IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 10

 


SCENE 10: -

(Raymond anaingia ofisini kwake akiwa Ni mtu mwenye furaha Sana, anaketi kwenye kiti chake anachukua simu ya mezani na kumpigia sekretari wake)

Raymond: Glory…naomba uniletee lile faili la Jana tafadhali…

Glory: sawa boss... (Ananyanyuka anachukua faili Hilo na bila kupoteza muda anaingia ofisini kwa Raymond akiwa ameshika faili) habari za asubuhi boss

Raymond: nishakwambia usiwe unaniita boss…niite tu kaka

Glory :( anacheka kidogo)

Raymond :( anaimba wimbo Fulani wa dini)

Glory: mbona Leo unaonekana una raha sana?

Raymond: we acha dada...Kwani naonyesha mpaka usoni kuwa Nina raha eeh

Glory: kabisa

Raymond: dada Mungu anajibu maombi Sana unajua eeh

Glory: kwanini?

Raymond: sijui nikwambie? Sijui itakuwa mapema Sana? Anyways, ngoja nikwambie iam in love…

Glory: wow...Kweli na nani?

Raymond: hiyo sasa ni siri yangu kwanza ila we jua kuwa iam in love

Glory: hongera Sana brother au na huyo mkeo mtarajiwa?

Raymond: ah…wapi sio na huyo kivuruge (anacheka)

Glory: una maneno wewe (anacheka)

Raymond :( anacheka)

Glory :( huku anaondoka) ngoja mi niende nisije nikakutwa hapa na mkurugenzi mkubwa hapa ikawa shida (anatoka)

Raymond: poa we kaendelee na kazi acha mimi niwaze (anacheka sana) ahh!!!(anajisemea mwenyewe)nimemkumbuka yule Mrembo…(anatabasamu)mimi nina nini jamani yaani mdada amekuja jana tu leo kanijaa akilini utasema sijui nini?yaani Christina simtamani kabisa yule mwanamke..kanitoka kabisa…lazima nijenge mahusiano na Angelina anaonekana ni mtu mzuri sana na mpenda watu,ngoja nipige nyumbani angalau tu nisikie sauti yake ndo niendelee na kazi zangu(anacheka)jamani ukisikia love at first sight no hii jamani(anachukua simu yake na kupiga simu ya mezani ya numbani kwake,inaita sana bila majibu hatimaye inakata)mbona hapokei?(anapiga tena)ngoja nimjaribu Ramadhani pale getini(inaita kwa muda kidogo tu halafu inapokelewa)nambie Rama kwema hapo?

Ramadhani: kwema za kazi

Raymond: nzuri kaka...Angelina yupo hapo?

Ramadhani: yupo bustanini anamwagilia Maua…vipi?

Raymond: ah!!Poa tu kuna maagizo nataka nimwambie sasa sijui unaweza kuniitia mara moja mtu wangu

Ramadhani: usihangaike Ray…niambie tu nitamwambia

Raymond: muite tu…nimwambie if you do not mind my friend

Ramadhani: sawa haina shida kabisa mtu wangu…kata nimuite halafu nitakupigia hata kwenye simu yangu

Raymond: poa nibipu tu mara moja

Ramadhani: poa (anakata simu kisha anaenda bustanini alipo Angelina) wewe dada…boss anataka kuongea na wewe kwenye simu…

Angelina :( anaacha alichokuwa anafanya kisha anamfata)

Ramadhan :( anambipu Raymond)

Raymond (haraka anapiga inaita kisha inapokelewa) nambie

Angelina: shikamoo kaka

Raymond: marahaba Angelina hujambo?

Angelina: sijambo kaka…za kazi?

Raymond: nzuri tu

Angelina: Ramadhani ameniambia kuwa kuna kitu unataka kuniambia kaka

Raymond :( anashikwa kigugumizi) …yes…ah…vipi umekula? Ah…mchana utakula nini? Au utapika nini?

Angelina :( anacheka kidogo) kaka bwana Jana si uliniambia Leo nipike wali samaki na mboga za majani ndo nitapika hivyo kaka au unataka kubadilisha?

Raymond: hapana hiyo iko sawa mdogo wangu…nilitaka tu kujua Kama uko makini na kwamba husahau kitu…

Angelina: nipo makini kaka yangu

Raymond: vizuri…tutazungumza baada kidogo mdogo wangu

Angelina: sawa kaka…uwe na kazi njema huko ulipo

Raymond: Asante (anatabasamu)

Angelina: Asante kaka

Ramadhani: poa rudisha simu sasa

Angelina :( anamrudishia Ramadhani simu yake kisha anaenda kuendelea na kazi zake)

Ramadhani: haya poa…. (Anamuangalia kwa matamanio) mtoto mzuri huyu mweeeee (anaingia kibandani kwake)

(Huku ofisini alipo Raymond)

Raymond:(anatabasamu) yaani mimi nimekuwa kama mtoto…mapenzi bwana…(anaegemea meza kama vile kujilaza)nampenda Angelina na ninatamani kila saa niwe naongea nae jamani(anaguna kidogo) Edmond akijua si ataniua mimi…embu nijitahidi kuficha…ila hapana cha kufanya nimwambie tu Angelina pamoja na Edmond au itakuwa haraka sana maana napo haraka haraka haina Baraka na mwenda pole hajikwai…ila pia ngoja ngoja huumiza matumbo na pia unaweza ukachelewa ukakuta mwana sio wako sasa nifanyeje na nafsi yangu kweli inakiri kwamba nimempenda sana Angelina na niko tayari kwa lolote,matusi ya baba,vitisho vya Christina ila siko tayari kugombana na rafiki yangu aliyeniaminia akaniletea huyu malaika…nampenda Angelina…I swear nampenda kuliko kawaida…she is the woman that I have always wanted(anatabasamu kidogo)she is beautiful and kind,hardworking,responsible yaani anaweza kuilea familia hata kama hali ni mbaya she is the opposite of Christina…(anakaa vizuri kisha anaendelea na kazi zake)lazima nimwambie mapema kuwa nina mchumba ndio ila nafsi yangu imempenda yeye…(anaguna)lakini atanielewa kweli jamani?ok ngoja nimwambie tu…potelea mbali au ngoja nisubiri kidogo itakuwa haraka sana hiyo(anaendelea na kazi zake kama kawaida)oh My God kwanini siwezi kufanya kazi zangu,namuwaza sana Angelina…huyu binti amenipa nini mimi jamani mbona nakuwa chizi sasa,embu niache ujinga wagonjwa wananihitaji kwa kila hali…natakiwa kuweka akili na nafsi yangu kwenye hii kazi(anafanya kazi)oh no nataka kumuona kabisa hata ikiwa kwa mbali nataka kumuona…(anatafakari jambo)No Raymond embu kaa utulie bwana,huyo ni shemeji wa rafiki yako…ukileta stori za mapenzi hapa itakula kwako na isitoshe wewe ni mume mtarajiwa wa mtu(anajilazimisha kuendelea na kazi)no…ngoja niende nyumbani mara moja nimuone hata kwa mbali(ananyanyua anabeba koti lake la suti)ila mimi mjinga yaani naacha kazi naenda kwa mwanamke…(anajishangaa)kwani huyu mtoto amenipa nini mimi jamani kiasi cha kuwa mjinga hivi(anakaa)ngoja niendelee na kazi zangu nitamuona jioni(anavuta kompyuta yake na kuendelea na kazi)nampenda sana Angelina wangu,ipo siku tutakuwa tu…ngoja niwe mpole na mvumilivu(anaendelea na kazi zake)

Sekretari :( anakuja akiwa amebeba faili lingine) boss umemaliza kufanyia kazi Hilo faili lipo lingine

Raymond: kwanza umerudia kuniita boss huku nimeshakukataza lakini pili hilo faili hata sijaligusa…

Sekretari: kwanza samahani kwa kujisahau na kukuita boss…lakini pili kwanini hujashika faili?

Raymond: naona basi…ile sura ya kipenzi inakuja mara nyingi nyingi kwenye faili

(Wanacheka Sana)

Sekretari :( anacheka Sana) aaah ila wewe hapana…sasa si umpigie simu

Raymond: hana simu

Sekretari: mnunulie wifi simu usilete ujinga

Raymond: eti ee…hiyo ni kweli dada ngoja nimnunulie simu niwe nampigia kila saa ila sasa akipokea sijui nitakuwa nafanyaje

Sekretari: kwanini?

Raymond: huwa napigwa butwaa nikisikia sauti yake

(Wanacheka tena)

Raymond: kiukweli sijawahi kumpenda mwanamke hivi

(Wanabaki wanacheka)

Post a Comment

0 Comments