IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 18

 


SCENE 18: -

ENGAGEMENT DAY: -

(ni siku ya Jumamosi,jioni tulivu sana….upepo wa baharini unavuma kwa mbali,umati wa watu wapatao mia moja na hamsini wamekusanyika katika  jumba la kifahari la Raymond Mtoto wa pekee wa mfanyabiashara maarufu jijini hapo,watu wanaonekana kufurahia hali ya hewa lakini pia mandhari safi nay a kuvutia ya nyumba hiyo ya kifahari,wahudumu mbalimbali wanawahudumia wageni waalikwa…akiwemo na bibi harusi mtarajiwa(Christina),wakati watu wapo nje wakiendelea kuburudika huku wakisubiri sherehe ianze,Raymond yupo ndani tena chumbani kwa Angelina na anaonekana hana raha hata kidogo)

Angelina: Raymond…ungetoka humu ndani uende ukumbini…maana tayari watu wapo nje na wanasubiri sherehe ianze…

Raymond: kwanini usifanye juu chini hii sherehe isiwepo Angelina…nakupenda wewe nataka kukuoa wewe

Angelina: naomba nikahudumie watu…tafadhali niache nikafanye kazi yangu, tulizungumza hili mchana unakumbuka? Acha niende (anatoka)

Edmond :( anaingia ndani) Raymond…uko wapi?

Raymond :( anafungua mlango wa Angelina) nipo humu…

Edmond: (anashangaa) wewe una kichaa? Wewe ndugu unafanya nini humo?

Raymond: nimekaa tu...yaani sin ahata chembe ya furaha...hii engagement isiwepo tu Mond…I swear natamani kutoroka mwenzio

Edmond: acha ujinga embu twende mzee Bembele anakutafuta

Raymond: sitaki kutoka humu ndani…na hakutakuwa na sherehe ya pete

Edmond: acha kufikiria kitoto Raymond…watu wamejaa kishenzi halafu Mimi sikujua Kama hii sherehe itakuwa kubwa...kudadeki

Raymond: sitaki sherehe…Mimi nataka kumuoa Angelina…natoka nje sasa hivi naenda kutangaza kuwa namuoa Angelina Na si Christina

Edmond: Hiii nyie huyu chizi...embu acha uchizi Mond

Mrs.Bembele :( anaingia ndani) Raymond…baba

Angelina :( anatokea jikoni) shikamoo mama…

Mrs.Bembele :( anamshika mashavu na kutabasamu) marahaba mwanangu hujambo

Angelina: sijambo mama

Raymond :( anakuja walipo)

Mrs.Bembele: najua hii ni ngumu sana kwa nyie wawili ila Raymond toka nje ukamvalishe pete huyo  Christina

Raymond: mama… (Anamuangalia kwa huruma)

Mrs.Bembele: sina cha kukusaidia Zaidi ya kukuambia wageni ni wengi na usipomvalisha pete Christina, baba yako ataaibika…

Raymond: unamaanisha mama hata ikifika ndoa nimuoe tu Christina ili baba asiaibike? Mama Unajua kuwa nampenda Sana…

Mr. Bembele :( anatokea nje) Raymond…

(Wote wanashtuka)

Mr. Bembele: bado unavaa tu muda wote? Halafu mbona mpo chumbani kwa mfanyakazi? (Kwa Angelina) nenda nje ukawahudumie watu…Leo watu wengi Sana huwezi jua unaweza kupata mchumba

Angelina :( hajibu chochote na anatoka nje)

Mr. Bembele :( Kwa Raymond) twende baba…ni muda wako sasa kuonyesha watu kuwa unatarajia kumuoa mpenzi wako wa siku nyingi sana Christina...comeon lets go

Mrs.Bembele: twende mwanangu

Mr. Bembele: Mimi natangulia (anatoka)

Raymond: mama I can’t do this…siwezi mama kufanya hivi…iam in love with Angelina…namtaka yeye

Mrs.Bembele: do it my son…tutajua mbeleni…ila kwa sasa just do it…

Raymond: No mama

Mrs.Bembele: please

Raymond: mama

Mrs.Bembele: twende baba...no way out

(Raymond, Edmond na Mrs.Bembele, wanaelekea moja kwa moja mpaka bustanini walipo watu. watu wanapomuona Raymond wengine wanapiga makofi wengine vigelegele yaani ni shangwe na nderemo zinalipuka mahali hapo)

Mmoja wa watu: wow…Bwana harusi wetu mtarajiwa…umependeza na suti yako…

Mr. Bembele: that is my son… (Anatabasamu)

Raymond :( anamuangalia Sana Angelina aliyekuwa amesimama pembeni yake)

Catherine :( anamnong’oneza Edmond) mbona shemeji kanuna hivi

Edmond: anampenda mwanamke mwingine

Catherine: nani?

Edmond: Angelina

Catherine: mdogo wangu?

Edmond: ndio

Catherine: makubwa (anashangaa)

Edmond: nyamaza…

(Pete ya uchumba inaletwa na mmoja wa wafanya kazi wa ofisi ya Raymond)

Christina :( anafurahi Sana)

(Watu wanashangilia Sana)

Angelina :( ameinama na anajisemea moyoni) bora hata nisingemkubalia…nisingekuwa naumia hivi…bora nisingeruhusu moyo wangu umpende Raymond

Raymond :( Kwa uyonge anapiga goti moja) Christina

Watu: woyooooooooooooo…

Raymond :( anamshika Christina mkono) will you marry me?

Watu :( wanapiga kelele)

Christina :( anatabasamu)

(Mama na shangazi wa Christina wanaonekana kuwa na furaha kuliko watu wote hapo)

Christina: Yes…Raymond…I will marry you…

(Watu wanashangilia Sana)

Raymond :( ananyanyuka huku anamuangalia Angelina chinichini)

Christina :( anamkumbatia)

Raymond :( anamkumbatia pia)

Christina: I love you Raymond…

Raymond: I love you too

(Shangwe na nderemo vinatawala mahali pale, watu wanawavamia Raymond na Christina huku wengi wao wakitaka kuiona pete ya gharama aliyovalishwa Christina, wakati watu wanamzingira Christina, Raymond anatumia mwanya huo kuongea na Angelina)

Raymond :( anamvuta pembeni Angelina) Angel…

Angelina: nambie Raymond…hongera Kwa kuchumbia

Raymond :( anamuangalia usoni) nakupenda…Sana…nakupenda Angelina

Angelina: wageni wanahitaji vinywaji …naomba nikafanye kazi yangu

Raymond: Tafadhali…naomba ukae na mimi kidogo

Angelina: baba yako ni mkali sana sitaweza kubishana nae (anataka kuondoka)

Raymond: Tafadhali Angelina usichukulie hiki kitu kirahisi hivyo

Angelina :( anamuonea huruma) tutaongea Raymond...kwa sasa naomba nikahudumie watu

Raymond :( anamkumbatia na kumvalisha pete Fulani) hii sio pete ya uchumba usishtuke...ni pete tu nataka uivae kama ishara ya upendo wangu kwako…

Angelina: Asante…

Edmond :( anaonekana kama alikuwa anamtafuta saa nyingi) ah…Raymond…unaitwa unajua…na kwanini mnakaa pamoja? Watu watawashtukia

Raymond: kwani ni dhambi?

Edmond: okay sina mood ya kuongea sana, unaitwa na baba yako

Raymond :( Kwa Angelina) nenda ukapumzike ndani, acha usifanye kazi yoyote wewe ni mke wangu…ingia ndani

Angelina :( anaingia ndani)

Raymond :( Kwa Edmond) twende

(Wanaelekea ukumbini)

Mr. Bembele :( anamuona Raymond) ulikuwa wapi baba?

Raymond: chooni…

Mr. Bembele: okay…watu walikuwa wanakuulizia

Christina :( anakuja alipo Raymond) naomba tucheze...Please

Raymond: nimechoka

Edmond :( anamshika bega Raymond na kumshawishi)

Raymond :( anavuta pumzi) okay… (Anamshika kiuno na kuanza kucheza nae)

Christina: uko sawa?

Raymond: yes   …. Niko sawa…kwani vipi?

Christina: umepooza kweli

Raymond: usijali ni uchovu tu

Christina: you are now my fiancé

Raymond: (hajibu chochote anaendelea kucheza kama mtu aliyelazimishwa sana)

(Watu wengine nao wanaungana nao kucheza, sherehe inafana kwelikweli watu wanakula, na kila kitu ni burudani tupu kasoro kwa raymond)

 

Post a Comment

0 Comments