IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 15

 


SCENE 15: -

JUMANNE SIKU YA SAFARI YA DUBAI: -

(alfajiri na mapema Raymond na Christina wanatoa mabegi nje ili kuelekea uwanja wa ndege kwa ajili ya kuanza safari yao ya kwenda Dubai, lakini kabla ya kuondoka, Raymond anaona ni vyema kumuamsha Angelina na kumuaga. hivyo anaenda mpaka mlangoni kwa Angelina na kugonga mlango)

Raymond: Angel…

Christina: mi nashindwa kuelewa kwanini unamuamsha huyo tunachelewa bwana…

Raymond: Ni lazima nimuone Angelina, sitaondoka bila kumuona

Christina :( anashangaa) unamaana gani kusema kuwa huwezi kuondoka bila kumuona

Raymond :( anajishtukia kuwa ameropoka) Ni msichana wangu wa kazi ni muhimu nimuone ili nimpe maelekezo maana hatutakuwepo mpaka ijumaa

Christina: halafu mbona unamuacha peke yake kwanini asiende kukaa hata kwa yule mke wa Edmond mpaka tutakaporudi? Mi siwaamini hawa wasichana tutakuta kila kitu kimebebwa humu ndani

Raymond :( anatikisa kichwa huku anaendelea kugonga mlango)

Angelina :( anafungua mlango)

Christina: eti ndo kajifanya kuamka sasa hivi unatuchelewesha bwana (anaangalia pembeni)

Raymond: just whats wrong with you Christina, kwanini unakuwa na roho ya hasira kiasi hiki?

Christina: stop judging Na ufanye haraka mi nakusubiri kwenye gari (anampokonya funguo na kuondoka zake)

Angelina: shikamoo kaka…

Raymond: marahaba mdogo wangu (anaachia tabasamu) yaani wewe mzuri hata ukiwa umetoka usingizini…

Angelina :( anacheka kidogo) kaka bwana umeanza utani wako…

Raymond :( moyoni) nakupenda Sana Angelina, I swear natamani nisiende hii safari nibaki na wewe hapa tukae tu tufurahi na kadhalika…

Angelina: kaka umeniamsha…

Raymond: ndio mdogo wangu…Mimi nasafiri naenda Dubai nitarudi ijumaa nadhani usiku kitu Kama hicho naomba uniangalizie nyumba yangu nadhani Edmond na Catherine watakuwa wanakuja mara kwa mara kwahiyo usiogope sawa mama

Angelina: sawa kaka nakutakia safari njema

Raymond: naomba nikukumbatie, Kama kaka yako tafadhali Ili safari yangu iwe salama

Angelina: wifi akiingia ghafla italeta picha mbaya…we nenda tu kaka mi nakutakia safari njema kaka

Raymond: sawa, mi naenda…ila ilikuwa tu kiheshima maana tumekuwa pamoja Mimi na wewe na tunaheshimiana nipe tu nafasi nikukumbatie ili nipate mema huko napoenda

Angelina :( anamkumbatia)

Raymond :( anamkumbatia pia) Asante Angelina yaani hujui kumbatio lako limenipaje furaha na faraja si umeona wifi yako alianza kunitibua…

Angelina: nenda sasa kaka, wifi anakusubiri…

Raymond :( huku anaondoka) sawa tutaonana ijumaa nikuletee zawadi gani kutoka huko?

Angelina: yoyote…

Raymond: poa… (Anatoka nje) Angelina my love, my housegirl, I really love you my darling

Christina: Raymond…tunaenda au hatuendi?

Raymond: hatuendi… (Anataka kurudi ndani)

Christina: ngoja nimpigie baba yako simu…sijui yaani sijui umekuwaje wewe mwanaume?

Raymond :( anapanda gari kimya bila kuongea chochote)

Christina: kiboko yako ni baba yako tu…

Raymond :( kimya)

Christina :( anaanza kuendesha gari na kuliondoa mahala pale) sasa nani atalirudisha gari nyumbani?

Raymond :( anamuangalia bila kusema kitu)

Christina: mbona husemi kitu unaniangalia tu jamani, mbona umekuwa hivyo hukuwa hivyo…

Raymond :( anajisemea moyoni) hivi ingekuwaje Kama Angelina au mwanamke kama Angelina angekuwa ndo mtarajiwa wangu I swear hiyo raha ambayo ingekuwa moyoni mwangu ingekuwa sio ya kifani…

Christina: una dharau siku hizi sijui kwanini...Yaani unanikera…

Raymond: jamani huko airport hatufiki…please sitaki kugombana na wewe sina hiyo nguvu tafadhali (anawasha redio iliyopo kwenye gari)

Christina: okay sitakusemesha maana naona unakereka Sana mpaka naogopa kweli

Raymond: afadhali…

(wanaendelea na safari huku kila mmoja wao anaonekana kuwaza mawazo yake mwenyewe, baada ya dakika kadhaa wanafika uwanja wa ndege, wanaposhuka kutoka kwenye gari Raymond anabeba begi lake na bila kujali anaingia ndani na kumuacha Christina peke yake anahangaika na kuegesha gari. anapokuwa ndani Raymond anaona ni bora tu, ampigie kipenzi chake simu inaita mwisho inapokelewa) nambie bado umelala

Angelina: nimeshaamka mbona tangu uliponiamsha kaka

Raymond: niite tu Raymond nitafurahi sana ukiniita Raymond...

Angelina: sawa Raymond…

Raymond: Safi kabisa mdogo wangu…

Angelina: Na wewe niite Angelina…

Raymond: sawa malaika…

Angelina :( anacheka kidogo) mmeshafika?

Raymond: ndio tumefika uwanja wa ndege nitakupigia tena nikifika Dubai…

Angelina: sawa Raymond…

Raymond: baadae… (Anakata simu)

Christina: kwahiyo ukaona kunisaidia kupaki gari nitafaidi Sana…

Raymond :( kimya huku anaendelea kutembea kuelekea ndani)

Christina :( anatikisa kichwa) sasa si Kama hukutaka kwenda Dubai si ungesema tangu siku nakuletea habari?

Raymond: unataka nirudi nyumbani maana nakuona unaongea tu…. huchoki kuongea jamani we mwanamke? Tangu Jana usiku unaongea tu…nimechoka kusikia malalamiko yako bwana

Christina :( anaamua kukaa kimya)

Raymond: Na ndio sikutaka kwenda Dubai wala wapi…nataka kukaa hapa nchini nikiendelea na kazi na maisha yangu…wewe na baba mmekomaa kweli kwenda huko Dubai

Christina: umekuwaje wewe

Raymond :( moyoni) Mimi mwenyewe najishangaa yaani nasikia tu hasira tu ya kwenda huko Dubai

Christina: sikuelewi…Raymond kwani kuna shida gani?

Raymond :( kimya)

Christin: unajua tumekaa muda Mrefu Sana hatuna maelewano hii safari itatuleta pamoja au wewe unaonaje?

Raymond :( kimya)

Christina :( anamsogelea na kumbusu shavuni)

Raymond :( anageukia pembeni)

Christina :( anamuona hayuko sawa) baby are you okay?

Raymond :( kimya)

Christina: talk to me jamani

Raymond :( kimya)

Christina: baby… (Anajaribu kumgeuzia upande wake) basi kama hutaki

Post a Comment

0 Comments