IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 13

 


SCENE 13: -

(Jioni nyingine Safi kabisa, Christina anafika nyumbani Kwa Raymond

Mlinzi: karibu shemeji

Christina: Asante (anaegesha gari kisha anaelekea ndani kwa Raymond) yupo huyu… (anaelekea ulipo mlango wa kuingilia chumbani kwa Raymond)

Mlinzi: yupo…

Christina :( anagonga mlango) hodi…

Angelina :( anafungua)

Christina :( anamuangalia kwa dharau) wewe ni nani?

Angelina: naitwa Angelina ni msichana wa kazi wa kaka Raymond…karibu nikusaidie dada…unamtafuta kaka Ray? na nimwambie anatafutwa na nani?

Christina :( anamfyonza kisha anaingia) shenzi Sana…wewe hujui Mimi ni nani?

Angelina: dada…sidhani Kama ni ungwana kunitukana ambapo nimekuuliza kitu kidogo tu…

Raymond :( anakuja akiwa ametokea jikoni ambapo anaonekana alikuwa anapika)

Christina: wewe dada kwanini umemuachia mume wangu apike?

Raymond: nimetaka mwenyewe kupika na sioni kosa hapo

Christina: Ray…huyu kinyago ni nani?

Raymond: we koma kabisa kumuita huyu dada kinyago ana jina huyu (kimya kidogo) anaitwa Angelina…

Angelina: Ni msichana wake wa kazi

Christina: sijakuuliza…

Angelina :( anakaa kimya)

Christina: mimi naitwa Christina…ni mke mtarajiwa wa Raymond...Ulitaka kujua, je. Una swali lingine…

Angelina: hapana…sina swali (anaenda jikoni)

Raymond :( Kwa ukali) we mwanamke unataka nini?

Christina: kwani vipi Raymond?

Raymond: sidhani hata Kama nakutaka tena Christina

Christina: pole Raymond…nimekuja kukupa taarifa kuwa wiki ijayo kwenye jumatano hivi tutakuwa tunaenda Dubai Kwa ajili ya shopping ya engagement party…yetu

Raymond: ah...Wapi...Mbona sina taarifa juu ya Hilo?

Christina: ndo nimekupa sasa hivi…baba Na mama yako walikuja kuniambia wakaniambia nije mwenyewe kukuambia kuwa tuna safari honey ya kwenda Dubai

Raymond: siendi na wala sitaki

Christina :( anacheka)

Raymond: kwanini una roho ya hivyo we mwanamke?

Christina: ipoje…

Raymond :( anampigia mama yake, simu inaita kisha inapokelewa) mama…shikamoo?

Mrs.Bembele: marahaba baba…vipi?

Raymond: mbona hamkuniambia kuwa natakiwa nisafiri kwenda nje? Hamjui kuwa nina ratiba zangu?

Mrs.Bembele: samahani mwanangu…ni baba yako ndo aliamua hayo yote

Raymond: bwana muwe mnaniuliza kuhusu hivi vitu…sio mnajipangia...Tu nishakuwa mtu mzima na sio mtoto mdogo bwana…

Mrs.Bembele: usikae unagombana na baba yako…we msikilize tu si unajua alivyo? We kuwa mpole mwanangu…nakupenda sana mwanangu…najua huyo mwanamke humtaki tena ila sasa baba yako keshaamua…kuwa tu kama wahindi kwamba umepangiwa kuoa mtu Fulani kuwa mpole na umuoe tu…

Raymond :( anakata simu kwa hasira)

Christina :( anacheka)

Raymond: yaani Christina…nakuchukia Sana

Christina: wewe vipi…kwani Mimi ndo niliamua hili si umchukie baba yako?

Raymond: I hate you so much; you are ruining my life…

Christina :( anacheka)

Raymond :( anaenda zake chumbani)

Christina :( anamfuata) Raymond

Raymond: naomba uniache

Christina :( anajikuta anajishusha) nisamehe mpenzi kama kuna sehemu nimekuudhi!!Nilikuwa nakutania tu jamani, nisamehe Sana mpenzi wangu Maana nimekuona umechukia sana

Raymond: (anashusha hasira) sijachukia na wala sina sababu ya kuchukia sema tu hawa wazazi wangu wamenifanyia kitu ambacho sijakipenda na ndo maana umeona nipo hivi ila usijali sijachukia kuwa na Amani,na kwa kuwa wameshaamua hiyo safari basi sina jinsi Zaidi y kutii walichokipanga

Christina: oh…my love (anamkumbatia) nakupenda na sitaki tuwe tunagombana kizembe baby

Raymond :( anaonyesha kutotaka kumkumbatia pia) ok …it is okay

Christina :( anaanza kujidekeza) leo nalala huku kwako na sio leo tu…mpaka siku tunasafiri

Raymond: hiyo itakuwa ni kukaa pamoja na  bado hatujaruhusiwa kuishi pamoja

Christina: sitaki kukukera baby…so sawa nitalala Leo then kesho nitaondoka

Raymond: sawa…

(Mlango unagongwa)

Christina :( anafungua mlango anakuta ni Angelina) nini?

Angelina: chakula tayari

Christina: mbona mapema Sana?

Raymond :( anatokea kwa nyuma yake) ndo tamaduni ya nyumba yangu…kwahiyo ni vyema wote tukaifata… (Anaelekea nje) Angel…njoo

Angelina :( anamfuata) abee kaka

Raymond: umeshatenga chakula?

Angelina: ndio kaka…karibuni mezani

(Raymond na Christina wanaelekea mezani)

Angelina :( Simu yake inaita, anatoka pembeni na kuipokea)

Christina :( anaishangaa ile simu) yaani kijakazi ana simu nzuri Kama ya boss wake

Raymond: kwani kuna ubaya gani jamani?

Christina: hakuna ubaya halafu mbona Kama vile unamtetea Sana huyu dada umeshalala nae?

Raymond :( anajikuta anakasirika Sana) unadhani Mimi ni msaliti kama wewe? (Anakasirika Sana)

Christina: okay tusianze ugomvi, tule

Christina: badilika wewe mwanamke…

Christina :( anapakua chakula kisha anaanza kula)

Raymond :( kimya)

Christina: halafu mbona hukuniambia kuwa umempata msichana wa kazi?

Raymond: sikuona haja ya kukuambia…

Christina :( anaguna) hayo majibu yako siku hizi

Raymond: yamefanya nini? Au unataka nikujibuje wewe mwanamke?

Christina: Ray, unataka kuachana na mimi? Unajua sikuelewi kabisa

Raymond: honestly yes…ila kwa kuwa ndo ishapangwa kuwa ni lazima nikuoe sina jinsi bali kuwa mpole tu unadhani nitafanyaje mimi?

Christina :( anaguna halafu anakaa kimya)

Raymond: Ina maana kati yetu upendo umeisha kabisa…kwani hilo hulioni?

Christina: lakini wazazi wamepanga mimi na wewe tuoane no matter what wenyewe hawataki kusikia kuwa sijui upendo umeisha kati yetu…tufunge tu ndo Ray…najua upendo utarudi kati yetu

Raymond :( kimya huku anaendelea kula chakula chake)

Christina: basi afadhali unijibu chochote Raymond…

Raymond: He!!!Wewe dada vipi?

Christina: naomba unijibu tu jamani!!

Raymond: sina cha kukujibu…endelea kula

(Angelina anarudi mara baada ya kumaliza kuongea na simu kuongea na simu)

Raymond :( huku anatabasamu) naona shemeji alikuweka sana maana si kwa kuongea huko

Angelina: hapana kaka ni mama yangu…anakusalimia sana…

Raymond :( anaachia tabasamu) Asante, anaendeleaje?

Angelina :( anatabasamu) anaendelea vizuri tu

Christina :( anabenjua midomo) kwahiyo wengine ni kugombana tu lakini kijakazi anachekewa basi sawa

(Raymond na Angelina wanakaa kimya)

Christina :( ananyanyuka) nimeshiba…asanteni kwa chakula... (Anaingia ndani kwa hasira)

Angelina: wifi mkali kweli

Raymond: achana nae… (Anavuta kiti) kaa ule chakula

Angelina: we unataka nitolewe masikio kwa jinsi wifi alivyo mkali siwezi hata kuthubutu kukaa na wewe, mi naenda kula jikoni (anaenda jikoni)

Raymond :( anabeba sahani yake na kumfuata jikoni)

Angelina: kaka vipi?

Raymond: mi nataka nikae na wewe kama hautajali

 (wanakaa kula, wanaonekana kufurahia maana wanaongea mambo mbalimbali, wanacheka na kila kitu kinaonekana kipo vizuri kati yao…wanaendelea kula na kucheka sana na mtu kama ungewakuta ungejua ni mtu na mpenzi wake au mtu na mtu wake wa karibu sana maana wanaonekana kuridhiana na kupendana pia)

Raymond: wewe mpole sana hadi raha (anatabasamu)

Post a Comment

0 Comments