IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 12

 


SCENE 12: -

(mchana mwingine ulio mtulivu kabisa jua kwa mbali linawaka na kila mtu anaonekana akiwa na mambo yake. Nyumbani kwa kina Christina, Christina amekaa na mama zake na kama ilivyo kawaida yao hawana kazi ya kufanya)

Christina: na sisi kwa uvivu tunatia fora (anaguna kidogo) yaani sisi wavivu jamani (anacheka) sasa hivi kila mtu anafanya kazi sisi tumekaa jamani (anacheka)

Shangazi: si ndo maana tunataka mabwana matajiri ili tuishi kama ma malkia

(Wote wanacheka kimbea)

Christina: na tunataka matajiri kweli...

(Mlango unagongwa)

Christina: nani tena?

Mama :( anamuita msichana wa kazi) dada embu kafungue mlango

Christina: yaani wanawake nyie ni wavivu mpaka kufungua mlango mnaagiza (anacheka)

Shangazi: wewe si upo kwanini usiende kufungua mama yako kamuita dada?

Mama: si ndo hapo?

Christina: basi yaishe, msije mkanitoa macho bure loh!!!

Msichana :( anafungua)

(Wazazi wa Raymond wanaingia)

Mama: oh…jamani karibuni

(Wazazi wa Raymond wanawakaribia)

Shangazi: karibuni sana

Mr na Mrs.Bembele: asanteni (wanakaa)

Mama: Christina kawaletee wageni vinywaji

Christina :( Kwa heshima) shikamoo baba, shikamoo mama…

Mr na Mrs.Bembele :( wanaitikia)

Christina: mnatumia vinywaji gani

Mr. Bembele: maji tu

Mrs.Bembele: hata Mimi nipe maji tu

Christina :( anajifanya mstaarabu) sawa (anaenda jikoni na baada ya muda anarudi na glasi mbili za maji na kuwatengea) karibuni (anaenda kukaa pembeni ya mama na shangazi yake)

Mr. Bembele :( anakunywa maji kidogo kisha anarudisha glasi mezani) habari za hapa?

Mama: nzuri tu mkwe za huko kwenu?

Mr. Bembele: salama tu

(Kimya kinapita Kama vile kila mtu anawaza ya kwake moyoni)

Mr. Bembele: ah… (anavunja ukimya) mimi na mke wangu tumekuja kuwapa taarifa kuwa wiki ijayo jumatano Raymond na Christina wataenda Dubai kwa ajili ya shopping ya engagement…na pia kupata mapumziko kidogo…kwahiyo leo ni ijumaa na wiki ijayo jumatano watakuwa wanaenda tuseme jumanne watakuwa wanaenda dubai kwa ajili ya shopping hiyo

(Mama, shangazi pamoja na Christina wanaonekana kufurahi sana)

Mama: Dubai?

Mr. Bembele: ndio Dubai…kwa waarabu (anacheka kidogo)

Shangazi: shopping ya kuvalishana tu Pete ya uchumba…

Mr. Bembele: ndio...

Mrs.Bembele :( anaonekana kutofurahishwa hata kidogo na Christina)

Mr. Bembele: sasa Christina utaenda kumwambia Raymond…maana hata hatujamwambia tumefanya Kama surprise

Christina: sawa daddy haina shida

Mrs.Bembele: mara ya mwisho kumona Raymond ilikuwa lini?

Christina: wiki iliyopita mama

Mrs.Bembele: na hapo unjiita mke mtarajiwa wa Raymond? Hujui hata anakula nini nani anamfulia nguo, hujui hata nani anamnyooshea nguo za kazini nani anamtandikia kitanda eti unajiita mke mtarajiwa (anabenjua midomo kwa dharau)

(Mama na shangazi wanaangaliana chinichini)

Christina: mama, kila nikienda simkuti

Mrs.Bembele: kwani huwa anaondoka na vyombo vya kupikia? au huwa anatembea na nguo zake

Mr. Bembele: Mama Ray…hawa ni watoto na hairuhusiwi kukaa pamoja kabla ya ndoa

Mrs.Bembele: hakuna hiyo mbona akitaka hela huwa anamtafuta popote mpaka anampata? Baba Ray we huoni huyu dada anachopenda kwa Raymond ni pesa? Yaani mwanangu anahangaika mpaka kaleta msichana wa kazi yaani hana raha hata kidogo, eti ana mke mtarajiwa loh (anaangalia pembeni)

Mr. Bembele: hayo ni ya watoto tuwaachie wenyewe

Mrs.Bembele: Mimi ni mama yake Raymond na ninamjua mwanangu ni wewe ndo unakomaa na hii ndoa itokee, Raymond hataki hata kidogo

Mr. Bembele: Raymond na Christina wanapendana sana na hilo liko wazi

Mrs.Bembele:  nani kakwambia? Yaani Raymond na Christina wapo tu bora liende baba Raymond…sio Raymond sio Christina hakuna anayempenda mwenzake huko…hivi wewe tatizo lako huwa hukai na mwanao ukamuuliza kwa kifupi tu hata mimi simfurahii huyu Christina

Mr. Bembele:(kwa akina Christina) jamani nisameheni leo sijui kaamkaje unajua sio siku zote zinakuwa ni jumapili naona kaamka na jipya leo nawaomba radhi kwa hilo jamani

Mama: hata usijali mkwe kuwa na Amani...Baba

Mr. Bembele: sawa… (Kwa Christina) inabidi ukampe ripoti mwenyewe…kamwambie kuwa mna safari ya kwenda majuu siku ya jumanne Ili ijumaa muwe hapa na sherehe itakuwa jumamosi

Mrs.Bembele :( anaguna) tunamtumbukiza mtoto wetu kwenye shimo refu ambalo mwisho wa siku sijui atakuja kutoka vipi maskini mwanangu

Mr. Bembele: Mama Raymond naomba uwe na adabu kidogo hii itakupa sifa nzuri kwa wakwe wako hawa watarajiwa

Mrs.Bembele: sitaki kuonekana nina sifa nzuri kwao maana hata siwataki kabisa mimi…yaani simtaki mimi huyu Christina (ananyanyuka na kuondoka zake)

Mr. Bembele :( ananyanyuka pia) jamani jitayarisheni na sherehe ya kutoa mahari na pete ya uchumba atake asitake atake lazima hii ndoa itafanyika mimi ndo baba wa familia ile kwahiyo msihofu (anatoka)

Mama na shangazi: sawa…hamna shida

(Mr. Bembele anaondoka kuelekea nje na kuungana na mkewe ambao kwa pamoja wanapanda gari na kuondoka zao, huku ndani Christina na mama zake wanaendelea na maongezi)

Mama :( anaguna) yaani mama Raymond hakupendi wewe Christina hata kidogo yaani umemfika kifuaani mpaka ameamua kuongea mbele ya mume wake…ulimfanyaje?

Christina :( huku anabenjua midomo) wewe unahisi Mimi Hilo linanipa mawazo? Aende zake huko (anafyonza) huyu mama anazeeka vibaya na sura yake mbaya…mi sijawahi kumfanya chochote, Raymond atanioa mimi na sio mtu mwingine

Shangazi: naomba nicheke (anacheka) maana nimejibana kwa muda Mrefu kucheka (anacheka tena) pamoja na hayo yote umeona baba mtu anakutetea na kama ni hivyo hatuna shaka lazima hii ndoa ifanyike bado miezi miwili tu tule wali na wiki ijayo jumamosi pete kidoleni

Mama: ni hatari, hongera mwanangu

Christina: Asante mama

(Wanacheka kimbea)

Mama: Mama Raymond atapata tabu Sana yaani mpaka namuonea huruma maskini…anahangaika sana eeh

Shangazi Na Christina: sana yaani

Christina: kama kichawi hiki kibibi kizee

(Wanacheka Kwa dharau na kebehi na kumteta sana mama yake mzazi Raymond)

Post a Comment

0 Comments