IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 14

 


SCENE 14: -

(jumapili nyingine kama ilivyo kawaida ya kila jumampili kwamba Raymond haendi kazini anakuwa nyumbani kwa ajili ya mapumziko, hivyo amekaa bustanini kwake, hewa inaonekana ni nzuri na mazingira ya nyumba ile iko sawa kabisa,na yote hiyo ni shukrani kwa Angelina,binti wa kazi na kipenzi cha siri cha Raymond .,Angelina yupo getini na Ramadhani na wanaonekana kubadilishana mawazo ikiwemo na kufurahia pamoja,Raymond yupo bustanini lakini anaonekana kuwa amemkubuka sana,Angelina kwahiyo anamtafuta)

Raymond :( anaita) Angelina…

(Angelina yupo Kwa mlinzi na wala hana wazo kama anatafutwa na bosi wake)

Raymond: Angel…

(Kimya)

Raymond:(anaamua kunyanyuka)huyu Mrembo yuko wapi jamani?(anaelekea kwa mlinzi ili amuulize,anakuta Angelina hana habari na anacheka mno kitendo kinachompa hasira na wivu,ukiangalia anamfahamu Ramadhani kwa uhuni)dah…mbona wanafurahiana hivi au Ramadhani keshanitangulia?...Dah!!!haiwezekani Angelina ni wangu,na atakuwa wangu…(anajishangaa)mbona nimewaka na wivu hivi,nakuwa kama Angelina keshakuwa mpenzi wangu yaani nashangaza hata nikimwambia Edmond kuwa nampenda Angelina ila bado sijamtamkia na ninaona wivu kila nikimkuta kakaa na mwanaume mwingine najawa na wivu atanishangaa…hivyo basi natakiwa nijitahidi sana kutoonyesha udhaifu wowote(anamuita Angelina)Angelina…

Angelina :( ndo anashtuka sasa) abeee kaka…

Raymond: hivi umeshapika?

Angelina: kaka sasa hivi bado asubuhi Sana na pia tumetoka kunywa chai muda si Mrefu…ila kama unataka kuniagiza sokoni ni sawa tu kaka

Ramadhani: yeye ndo bosi

Angelina: eeeh… (Anacheka)

Ramadhani :( anacheka pia)

Raymond :( anajikuta anachukia bila sababu ya msingi) naona mnafurahiana Sana eeh

Ramadhani: lazima tufurahiane bosi… (Anamshika Angelina bega) huwezi jua bosi labda kanaweza kakawa ka shemeji kako…kabinti spesho

Raymond :( anazidi kupandwa hasira na wivu) unamaanisha tayari umeshammiliki? (Anamuangalia Angelina ambae muda wote anaonekana kucheka kwani ana kuchukulia utani)

Ramadhani: sijammiliki ila nikitaka naweza…sekunde tu

Raymond :( anapatwa na wivu anatamani hata kumrukia Ramadhani ambae muda wote huo anaongea anadhani wanataniana kumbe mwenzie anaumia sana kutokana kuwa amempenda Angelina kwa dhati na hataki kumpoteza) hongera…yako...

Ramadhani :( anacheka) Asante boss…

Raymond :( anataka kuondoka)

Angelina: kaka huyu anatania wala usimchukulie Sana, ni utoto ndo unamsumbua

Raymond:(anashusha pumzi mithili ya mtu aliyechoka sana) sawa…toka hapo uende sokoni na pia wewe si wa kukaa getini Angelina wewe ni wa kukaa ndani…kuna kila kitu kuna tv na pia nimekununulia simu nzuri, ukikosa wa kuongea nae uwe unaongea na mimi kwenye simu

(Ramadhani na Angelina wanabaki wanamshangaa)

Raymond: natania Kama mlivyonitania…

(Wote wanacheka)

Ramadhani: si ndo nikaanza kuwaza yamekuwa hayo jamani?

Raymond: hata msinijali sana ndugu zangu…ok Angelina, nenda sokoni uje nikusaidie kupika (anatabasamu)

Angelina :( anatabasamu) sawa kaka (haraka anaingia ndani kuchukua kikapu cha sokoni na kuondoka zake)

Raymond :( Kwa Ramadhani) na wewe punguza bwana yaani mtoto wa watu kaja juzi tu leo unamtaka, kila saa unamuita huku

Ramadhani :( huku anacheka) ushamtamani Mtoto wa watu nini?

Raymond: hamna wewe…ni msichana wangu wa kazi atabaki kuwa mdogo wangu na isitoshe nina mchumba hata wewe unajua

Ramadhani: yule mnaegombana nae kila mkikutana? (Anacheka Sana) mwanamke kiwingu yule…Duh

Raymond: ndo hivyo, sasa unadhani nitafanyaje Kama ndo alitolewa kwenye ubavu wangu…nitapingana na mipango ya Mungu?

Ramadhani: duh…Kama Mungu alikupangia yeye ndo awe Hawa wako rafiki yangu kazi unayo…

Raymond :( anacheka kidogo) sasa unadhani nitafanyaje?

Ramadhani: tafuta chombo kipya…wewe kaka una hela zako

Raymond: Kama Angelina hivi

Ramadhani: si umesema ni mdogo wako huyo?

Raymond: mfano tu

Ramadhani: eeh…katoto kadogo dogo kana heshima zake

Raymond: sawa nitafanya mpango…

Ramadhani: hapo sawa, ila sasa sio Angelina maana nishampangia

Raymond :( anajikuta tena anakasirika) …achana na Angelina bwana tuongee mada nyingine bwana

Ramadhani: poa hamna noma au umempenda Angelina tunazugiana tu hapa?

Raymond: hamna…halafu Jumatano au jumanne nasafiri naenda Dubai narudi, ijumaa, jumamosi namvalisha Pete ya uchumba Christina...

Ramadhani: yaani unamvalisha Pete huku unaona kabisa hamna maelewano?

Raymond: nitafanyaje ndo baba kapanga kwahiyo sio umbake Angelina huku nyuma nitakutoa masikio

Ramadhani: wewe Angelina ameshakuteka wewe (anacheka)

Raymond :( huku anatabasamu) hamna ni dogo tu Fulani…hamna jipya

Ramadhani: haya bwana yetu macho, tutakuja kusikia tu si tupo (anacheka)

Raymond: hamna (huku anaingia ndani)

Ramadhani: angalia huyo unaetaka kumvalisha Pete asije akatutoa wote masikio

Raymond :( anacheka) mtajijua wenyewe…

Ramadhani :( anaingia kibandani kwake)

Raymond:(anajisemea moyoni)I love Angelina so much mpaka siwezi tena kuficha hizi hisia…nampenda,tangu nimemuona nimeshindwa kufuta picha yake kichwani mwangu…nampenda…and I wish to make her my wife(anajitupa kwenye sofa kama mzigo)Raymond weds Angelina…hiyo siku will be the happiest day of my life…(anajichekea mwenyewe)lakini mimi mjinga ee…Angelina si mdogo wangu huyu jamani mbona nataka kutia aibu mimi…lakini hamna kwani tumezaliwa tumbo moja…sio mdogo wangu ni mwanamke wa ndoto zangu…I will marry her…yes I will marry her(anajishangaa tena)hivi mimi nina akili kweli jamani?(anajicheka sana)oh Angelina…iam going to make you my wife…oh my God…I cant wait to be your husband..Na ulivyo shapu unaweza ukawa unakuja kunifungulia geti wewe yaani dah…eeh Mungu nisikie na umfanye Angelina awe wangu jamani (anacheka peke yake)

Angelina: kaka tunapika nini?

Raymond: chochote maza hausi…wewe ndo mmiliki wa himaya yangu

Angelina :( anashangaa Sana) nini?

Raymond: nini kwani?

Angelina: umesema maza hausi?

Raymond: nakutania (anacheka) pika chochote (anacheka sana)

Angelina: kaka bwana... (anacheka sana)

Post a Comment

0 Comments