SCENE
9: -
(Monica
anafika nyumbani kwa kina Olivia, anapofika nyumbani hapo anagonga mlango na
haraka Olivia anafungua mlango)
Olivia:(anafungua
mlango, anatabasamu mara baada ya kumuona rafiki yake) Monica, karibu shoga
yangu…
Monica:(huku
anaingia) asante shoga yangu…
(wanafika
sebuleni, wanakaa kwenye sofa za gharama zilizopo sebuleni hapo)
Olivia:
nambie unatumia kinywaji gani?
Monica:
maji tu shoga yangu
Olivia:(anatabasamu)
poa… (anaenda jikoni)
Monica:(anabenjua
midomo kisha anafyonza)
Olivia:(anarudi
akiwa amebeba glasi mbili za maji moja anampa rafiki yake huku nyingine
akiitumia yeye) enhe (anakunywa kidogo) nambie…shemeji anasemaje?
Monica:(anakunywa
kidogo) ah…Edwin?
Olivia:
sasa je au una bwana mwingine shoga yangu?
Monica:
ah…wapi nina yeye tu...hana usemi anakusalimia…sana
Olivia:(anacheka
kidogo) kweli eeh…hata mimi namsalimia pia (anacheka tena)
(kimya
kidogo)
Monica:na
wewe shem anasemaje?
Olivia: utamuweza?
yupo tu...
Monica:
mnaendelea vizuri tu…
Olivia:
sana…
Monica:
vizuri sana… (anajisemea moyoni) muda wa kuendelea vizuri umeisha
mama…namtaka Patrick ili anifanyie haya aliyokufanyia Olivia...
Olivia: vipi?
mbona kimya ghafla?
Monica:
sina cha kuongea tena ndugu yangu
Olivia:(anacheka)
Monica:
kwahiyo mnaaminiana sana na hakuna mnachofichana
Olivia:
hamna kitu tunachofichana...ananiambia kila kitu yaani ananipenda kweli na
hanifichi jambo...si unajua tunaandana kuwa wanandoa
Monica:
hata wewe ile inshu ya yule mzee kukuchumbia kisha kukuacha kwenye mataa nayo
umemwambia
Olivia:
hilo nilimwambia hata kabla hatujaanza mahusiano kipindi hicho ndo tunachati
kama marafiki
Monica:
kumbe…basi kumbe mnaaminiana sana
Olivia:(anacheka)
na kupendana pia…nampenda Patrick na kumheshimu sana na Zaidi namuamini sana
nay eye ananiamini sana…
Monica:
basi vizuri…kumbe hata aliwahi kukuambia kuwa aliwahi kuuza na kutumia madawa
ya kulevya? akakamatwa huko South Africa?
Olivia:(anashtuka
sana) alikuwa anauza madawa ya kulevya …na kutumia pia? mbona hakuniambia
hili?
Monica…dah!!!sasa
utasemaje kuwa mnaaminiana na kuambiana mambo yenu yote mbona mwenzio
anaonekana hakuamini na kukuficha?
Olivia:
siamini kabisa kwa kitu unachoniambia…Patrick anajifanya kunipenda kumbe
ananificha mambo yake
Monica:
ila naona kuwa sio kosa kubwa sana
Olivia:
inategemea na jinsi tulivyowekeana, tumewekeana kuwa tunaambiana kila kitu… (anachukua
simu yake na kupiga) ngoja nimpigie… (ananyanyuka na kwenda zake
chumbani kwake) Patrick...
Patrick:
mwanamke…nambie mpenzi wangu
Olivia:(anaonyesha
jazba) jamani Patrick kwanini hukuniambia kuwa uliwahi kujihusisha na
madawa ya kulevya
Monica:(anamchungulia
kwa mbali) kimewaka(anatabasamu)ngoja nimwambie Edwin (anapiga
simu kwa Edwin, simu inaita hatimaye inapokelewa) kimewaka huku…
Edwin:
usiniambie…
Monica:
sana…Olivia kakasirika mi namjua huyu hapendi uongo sana
Edwin:
safi…sana… (anakata simu)
(kwa
Olivia)
Olivia:
Patrick unajua kuwa nachukia uongo
Patrick:
tulia nakuja tuzungumze
Olivia:
hapana Patrick we ni mtu hatari nitajuaje kuwa hauzi tena hayo madawa? Sitaki
kukuona tena sitaki kukuona tena, Patrick…it is over…
Patrick:
usinifanyie hivyo Olivia…wewe mwenyewe unajua navyokupenda…ni kosa ndio lakini
sio kosa kubwa la kufanya penzi letu likaharibika…mpenzi wangu...
Olivia:
niache Patrick… (Anakata simu)
Patrick
:( anampigia) pokea simu tafadhali…
Olivia:
yaani amenifanya mimi mtoto mdogo ananificha mambo yake pengine anaendelea kuyauza...Siwezi
kuwa na mwanaume muuza madawa ya kulevya... (Anarudi sebuleni)
Monica:
vipi shoga yangu?
Olivia:
nimeachana na Patrick…yaani simtaki maana kama amenificha inamaana kuwa bado
anayauza na sitaki kuolewa na mwanaume muuza madawa ya kulevya
Monica
:( anacheka chinichini, akiangaliwa na Olivia anajifanya kuhuzunika)
Olivia:
yaani wanaume
Monica:
yaani waache tu…wapo kama wamezaliwa na baba mmoja, ila mimi nimeambiwa kila
kitu na Edwin na kwamba walikuwa wanauza madawa ya kulevya ila kwa sasa wote
wameacha na aliongea hivyo akijua labda tayari ameshakuambia
Olivia:
hajaniambia na labda ni kwasababu anaendelea kuuza madawa hayo, mi nitatoa
taarifa polisi asilete utani na mimi
Monica:
muache usimsemee mwenzio jamani
(Baada
ya dakika chache mlango unagongwa, haraka Olivia anaenda kufungua anakuta ni
Patrick, anaufunga mlango)
Monica
:( anajisemea moyoni) ah…huyu nae amekuja kufanya nini?
Olivia:
naomba uondoke nyumbani kwangu…Patrick nadhani nimeshakuambia kuwa sitaki
mahusiano na wewe na kila kitu ulichonipa nitakurudishia...
Patrick:
jaribu kunisikiliza...Olivia…ni kweli
Olivia:
too late Patrick...Siwezi kukusikiliza tena…iam sorry we endelea tu na maisha
yako uliyoyachagua…
Patrick:
don’t panic my love embu kaa utulie…tafakari
Olivia:
haina haja ya kutafakari chochote Patrick…it is over basi…ngoja nifunge kila
ulichonipa kesho nitakuletea nyumbani kwako…
Patrick:
haina haja kurudisha nilivyokupa
Monica :(
anacheka chini chini)
Olivia:
nilikupenda Sana Patrick…lakini badala yake ukawa unafanya mambo bila ya mimi
kujua…it is over Patrick…nimeachana na wewe…Monica
Monica:
abeeee….
Olivia:
mwambie Patrick aondoke…
Patrick
:( anaondoka kimya kimya)
Olivia
:( anajikuta anapata uchungu) hivi unajua kuwa Patrick alikuwa mbioni
kuja kunichumbia ili anioe?
Monica:
dah…sasa si umsamehe mwenzio kakosa kenyewe kadogo hivyo jamani?
Olivia:
Siwezi…na hilo kosa sio dogo…nimemuacha kuanzia sasa hivi
Monica:
utamwambiaje mama yako?
Olivia:
nitajua mwenyewe…iam sorry naomba Kama hutojali naomba nibaki peke yangu…
Monica:
bila shaka rafiki yangu (anabeba mkoba aliokuja nao na kuondoka zake)
kwaheri
Olivia: poa…tutaonana
(anaingia zake chumbani kwake)
Monica
:( anatoka nje kisha anampigia simu Edwin inaita kisha inapokelewa)
hello…Edwin…wameachana kabisaaaa
Edwin:
Safi sana…cha kuombea usiku wasiongee maana wanaweza kuyajenga
Monica:
ndo hivyo…
Edwin:
kesho asubuhi…nenda kwa Patrick na mimi kwa Olivia…tutajifanya tunawapooza
kujenga urafiki na hatimaye mapenzi…
Monica:
ndo hivyo…hongera mume mtarajiwa wa Olivia
Edwin :(
anacheka kidogo) Na wewe hongera mke mtarajiwa wa Patrick…
(wanacheka
kisha wanakata simu Kwa pamoja)
Monica:
pole Sana Olivia… (Anacheka kisha anaendoka zake)
(Upande wa Olivia bado anaonekana ana hasira juu ya
habari ya Patrick)
Olivia:
yaani Patrick jamani mbona anaonekana mstaarabu halafu aliniambia kuwa yeye ni
mlokole au nalo ni kwasababu anajua mimi ni mlokole kaamua kuniingia hivyo?
namchukia kama ndo mipango yake ndo hiyo(Analia )jamani shetani
huyu…kwanini kila nikifika hatua nzuri na mwanaume ni lazima mambo yaharibike?Patrick
mpenzi wangu jamani(Analia)nimeachana nae na sijui kama kuna uwezekano
wa kurudiana na yeye naumia sana mahusiano yetu yameisha pamoja na ahadi nyingi…(Analia)je
anaweza kuwa bado anayauza ndo maana haniambii?je nimshtaki…au ngoja nimuache
tu maana nampenda na wala sitataka kumuona akiwa na matatizo yoyote…lakini
kwanini nimempenda mwanaume ambae ni tishio kwa jamii?
Mama
:( anamuangalia Kwa mbali na anahakikisha uwepo wake haugunduliwi na Olivia)
huyu mtoto ana nini jamani mbona Analia? Sipendi kumuona Analia sijui nini…nitamuuliza...Ngoja
atulie (anaendelea na shughuli zake)
Olivia
:( anaendelea kulia Kwa uongo wa Patrick) najua mpaka leo atakuwa
anayauza..Hajaniambia tu…sasa mwanaume wa hivi ni mtenda dhambi na sipo tayari
kuwa nae, its over Patrick huna tena nafasi kwangu nakuchukia sana
(Upande wa Patrick amekaa kwenye gari yake na
anaonekana ana mawazo sana)
Patrick:
dah!!!Olivia amechukia sana kwa kitendo cha kutomwambia ukweli wote wa maisha
yangu ningejua basi ningemwambia kila kitu...na ninamjua aliyewaambia yote
hayo…ni Edwin yamkini alikuwa anaongea tu na mpenzi wake kama kuongea lakini
kwa kuwa wanawake wamebobea kwenye umbea basi Monica kampelekea umbea kwa mpenzi
wangu…usijali mama wewe punguza hasira nitarudi kuongea na wewe (anawasha
gari kisha analiondoa)
(Upande wa Olivia)
Olivia:
nakupenda Sana Patrick mpenzi wangu
Patrick:
nakupenda Sana kipenzi changu…nakujitaji bado
Olivia:
ila nakuchukia umenidanganya eti wewe mlokole kumbe muuza madawa nachukia uongo
(Analia)
Patrick:(bado
anaendelea kuendesha gari lako) nakupenda Olivia utaendelea kuwa wangu
Olivia:(akiwa
bado amekaa chumbani kwake) madawa ya kulevya si yanaweza kuua mtu? kwahiyo
Patrick alikuwa muuaji? (Analia)
(Patrick anaendelea kuendesha gari lake kuelekea
nyumbani huku Olivia bado Analia)

0 Comments