IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 11

 


SCENE 11: -

(Raymond anarudi nyumbani kwake mara baada ya kumaliza kazi zake za siku, anapofika kama kawaida anafunguliwa geti na Ramadhani ambae ni mlinzi wake na mara baada ya kufunguliwa geti anaingiza gari na kuliegesha eneo la maegesho halafu haraka hata bila kumsalimia Ramadhani anaingia ndani)

Raymond :( huku anakaa kwenye sofa dogo lililopo hapo sebulen) Angelina…

Angelina :( anatokea chumbani kwake) abee kaka

Raymond :( anamuangalia kwa muda kisha anaachia tabasamu zuri)

Angelina :( anatabasamu pia) kaka mbona unacheka?

Raymond: sicheki natabasamu

Angelina: kwanini?

Raymond: nimefurahi kukuona mdogo wangu au siruhusiwi kufurahi nikikuona?

Angelina: wala!!(Anacheka) hata Mimi nimefurahi kukuona kaka, za kazi?

Raymond: nzuri tu…za hapa?

Angelina: nzuri tu

Raymond: umeshapika?

Angelina: ndio kaka, nimemaliza kupika ndo nikaenda kuoga

Raymond: sawa mdogo wangu... (Anavuta begi lake la kazini na kutoa simu aina ya Samsung Note 10 na kumkabidhi)

Angelina: kaka...hii simu?

Raymond: zawadi…nimekuletea zawadi, umefurahi

Angelina: nimefurahi lakini si itakuwa bei sana kaka yangu?

Raymond: kawaida tu dada

Angelina: huo ni Zaidi ya mshahara wangu kaka kwakweli asante ila sitaweza kabisa kuipokea simu ya bei hivi

Raymond: tafadhali naomba uipokee Angelina napenda kuongea na wewe mara kwa mara mdogo wangu

Angelina: kaka

Raymond: ipokee tu

Angelina: Mimi nina malengo mengi sana na mshahara wangu kaka, familia yangu inanitegemea kwa asilimia 80 kaka yangu

Raymond: sitakukata mshahara wako hata shilingi

Angelina: kweli kaka?

Raymond: niamini mimi mdogo wangu (anampa) ipokee tu mama

Angelina :( anaipokea kwa heshima) Asante kaka

Raymond: usijali mdogo wangu

Angelina :( anaifungua) Mimi kitambulisho changu nilikisahau nyumbani labda kesho unipe simu niongee na Catherine anipe cha kwake ili niweze kusajili laini

Raymond: nimeshakusajilia mdogo wangu...Kutumia kitambulisho changu na namba ya kwanza nimeweka ya kwangu nyingine labda ya shemeji itaingia hapo baada ya kwangu

Angelina :( anacheka Sana) ya shemeji?

Raymond: ndio shemeji yangu kwako…kwani wewe huna mpenzi?

Angelina: hapana sina na wala sina mpango wa kuwa nae kwa sasa…nina mambo mengi sana

Raymond: unapika vizuri, una heshima na Zaidi una sura nzuri na umbo zuri utakosa kweli mwanaume au ulikuwa nae ukaachana nae?

Angelina: hapana kaka sijawahi kuwa na mpenzi

Raymond :( anatabasamu) njoo ukae hapa…

Angelina: hapana kaka sitaweza acha tu nisimame

Raymond: kwanini hautaweza?

Angelina: mke wako anaweza akaja ghafla akanikuta nimekaa kwenye sofa la gharama tena na wewe

Raymond: ok... (Anasimama nay eye) tuongee tumesimama

Angelina: kaka kwanini unafanya hivyo?

Raymond: nasimama Kama wewe…

Angelina :( anacheka kidogo)

Raymond :( anatabasamu)

Angelina :( huku anatafuta sofa la kukaa) haya nimekaa

Raymond :( anamfuata alipokaa)

Angelina: kaka si ukakae ulipokuwa umekaa jamani

Raymond: yaani wewe humuogopi Christina Bali uananiogopa Mimi sijui unahisi nitakubaka yaani hauna uhuru kabisa

Angelina: sio hivyo kaka

Raymond: Bali ni nini?

Angelina: haileti tu picha nzuri ulivonisogelea hivyo kaka yangu

Raymond: Mimi mbona nimekusogelea kawaida tu

Angelina: haya kaka tuendelee kuongea

Raymond :( anataka kumshika mkono)

Angelina :( anaogopa)

Raymond :( anajisemea moyoni) huyu shetani ashindwe…huyu ni mke mtarajiwa wangu sitakiwi kumuonyesha udhaifu wangu…

Angelina: kaka nashukuru kwa simu ngoja nikaiweke chumbani kisha nitarudi

Raymond: sawa

Angelina :( anaondoka haraka)

Raymond: nachotakiwa ni kuwa muangalifu sasa nikimuonyesha udhaifu mapema naweza kumkosa

(Huku chumbani alipo Angelina)

Angelina: kwanini kaka Raymond alitaka kunishika mkono? Au alikuwa anataka kunibaka? (Anaguna) kwanini amefanya hivyo, halafu anavyoniangalia jamani ee, Mungu wangu lazima niwe makini yaani sitaki kukaa nae karibu…Mimi hapa ni mfanya kazi za ndani na si vinginevyo

Raymond :( anaenda mpaka mlangoni kwa Angelina na kisha anagonga) hodi

Angelina :( anaogopa) Mungu wangu anagonga…sifungui hata kidogo acha agonge mpaka akome

Raymond: Angel…samahani sijui nini tu kilinijia lakini haikuwa kwa nia mbaya mdogo wangu nisamehe

Angelina :( anajisemea moyoni) yaani (anaguna) wanaanzaga hivihivi we unadhani akishanibaka akanipa mimba atanikumbuka kweli na tayari ana mke huyu (anaguna tena) acha tu nimjibu mbovu ili anikome, au ndo maana amenipa simu…

Raymond: samahani njoo utenge chakula tule

Angelina :( anafungua na kumrudishia simu) kaka asante kwa simu ila naona umetaka kuitumia simu kunichezea

Raymond: hapana Angelina…mimi nimeokoka siwezi kukufanyia hivyo hiyo simu nimekuletea maana unaweza kukuta saa nyingine nataka kukupigia labda unakuwa uko mbali na nyumbani sio kwa ubaya Angelina tafadhali naomba unisamehe, tafadhali, sitaki tugombane maana tunakaa sehemu moja kwanini tukwaruzane kwa vitu vidogovidogo kama hivi? Mimi sipo hivyo mama

Angelina :( anashusha pumzi kisha anaguna kidogo) sasa kwanini ulitaka kunishika mkono kwa mazingira ya utata?

Raymond: ila sijakushika…ningekushika ndo ungelalamika ila sijakushika mdogo wangu

Angelina: sawa kaka, najua hujanishika ila ulitaka kunishika inamaana nisingewahi kukuzuia ungenishika…sawa lakini ila mi naomba tuheshimiane kama kaka na dada…

Raymond: sawa mdogo wangu (anajisemea moyoni) sawa wife… (Anatabasamu)

Angelina: unatabasamu nini?

Raymond: wala…Mimi wala sitabasamu mbona?

Angelina: haya bwana…

Raymond: katenge chakula tuje tule

Angelina :( anaenda jikoni kisha anaanza kutenga chakula mezani) karibu chakula kaka

Raymond :( anaenda mezani)

Angelina :( anamsogezea sahani)

Raymond :( anachukua huku anamuangalia usoni) mbona umenuna Sana?

Angelina: hapana kaka sijanuna…nimeamua tu kunyamaza kuwa na Amani kaka yangu

Raymond: usininunie mdogo wangu

Angelina (anatabasamu kidogo)

Raymond :( anacheka) ewaaaaa!!!Hapo sasa ndo sawa (anacheka tena)

Angelina: sawa bwana

Raymond: kaa basi tule

Angelina: hapana kaka Mimi nakaa jikoni

Raymond: twende…tukakae wote

Angelina: kaka

Raymond: mi najua unaniogopa Mimi sitajaribu kukushika tena chochote we kaa tu na mimi hapa tule

Angelina: haya ngoja nikubali yaishe…tutoke jikoni twende tukakae huko

Raymond: Mimi nataka hapahapa…nimepapenda

Angelina :( anacheka kidogo) yaani wewe una utani mkeo akikuta huku jikoni

Raymond: we nae huachi kumzungumzia mke wangu kila saa mke mke…kuna stori nyingi tu ambazo tukikaa tukazungumza tutafurahia sana kuliko kila saa mke ah!!!Unanichosha

Angelina :( anacheka) basi nisamehe kaka sitamzungumzia mke wako tena, hata Kama ikiwa vipi sitamzungumzia…ila sasa kwanini umekaa jikoni…wakikuta ndugu zako…nitalaumiwa mimi kwanini nimekuruhusu wewe baba mwenye nyumba kulia chakula jikoni

Raymond: nikwambieje kuwa nilipokuwa peke yangu hi indo ilikuwa sehemu yangu ya kulia chakula...

Angelina: haya bwana…ngoja nikubali (anakaa chini sakafuni)

Raymond :( nae anakaa sakafuni)

(Wanakaa pamoja na kufurahia chakula cha jioni, wanaendelea kula huku wanaonekana kusahau tukio la kutaka kushikana viuno, wanacheka wanazungumza kwa ufupi wanaonekana kama mtu labda na mke wake au mpenzi wake maana wanafurahiana kuliko kawaida)

Post a Comment

0 Comments