MUNGU MKUU 59


 

SCENE 59: -

BAADA YA MIEZI MIWILI

SIKU YA HARUSI YA MIRIAM NA JEREMY: -

(Asubuhi ya siku muhimu sana ambayo ilikuwa inasubiriwa na sio miriam na Jeremy tu bali kwa kila mtu aliyekuwa anawafahamu wawili hao. Miriam na rafiki zake wamekaa katika chumba maalumu wakijiandaa kwa ajili ya kwenda kanisa. Miriam amevaa gauni malumu la kujiandaa kwa ajili ya vazi maalumu kwa ajili ya harusi)

Miriam: (anakunywa kinywaji chake)

(kila kitu kinaonekana ni cha gharama sana ni kwasababu ya uwezo mkubwa wa kifedha alionao Jeremy yaani mume mtarajiwa wa Miriam na baba yake mzazi Miriam)

Miriam: oh, Mungu wangu asante kwa kunionyesha UKUU wako kila wakati katika maisha yangu…kila mara ulitembea na mimi asante sana Mungu wangu

Mtoto wa kiume: (kati ya umri wa miaka 5 mpaka 7 anakuja) hodi

Dada1: oh, karibu nini tena?

Mtoto: (anampa mfuko mdogo) nimeambiwa nimpe mama G

Miriam: nipo hapa nani amekupa (ananyanyuka na kumfuata)

Mtoto: nimepewa na baba G

Miriam: oh, asante sana (anauchukua anafungua ndani) kuna nini?

Ariana: fungua sasa...

Vanessa: fungua tuone

Miriam: tulieni sasa

Mary: angalieni tusichelewe kanisani

Miriam: (anafungua anakutana na mkufu wa dhahabu wa thamani na saa ya gharama sana) oh My God

Ariana: wow

Mary: wacha we

Miriam: (anaangalia ndani) kuna karatasi kama barua ya mapenzi sijui (anacheka)

(wanacheka)

Mary: hiyo soma mwenyewe

Vanessa: naomba nikiri wifi kuwa natamani uisome kwa nguvu lakini acha niseme tu mama yupo sawa kabisa kwamba ni lazima usome peke yako

Miriam: okay ngoja nisome basi (anaifungua) oh Jeremy (ananza kuisoma) mama G, kipenzi changu, jina la bwana lihimidiwe na acha Mungu aitwe Mungu na nitamtukuza Mungu siku zangu zote za maisha yangu kwa sababu ya UKUU wake…nilipokuona kwa mara ya kwanza miaka kama miwili iliyopita nafsi yangu ilikiri wazi kuwa ni wewe na wewe pekee ndo chaguo langu…penzi letu lilikuwa sio lenye kuwezekana ila kwa UKUU wake alitupigania mpaka tukawa wapenzi tena kwa Baraka za baba na mama na mama mzazi na wazazi wangu lakini shetani aliingilia kati hatukukata tamaa tulipambana hata magumu yalipotufika ulitaka kukata tamaa lakini penzi letu lilishinda mpenzi wangu…kwa UKUU wake tulimpata mtoto wetu…mtoto ambae ni matunda ya penzi letu…asante mpenzi kwa kukubali kusafiri pamoja na mimi kwenye hii safari tuendelee kumsihi Mungu atembee na  sisi..nakupenda sana Miriam nitakuona kanisani ambapo tutaunganishwa mpaka kifo kitakapotutenganisha.,nakupenda sana my love…I cant wait to spend the rest of my life with you baby.

Ariana: oh Miriam

Miriam: (anafurahi sana) yaani hamjui baba G ameniambiaje kwenye hii barua

Mary: kasemaje mbona unatuogopesha

Miriam: oh mama

Mary: nini?

Miriam: ananipenda…

Ariana: jamani tunajua hilo…

(wanacheka)

Keddy: (anakuja) jamani (anamuona Miriam) usiniambie lile gauni la Uturuki ndo hilo…

Miriam: no mama…(anacheka) hilo hapo

(Gauni la gharama tena lenye mkia mrefu limening’inizwa juu)

Keddy: Oh My God…

Miriam: vipi?

Keddy: it is so beautiful…utapendeza sana…

Miriam: ngoja nivae

 (wanamsaidia)

Mary: wow…haya twendeni

(wanaondoka)

Miriam: (amependeza sio utani)

(Baada ya dakika kadhaa wanafika kanisani ambako tayari kuna watu wameshafika na miongoni mwa watu wale yupo Jeremy yaani bwana harusi)

Vincent: (kwa Ken) naomba umsindikize Miriam kwa mumewe

Ken: wewe ni baba yake…

Vincent: wewe ndo baba yake naomba umpeleke mtoto wetu kwa mumewe

Ken: sawa…asante sana...

Vincent: hapana wewe ndo asante sana…asante kwa kumlea mwanangu kwa miaka 19 Mungu akubariki sana

Ken: usijali ndugu yangu (anamkumbatia)

Mary: (kwa Keddy) haya mshike mkono mwanao...umsindikize kwa mumewe

Keddy: (anamshika mkono Miriam)

 Miriam: (anatabsamu) G yuko wapi?

Mary: yupo na mjomba wake usijali

Miriam: okay…twendeni sasa

(mlango unafunguliwa)

Miriam: (akiwa ndani ya gauni matata anaachia tabasamu ang’avu mara baada ya kuwaona watu)

Watu: (wanafurahia uzuri wa Miriam)

Jeremy: wow…this is the woman that I want to spend the rest of my life with…my dearest little mama

Miriam: (anatabasamu mara baada ya kumuona Jeremy wake)

Jeremy: (anang’ata midomo) God made my woman just like the way I imagined

Miriam: (akiwa sambamba na wazazi wake wa kufikia taratibu wanaekekea alipo Jeremy)

Jeremy: come my love…come and make the world believe in the existence of God of  amd  that everything is possible with God

Miriam: (anajongea alipo Jeremy)

Jeremy: (anatabasamu)

David: (anatabasamu)

Mama Jeremy: mwanangu hatimaye umepata yule uliyemtaka mwanangu nah ii ulifanya mwenyewe ulituomba tukutafutie mke siku umeenda kumuona mke ukakutana na mwanamke wa maisha yako na sasa unaenda kumfanya kuwa mama wa familia yako (anatabasamu)

Miriam: (anafika alipo Jeremy anamshika mkono)

Ken: (anamkumbatia Jeremy) take care of our princess…

Jeremy: she is my queen papa I will always take care of her…

Keddy: (anatabasamu)

Mary: (amekaa walipo waumini wengiine) mwanangu… (anatabasamu)

Vincent: (anamuona) mwenzetu vipi mbona unatabasamu mwenyewe?

Mary: nimefurahi…mwanangu kapendeza jamani…asante kwa yote mume wangu

Vincent: hapana mimi mbona sijafanya kitu?

Mary: Vincent…

Vincent: ona wameanza tulia

Jeremy: (anamshika mkono Miriam)

Miriam: (anamshika mkono pia)

(kwa pamoja wanamgeukia mchungaji)

Mchungaji: (anatania) mbona mmependeza sana

Watu: (wanacheka)

Jeremy: (anacheka pia)

Mchungaji: bwana Yesu asifiwe kanisa

(wanaitikia)

Mchungaji: leo tumekusanyika hapa kushuhudia muungano wa wawili hawa Jeremy David na Miriam Vincent Mshana

Watu: (wanasikiliza kwa umakini)

Mchungaji: (kwa Jeremy) Jeremy je unamchukua Miriam kuw mke wako wa maisha kwamba utamtunza, kumpenda na kumthamini siku zote za maisha yako mpaka pale kifo kitakapowatenganisha?

Jeremy: kwa moyo wangu wote ndio

(watu wanashangilia)

Mchungaji: (kwa Miriam) Miriam je unamchukua Jeremy kuwa mume wako kwamba utampenda na kumheshimu katika shida na raha mpaka pale kifo kitakapowatenganisha

Miriam: kwa moyo wangu wote ndio

(watu wanashangilia)

Mchungaji: basi kwa ukiri wenu naomba pete ili zoezi hili likamilike

(zoezi la pete linaendelea na hatimaye wawili hao wanatangazwa kuwa mume na mke)

Mchungaji: na sasa ni bwana na bibi Jeremy David

(Watu wanawapongeza sana, maharusi wanasaini vyeti vya ndoa wanapomaliza wanavionyesha kwa watu ili waone)

Colton: (anampeleka Glory kwa mama yake)

Miriam: oh, my baby...

(wanapiga picha za ukumbusho na kila mmoja wao anaonekana kufurahia yale yanayoendelea mahali hapo, wale wapenzi waliopitia magumu mengi n abado wakasimama imara sasa ni wanandoa na wazazi wa mtoto wa kike kweli MUNGU MKUU akiamua kwa ukuu wake inatokea kama ilivyo wa Miriam na Jeremy.Picha zinaendelea kupigwa na watu mbalimbali na Miriam anaonekana kufurahi sana lakini furaha yake haishindi ile ya mumewe mpenzi)

Jeremy: we did it my love (anamkumbatia mkewe)

Miriam: yes my love with God’s greatness we did it (anamkumbatia)

Post a Comment

0 Comments