ON MY WEDDING DAY 08


 

SCENE 8: -

(Edwin yupo nyumbani kwake na anaonekana wala hana dalili ya kutoka nyumbani siku hiyo, anavuta sigara huku anakunywa kinywaji kikali yaani pombe, na anaonekana ana hasira sana na mawazo pia)

Edwin: dah!!yule demu ni bonge la demu sijui Patrick alimtoa wapi kudadeki…demu mkali sana, namtaka kwa udi na uvumba yaani sijawahi kuvutiwa na mwanamke kama nilivyovutiwa na huyu dada sijui kwanini sikumuona mapema jamani, ila sio mbaya ngoja nipate msaada kwa yule rafiki yake (anachukua simu yake kubwa aina ya iphone na kumpigia Monica, inaita kwa muda kisha inapokelewa)

Monica: hello…

Edwin: Yes, mrembo…mambo.

Monica: poa nani?

Edwin: Edwin, rafiki yake Patrick

Monica: aaah!!!Sawa vipi za toka Jana?

Edwin: nzuri…za kwako?

Monica: ah!!!Tunamshukuru Mungu Kwa wema wake tunaendelea vizuri

Edwin: sawa kabisa…uko wapi?

Monica: nyumbani kwangu

Edwin: wapi?

Monica: mkolani

Edwin: mkolani?

Monica: ndio...

Edwin: samahani unaweza kupata nafasi ukaja nyumbani kwangu? nina mazungumzo na wewe kidogo

Monica: mazungumzo gani tena jamani mbona unaniogopesha? ya kheri hayo?

Edwin: ya heri kabisa kuwa na Amani

Monica :( anaguna kidogo)

Edwin: we njoo wala usijali sio mabaya Sana

Monica: sawa…ila nakujaje? Maana sina hata nauli wala sipajui kwako

Edwin: hiyo niachie Mimi usiumize kichwa mrembo namtuma dereva wangu sasa hivi atakupitia hapo muda si mrefu

Monica: poa…atanikuta

Edwin: poa (anakata simu kisha anaenda nje kumuita dereva wake) Raphael…

Raphael: naam…

Edwin: njoo nikuagize

Raphael :( anamuendea) nambie…

Edwin: nenda mkolani…nakupa namba ya dada Fulani utaenda kumleta

Raphael: shemeji nini?

Edwin: hapana rafiki yake... (Anatabasamu)

Raphael: wewe nae mtata…

Edwin: kwanini?

Raphael :( anachukua simu yake) haya taja namba

Edwin :( anamtajia)

Raphael :( anamaliza kuandika kisha anaweka simu mfukoni mwake kisha anaondoka)

Edwin :( anarudi ndani, anakaa kwenye sofa safi, anawasha na runinga kubwa iliyobandikwa ukutani kwake kisha anaanza kufurahia muziki)

BAADA YA NUSU SAA

(Dereva anamleta Monica katika jumba Safi la Edwin, Monica analishangaa sana jumba lile ni kubwa zuri, kuna walinzi kuna watumishi mbalimbali anaonekana kuvutiwa)

Monica :( anajisemea moyoni) bonge la jumba lakini ya Patrick ndo basi kabisa

Raphael: karibu dada…boss yupo huku (anamuongoza njia)

Monica :( anamfuata)

(Wanafika alipo Edwin)

Edwin: oh…Monica eeh

Monica: ndio Monica

Edwin: karibu nyumbani kwangu...Kwenye himaya yangu

Monica: Asante Sana (anaangaza huku na huku) yeah…pazuri sana

Raphael :( anatoka nje)

Edwin: kadada…embu njoo umsikilize...Mgeni

Kadada :( anakuja)

Monica: Mimi juisi tu…mdogo wangu

Kadada: sawa (anaelekea jikoni)

Edwin: sawa nambie…rafiki yako hajambo? (Anang’ata midomo)

Monica :( anacheka kidogo)

Edwin: mbona unacheka sasa

Monica :( anacheka kidogo) unaonekana umempenda Sana

Edwin: siwezi kudanganya…ni kweli kabisa nampenda mno

Monica: si mpenzi wa rafiki yako

Edwin: I do not care

Kadada :( analeta kinywaji anamkaribisha kisha anaondoka)

Monica: Eddy?

Edwin: yaani nampenda Olivia kupita kiasi na kitu kilichonifanya nikuite hapa leo ni hicho…unanisaidiaje nimpate Olivia?

Monica :( anacheka)

Edwin: ukinisaidia nitakupa pesa na kukupangia chumba kizuri na hata biashara nisaidie tu kumpata Olivia

Monica: hata Mimi namtaka Patrick

Edwin :( anatabasamu huku anatikisa kichwa ishara ya kukubali) hapo sasa umenena…

Monica: namtaka Patrick kuliko hata unavyomtaka Olivia…

Edwin: hapo sasa ndo tunaongea lugha moja rafiki yangu

Monica :( anacheka kidogo)

Edwin: nini kifanyike?

Monica: nakusikiliza

Edwin:(anatabasamu kidogo) tuwagombanishe wachukiane milele, yaani tutafute kitu ambacho hawajawahi kuambiana kwa mfano mimi nina kitu kimoja ambacho nakijua kuhusu Patrick na nina uhakika hajawahi kumwambia olivia nina uhakika

Monica: nini hicho?

Edwin: hapa sasa ndo nahitaji msaada wako, Patrick aliwahi kuwa muuza madawa ya kulevya miaka mingi iliyopita na aliwahi kufungwa South Africa, wazazi wake walimtoa na alipotoka hakuwahi kuyauza tena ndo wazazi wake wakafanya mpango wa kumpa biashara ya madini

Monica :( anashangaa) aisee…

Edwin: ndo hivyo ulikuwa bonge la msala sema pesa za wazazi wake zilimuokoa…yaani angenyongwa yule

Monica :( anashangaa)

Edwin: Nina uhakika hajawahi kumwambia Olivia…na ni vitu vya muhimu sana hasa pale unapoanza mahusiano na mtu…ni vyema ukamwambia

Monica: sasa mimi nitamwambiaje Olivia?

Edwin: si katika stori…unajifanya nimeshakuwa mtu wako…kwamba nikakwambia ukweli juu ya maisha yangu tukajikuta tunamzungumzia Patrick ndo tukaongea hayo…ila mwambie asitutaje kwa Patrick

Monica: sawa…Hilo ni wazo zuri sana…

Edwin: yes, na ninavyojua wanawake huwa hawapendi kufichwa kitu na wapenzi wao

Monica: kabisa na hivyo basi…nitaenda kesho kwa Olivia

Edwin: akivunjika moyo Mimi ndo nitamtuliza Kwa kisingizio cha shemeji, shemeji…halafu mwisho wa siku ataingia tu mkenge, wakati huo na wewe jitahidi kuwa karibu na Patrick halafu mwisho wa siku atakuwa wako

(Kwa pamoja wanagonga glasi na kufurahi sana)

Monica: hatimaye, Patrick atakuwa wangu

Edwin: na Olivia atakuwa wangu…yaani hawataamini kuwa wanaachana kizembe hivyo

Monica: wanajifanya kupendana sana utasema wao ndo wa kwanza kuwa na mahusiano

Edwin: kumbe na wewe sio mtu wa mchezomchezo eeh…

Monica: sio kidogo rafiki yangu

Edwin: cheers

Monica: cheers… (Wanagonga glasi)

Edwin: oh…Patrick my brother, Olivia sio wako tena nishamchukua

Monica: Olivia, Patrick sio wako tena ni wangu na nishamchukua

(Kwa pamoja wanacheka Sana na kushangilia ushindi ambao bado haujawa, wanaendelea kunywa na kucheka kwa muda mrefu sana)

Monica: hii ni kwa ajili ya ushindi wetu…

Edwin: yes…

Monica :( anacheka)

Edwin: yes…

Monica: kumbe Patrick ana dark past

Edwin: yaani halafu alikuwa anauza na kuyatumia, amehenyesha watu yule kuwabebesha watoto wa watu madawa matumboni mwao

Monica: sipatii picha Olivia atakavyochukia

Edwin: Nina uhakika kuwa atakasirika sana

Monica: Sana maana ni mlokole huyo atahisi labda bado Patrick anayauza yaani itakuwa mtafaruko

Edwin: si ndo tunaoutaka kwao

Monica: wewe sio wa mchezo baba

Edwin: usinichezee

(Wanacheka huku wanagonga glasi)

Post a Comment

0 Comments