IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 9

 


SCENE 9: -

(Jioni ya siku hiyohiyo, Raymond anafika nyumbani kwake)

Raymond :( anapiga honi)

Ramadhani :( haraka anafungua geti)

Raymond :( anaingiza gari lake anafika maegesho, analiegesha kisha anashuka kuelekea chumba cha mlinzi) Ramadhani…za jioni ndugu yangu

Ramadhani: salama za kazi?

Raymond: njema tu…yuko wapi Angelina...Simuoni hapa

Ramadhani: yupo chumba cha sinema…anaangalia sinema

Raymond: sawa…ngoja nimuone

Ramadhani: ngoja nikuitie (anataka kwenda)

Raymond: hapana usijali...Nitaenda kumuona… (Anaelekea chumba cha sinema baada ya hatua kadhaa anafika) Angelina…

Angelina :( ananyanyuka kwa kuwa alikuwa amejilaza) abee…kaka

Raymond :( anakaa pembeni yake) hujambo?

Angelina: sijambo kaka, shikamoo…

Raymond: marahaba… (Anamuangalia usoni na nafsi yake inakiri ni kweli kabisa amemkubali mtoto wa kihangaza) unaonekana una heshima

Angelina :( anacheka kidogo)

Raymond: sawa…naomba uniambie kidogo kuhusu wewe…umri wako, kabila lako, elimu yako…niambie pia kuhusu familia yako

Angelina: sawa, Mimi kwa majina naitwa Angelina Daniel…ni mtoto wa kwanza katika familia ya watoto watano, umri wangu…nina miaka ishirini na mbili

Raymond :( wakati huo Angelina anaongea yeye anatabasamu tu huku anamuangalia sana usoni)

Angelina: kabila langu mimi ni mhangaza, na elimu yangu ni darasa la saba maana nilishindwa kuendelea na elimu yangu ili kuwaachia wadogo zangu wasome…maana mama yangu alikuwa hana uwezo wa kutusomesha wote

Raymond: baba yuko wapi?

Angelina: alishafariki siku nyingi Sana

Raymond: maskini

Angelina: ndo hivyo kaka

Raymond: mama ana shughuli gani?

Angelina: hana shughuli yoyote

Raymond: sasa huwa mnaishije?

Angelina: nahangaika Sana…nahangaika kwa ajili ya wadogo na mama yangu, mama yangu amepooza...Kwahiyo mama yangu hafanyi kazi…kwahiyo ili maisha yaendelee huwa nafanya kazi mbalimbali ili tupate kula na kadhalika

Raymond: unaonekena ni mwanamke shupavu sana

Angelina: ukubwa jalala kaka…mabaya yote yanakupata ili wengine waishi

Raymond: aisee nimekufurahia Sana, sasa Catherine ni dada yako kivipi?

Angelina: mtoto wa baba yangu mkubwa

Raymond: wenyewe huwa hawawasaidii?

Angelina: si ndo dada Catherine akaniambia nije huku tena akaniambia kuwa wewe, wewe si ndo Raymond?

Raymond: ndio

Angelina: aliniambia kuwa utakuwa na uhitaji wa mfanyakazi,kwahiyo nikaja na kweli Mungu ni mwaminifu nikapata kazi tulikuwa hatua uhakika ila dada akaniambia kuwa nitapata kwako tu na ikawa kweli

Raymond: dah…wewe unasali?

Angelina: ndio nasali T.A.G

Raymond: wow…Kama mimi na Edmond

Angelina: eti eeh…

Raymond: tutakuwa tunaenda kusali jumapili, Mimi…wewe, Edmond na Catherine…

Angelina: sawa kaka…napenda sana kuongea na Mungu wangu…maana ameshanitendea makuu mengi maishani mwangu…mimi na familia yangu tunaishi kwa neema yake

Raymond: dah…nimekufurahia Sana

Angelina: Asante kaka…

Raymond: sawa…ungependa nikulipe shilingi ngapi?

Angelina: yoyote tuu kaka…siwezi kukupangia

Raymond: wewe unataka shilingi ngapi?

Angelina :( anacheka)

Raymond: Mimi nitakulipa laki na hamsini

Angelina: kazi za ndani???

Raymond: utaanzia hiyo…au nimekupunja

Angelina: hapana kaka iko sawa kabisa sema tu nimeshangaa maana sijawahi kushika pesa nyingi hivyo

Raymond: usijali...Nichukulie Kama kaka yako…ukiwa na shida utakuwa unaniambia tu tunasaidiana dada

Angelina: sawa kaka

Raymond: haya kaniletee chakula ulichopika

Angelina: sawa kaka

Raymond: umepika nini?

Angelina: wali, nyama na maharage (huku anaondoka)

Raymod: niletee…na ndizi mbivu…napenda sana

Angelina :( anaondoka)

Raymond: eeh huyu ndo mwanamke sasa ni mzuri, mchapakazi, na jasiri pia nampenda sana…anafaa kuwa mke wangu…iam in love with my housegirl…nampenda msichana wangu wa kazi…(anatabasamu) love at first sight...

Angelina :( anarudi amebeba chakula kwenye trei na kumtengea Raymond) karibu kaka (anamnawisha)

Raymond :( ananawa) Asante… (Anapakua wali huo kisha anapakuwa na mboga…halafu anaonja) mmmh!!!Chakula kizuri Sana

Angelina: nimefanya kazi Kwa waarabu kama msichana wa kazi, walikuwa wananifundisha sana kupika kwahiyo kwenye mapishi niko vizuri sana

Raymond :( huku anaendelea kula) vizuri Sana…mi Nina mchumba hajui kupika hata chai

Angelina: labda bado mdogo

Raymond: ana miaka 36…

Angelina :( anacheka)

Raymond: utamuona…ila sitamuoa…nitakuoa wewe (anacheka)

Angelina :( anacheka) Mimi???

Raymond: nakutania ila kwani hutaki kuchumbiwa na mimi?

Angelina: wewe si mchumba wa mtu???

Raymond :( anacheka) haya bwana sina usemi nakuacha tu...nakutania lakini usije ukaona nakusumbua

Angelina :( anacheka)

(Raymond anaendelea kula na anaonekana anakifurahia sana chakula kile, anakula huku Angelina amekaa pembeni yake na wanazungumza na kucheka utasema walijuana siku nyingi huku ndo wamejuana, wanacheka, wanafurahi maisha kwa ujumla)

Raymond: chakula kitamu sana asante (anatabasamu)

Post a Comment

0 Comments