SCENE 17: -
(Majira ya
saa NNE usiku siku hiyohiyo ambayo Raymond na Christina wamerudi kutoka Dubai, Angelina
anaingaia chumbani kwake mara baada ya kumaliza kazi zake za kila siku)
Angelina: bora kaka Ray karudi maana mmh…hili jumba
lilivyo kubwa yaani nilikuwa naogopa kulala peke yangu(anaangalia kitandani anaona gauni zuri sanai)hili gauni limefikaje
hapa na nani kalileta?(analinyanyua,kikaratasi
kidogo kinaanguka,anainama kukiokota)hiki kinasema…vaa gauni hilo na viatu
viko chini ya uvungu na unifuate bustanini…(anaguna)nani
huyu kaniandikia ujumbe(anainama
kuangalia chini ya uvungu anakutana na viatu vizuri na vya thamani…anavaa gauni
kisha anavaa viatu anapaka poda kidogo kisha anatoka kwenda bustanini,baada ya
hatua chache anafika bustanini)wewe ni nani…asante kwa zawadi nzuri ya
viatu na gauni..
Mtu :( anageuka
taratibu na mwisho anajionyesha sura ni Raymond) ni mimi…Angelina...
Angelina :( anashangaa
Sana) kaka Raymond?
Raymond: Angelina…
Angelina: Asante kwa gauni zuri kaka yangu yaani una
roho ya pekee halafu ile hela uliyonipa nimewatumia nyumbani nimewaambia
wafungue ka biashara wameshukuru sana
(Sehemu hiyo imepambwa Kwa Maua mazuri sana na kuna utulivu wa hali ya
juu)
Raymond :( anatabasamu)
usijali
Angelina: haya kaka…gauni zuri kweli halafu kumbe
kuna sehemu nyingine ya bustani pazuri hivi…sikuwahi kujua
Raymond :( anamkaribia
na kumshika mkono) nakupenda Angelina…nakupenda sana, nilitaka nisikuambie
chochote ila nimeshindwa, nakuhitaji sana katika maisha yangu
Angelina :( anamshangaa Sana) kaka yangu…kivipi
tena kaka
Raymond: kimapenzi… (Anamshika mkono) tangu nakuona kwa mara ya kwanza kabisa moyo wangu
umekubali na kujiridhisha kwamba ni wewe ndo nataka uwe mke wangu (anamshika mikono yote miwili)
Angelina:(anamsukuma)
hapana…siwezi wewe ni mume wa mtu, na pia hata hatuendani maana wewe ni tajiri
sana siwezi hata siku moja nikafanya ujinga wa kuwa na wewe kimapenzi huku
najua unaenda kuwa mume wa mtu…tafadhali naomba uendelee kuniheshimu kama mdogo
wako…na pia umeona unaweza kuninunua kwa gauni na viatu kweli watu matajiri mna
dharau sana
Raymond: sio hivyo…nilitaka upendeze tu kisha
nikuambie yaliyo moyoni mwangu nakupenda Sana hata Catherine na Edmond hata
mama yangu wanajua na wapo tayari kuwa na sisi katika safari yetu mpya
tafadhali nipe nafasi mpenzi wangu na hakika nitakutunza
Angelina: wewe ni mume mtarajiwa wa mtu…kesho tu
unaenda kumvalisha pete ya uchumba mchumba wako…mimi sitaki matatizo na mchumba
wako, unamjua alivyo
Raymond: Mimi na yeye hatuna upendo yaani
hatupendani…yeye ana mwanaume anayempenda na mimi nina wewe…naapa mbele za
Mungu kuwa nakupenda sana, embu naomba
unielewe Angel…tafadhali
Angelina (anaanza
kumuelewa) sasa vipi kuhusu baba yako atakubali Mimi kuwa na wewe
Raymond: haijarishi nitakulinda siku zote za maisha
yangu… (Anamshika mikono yake)
nakupenda (anambusu kwenye paji la uso)
Angelina: lakini Mimi sitaki kubeba mimba sasa
hivi…
Raymond :( anacheka)
nani amekuambia kuwa ukishikwa na mwanaume tu au akikubusu unabeba
mimba…usijali nitakulinda na sitakuchezea…nitakuoa…umesikia ee (anacheka) yaani wewe
Angelina: sawa
Raymond :( anatabasamu)
kwahiyo unamaanisha kuwa…
Angelina: nimekukubali…utakuwa mpenzi wangu
Raymond: na baadae mumeo… (Anacheka)
Angelina :(
anacheka pia) ndio…
Raymond :(
anambeba) asante Angelina hujui nimeisubiri hii siku muda gani tangu umekuja
nimekufungulia mlango siku ile unaletwa na Edmond…nilipokuona tu nafsi yangu
ilikubali kuwa wewe ndo wangu wa maisha
Angelina :( anacheka)
umefurahi Sana?
Raymond :( huku
anakaa) nimefurahi (anamsogelea)
Angelina: Ramadhan atatuona…
Raymond: sijali…hata akija Christina sasa hivi na
kutushuhudia kuwa sitajali (anampigia
mama yake simu)
(simu ya mama
yake inaita)
Mrs.Bemebele :( anashtuliwa
na mlio wa simu anafikicha macho)
nani tena usiku huu? (Anaangalia simu
anakuta ni Raymond) na wewe usiku wote huu una yapi?
Raymond: amenikubali… (Anatabasamu)
Mrs.Bembele: kweli??(Anatabasamu) hongera mwanangu…
Raymond :( anampa
Angelina) ongea na mama
Mrs.Bembele :( anatoka
kitandani na kwenda jikoni)
Angelina: shikamoo mama...
Mrs.Bembele: marahaba mwanangu…Asante Kwa kumpa
furaha huyo kijana
Angelina :( anacheka)
Mrs.Bembele: laleni kesho ni siku ngumu hasa kwako
ila elewa kuwa mwenzio anakupenda sana...imetokea tu inambidi atimize hilo ili
yasiwe makubwa kwa baba yake si unaelewa?
Angelina: naelewa mama
Raymond :(
anatabasamu)
Mrs.Bembele: nakata simu, nasikia baba yenu ananifuata
(anakata simu kisha anafungua friji na
kutoa maji na kuanza kunywa)
Mr. Bembele: mna nini cha siri na Raymond?
Mrs.Bembele: umejuaje kuwa naongea na Ray?
Mr. Bembele: nimehisi tu...au unaongea na mwanaume
mwingine mama Ray?
Mrs.Bembele: hapana baby...
Mr. Bembele: enhe mlikuwa mnaongea nini na Raymond?
Mrs.Bembele: kanipigia simu kaniambia kuwa hawezi
kulala maana anawaza Sana sijui kesho itakuwaje
Mr. Bembele: wala asijali sana kila kitu kitakuwa
sawa tu
Mrs.Bembele: nimemwambia pia… (Anachukua jagi la maji kisha anaondoka)
Mr. Bembele :(
anajisemea moyoni) kuna jambo lingine tofauti hapo…unavyomchukia Christina…
(Anaguna kisha anamfuta mkewe chumbani
kwao)
(Upande wa Raymond na Angelina)
Raymond: mama amekufurahia Sana…unaona sasa
hatutakuwa na shida
Angelina: mama ni mcheshi
Raymond: na ni mpenda watu wa rika zote na tabaka
mbalimbali
Angelina :( anapiga
miayo)
Raymond: usingizi…
Angelina: Sana…
Raymond: twende…nikusindikize chumbani kwako
ukalale… (anatabasamu kidogo)
Angelina: (anaguna)
Raymond: kuwa na amani wala sitafanya chochote
kinyume na matakwa yako…
(Wanaenda moja kwa moja mpaka chumbani kwa Angelina)
Angelina: Raymond…
Raymond: usiogope, siwezi kufanya chochote
usichokitaka…kuwa na Amani nadhani nimeshakuambia
Angelina: Asante…
(Angelina
anapanda kitandani wakati huo Raymond kasimama pembeni ya kitanda, anamfunika
kisha anamuwekea neti vizuri)
Angelina: nenda kalale maana kesho ni siku kubwa
kwako
Raymond: natamani isifike… (Anazima taa kisha anatoka na kwenda chumbani kwake) nakupenda Angel
0 Comments