzi letu haijalishi tulimpataje jibu ni kwamba yeye ni zawadi kubwa sana tuliyopewa nay eye aliye MKUU kuliko vyote na huyo ni MUNGU

Jeremy: yes, my wife…nisamehe kama nimesema vibaya mpenzi…ni kweli mtoto wetu ni zawadi na matunda mazuri ya penzi letu

Miriam; (anambusu)

Jeremy: (anarudisha busu kwa mahaba mazito)

Miriam: I love you my king

Jeremy: I love you my queen

(wanakumbatiana kwa mahaba mazito)

Glory: (anacheza cheza)

Miriam: (anamuona) G kaamka

Jeremy: hana muda na sisi…

Miriam: (anacheka) hata mimi namuona hana muda na sisi

Jeremy: (anambeba mkewe)

Miriam: (anacheka) jamani Jeremy

Jeremy: asante Yesu Miriam ni mke wangu sasa

Miriam: (anacheka)

Jeremy: (anamlaza kitandani)

Miriam: (anatabasamu)

Jeremy: all that is well ends well…all is well kwa UKUU wa MUNGU

Miriam: namuomba Mungu awe na sisi daima na daima

Jeremy: (analala pembeni yake) love you baby

Miriam: I love you

Glory: (Analia kwa nguvu)

Miriam: oh Glory

(wanacheka)

THE END

Miriam na jeremy wanaendelea kuishi kwa amani bila kuogopa kitu chochote, wanapata watoto wengi kadri ya jinsi walivyopenda na Mungu alivyowajalia , Mary na Vincent wanafanikiwa kupata mtoto mwingine wa kike ambae ni mdogo wake Miriam na Colton, Colton na Vanessa wanabarikiwa watoto pia na wanaishi kwa Amani na upendo.  baada ya muda mrefu hatimaye Ariana nae Mungu anamsaidia anapata mume anaolewa na kuzaa watoto mapacha, kila mtu anaishi vizuri kadri alivyoomba kwa Mungu.

Post a Comment

0 Comments