IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 16

 


SCENE 16: -

(Jioni nyingine ya siku ya ijumaa, Edmond na wazazi wa Raymond wamekaa uwanja wa ndege wakiwasubiri Raymond na Christina wawasili)

Edmond :( anaguna) mmmh…wamechelewa

Mr. Bembele :( anamuangalia kwa dharau) wewe unajua nini wewe? Hata ndege umeshawahi kupanda kweli wewe?

Edmond :( kimya)

Mrs.Bembele: jamani mume wangu maneno gani hayo? Kwanini unamdharau Mtoto wa watu?

Mr. Bembele: Na wewe mke wangu…kwani hapo nimesemaje?

Edmond :( kimya)

Mrs.Bembele: basi tufanye yameisha baba

(Raymond Na Christina wanawafika walipokuwa)

Raymond: hello…mambo zenu

Edmond: oh… (Anamkumbatia)

Mr. Bembele: kwahiyo Mimi baba yako na uzee wangu nimejikongoja weee mpaka nimekuja kukupokea hujaniona umemuona tu huyo Mond mwenzio si ndio?

Raymond: dad…please…

Mrs.Bembele: sidhani hapo kuna tatizo baba Raymond…tafadhali msianze ugomvi hapa mbele za watu ni aibu jamani

Christina :( anatabasamu) shikamoo baba…

Mr. Bembele: marahaba mwanangu za Dubai? Did you enjoy?

Christina: Sana dad...Asante… (Anaachia tabasamu)

Mr. Bembele: usijali…nitafanya chochote kukufurahisha mkwe wangu…

Raymond :( anatikisa kichwa ishara ya kutokubaliana na neno mkwe)

Edmond :( Kwa Raymond) enhe…Mond nambie

Raymond: ah…fresh…tu mapya?

Mr. Bembele: bado tu umemuona huyo rafiki yako?

Mrs.Bembele: shida nini baba Raymond…Mimi mbona hajanisalimia?

Raymond: let’s get out of here!!!Itakuwa msala sasa hivi…

(Wanatoka nje na kuelekea kwenye gari kubwa waliokuja nalo kina Mr. Bembele na mkewe)

Edmond :( anataka kupanda kwenye gari)

Mr. Bembele: (kwa Edmond) wewe Mtoto huruhusiwi kupanda hili gari…nakuchukia Sana maana wewe ndo chanzo cha mimi na mwanangu kugombana kila mara…

Edmond :( Kwa upole anashuka na kujiweka pembeni)

Raymond :( Kwa kuwa na yeye alikuwa amekwisha panda gari anashuka) huu ni unyama uliokithiri…sitaruhusu usimfanyie haya rafiki yangu eti kisa nini…kwamba anatoka katika familia ya kimaskini?

Mr. Bembele: umaskini ni laana wewe Mtoto elewa…

Raymond: hata Kama hata wao ni watu…na huwezi kunipangia nimpende nani naweza hata nikaoa mwanamke maskini

Mr. Bembele :( anacheka Kwa kejeli) unamuoa Christina na si mwanamke maskini…utake usitake utamuoa Christina

Christina :( anachekelea moyoni)

Raymond: sio lazima…kumuoa Christina

Mrs.Bembele :( anagundua Christina anaufurahia ugomvi huu) tafadhali acheni kugombana for heavens sake mnawafurahisha na maadui ambao hawana mapenzi mema na hii familia

Mr. Bembele: Kama nani?

Mrs.Bembele :( Kwa ujasiri) Kama Christina

Christina: Mama Mimi tena?

Mrs.Bembele: unaweza kuniambia unachekea nini?

Christina: sijacheka mama… (anajifanya mpole) unanichukia ndio nakubali ila kitendo cha kuona kila nachofanya ni kosa…kwakweli sikubali…

Mr. Bembele :( Kwa mkewe) mama Raymond muombe msamaha mkwe wako mara moja na nimesema…mimi mume wako…

Christina :( anajisemea moyoni) tuone sasa utafanyaje wewe bibi kizee mshenzi usie na akili…

Mrs.Bembele :( anamgeukia Christina) nisa…

Raymond :( anamkatisha mama yake) No…never, kwani umemkosea nini?

Mr. Bembele: Raymond…usiingilie maamuzi yangu…niheshimu...Mimi ni baba yako na nimekupa kila kitu

Raymond :( anamuangalia usoni) kwahiyo dad…ulinipa kila kitu ili uniamuru chochote tu…na sio kwa upendo?

Mr. Bembele: sijamaanisha hivyo baba (anapoa)

Raymond: Kama ulinipa Ili unifanye chochote dad…nakurudishia kila kitu na itakuwa ni vizuri maana hata kumuoa Christina sitamuoa tena…

Mr. Bembele: mwanangu umenielewa vibaya baba…nimekupa Kwa upendo kabisa

Raymond: mama, Edmond…tuondoke zetu, sisi hapa ni maskini na hatuna hadhi ya kusimama na Mr. Bembele

Mr. Bembele: no son, sio hivyo baba yangu jamani basi nisamehe Mimi mwanangu

Raymond :( anaita taksi) navirudisha vyote (Kwa mama yake na Edmond) twendeni… (Anapanda kwenye gari)

(Mrs.Bembele na Edmond wanapanda kwenye gari na kuondoka zao)

Mr. Bembele: shit!!!nimefanya nini mimi jamani? Nimegombana na mwanangu tena!!! Hii imeshakuwa ni tatizo

Christina: mwanao ana kiburi tu…muache akitulia atarudi tu kuomba msamaha

Mr. Bembele: Raymond ni mwanangu wa pekee na ninamfahamu vizuri sana akiamua kitu kaamua… (Anampigia simu Raymond inaita Sana mwisho inakata) hapokei (anasikitika)

(Upande alipo Raymond, Edmond na Mrs.Bembele)

Mrs.Bembele: usiwe na hasira baba msamehe baba yako…

Raymond: siwezi…atanisumbua sana eti kisa alinipa nyumba, gari, na kazi ndo anipe na mwanamke na rafiki pia?

Edmond: take it easy...

Raymond :( anatulia kidogo) by the way…kuna jambo nataka kuwaambia…

Mrs.Bembele: au ndo sababu ya kutuleta humu?

Raymond: no dad…kaniboa…anyway nataka tu kutumia hii nafasi ya kuwaambia yangu ya moyoni…

Edmond: tuambie…tunataka kusikia? Christina ana mimba?

Raymond: no… (Kimya kidogo) sijui mtalipokeaje ila ni lazima niwaambie…

Mrs.Bembele: enhe… (Anaonekana ana shauku Sana)

Raymond: IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL

Edmond Na Mrs.Bembele :( wanakuwa Kama wamegandishwa maana wanashangaa sana)

Raymond…. yes, nampenda…Sana Angelina…I feel she is right for me…

Edmond: yaani Raymond

Raymond: naelewa unachotaka kusema kuwa ni shemeji yako na kwamba nimemchezea…au nilikuwa na nia hiyo…jamani ilikuja tu tangu siku ya kwanza namuona…it was love at first sight…yaani nilipomuona tu…I swear nikampenda na haikuwa nia yangu kwamba Edmond akiniletea mwanamke mimi nitamfanya awe wangu…imetokea tu

Edmond: wala hiyo haina shida…nataka kukuambia kesho unamvalisha Pete Christina…

Raymond: I swear akili yangu haifanyi kazi nachotaka tu ni kukimbia nyumbani na kumzawadia Angel…hizi zawadi na kumwambia kila kitu…kuwa nampenda nataka awe mke wangu

Mrs.Bembele: sasa baba…usiache kesho kumvalisha Pete huyo mwanamke…fanya hayo kwa kumtunzia baba yako heshima yake…sawa baba ee tumeshaalika watu baba naomba uelewe hilo sawa ee

Raymond: sawa mama…naelewa

Post a Comment

0 Comments