IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 19

 


SCENE 19: -

(asubuhi nyingine baada ya siku ya sherehe ya uchumba kati ya Christina na Raymond. Raymond anapata chai huku anaonekana anaperuzi kitu mtandaoni)

Raymond :( anaguna) yaani huyu mwanamke anapenda kujionyesha kweli…picha kila sehemu huko instagram…yaani (anaweka simu pembeni na kuendelea kunywa chai) huu ni ushamba, yaani kahakikisha kila mtu anaona picha hizi ushamba nao ni mzigo (anafyonza)

Angelina :( anakuja kutokea jikoni) shikamoo…

Raymond: kaka Ray… (Anacheka Kwa nguvu)

Angelina :( anacheka pia) hata nilikuwa sitaki kukusalimia hivyo…

Raymond: ulitaka kunisalimiaje? Shikamoo mume wangu au?

Angelina :( anacheka) kwani umeshakuwa mume wangu? Raymond bwana una masihala sana

Raymond: natarajia…si natarajia kuwa mumeo?

Christina :( anatoka chumbani akiwa amevaa nguo za kulalia)

Angelina :( anaangalia chini)

Raymond :( anamuangalia Angelina)

Christina: good morning my love… (Anambusu Raymond shavuni)

Raymond :( hajafurahia) morning…umeamkaje?

Christina: nimelala vizuri Sana my love yaani Nina raha kweli mwenzio

Raymond: Ni vyema Kama ni hivyo…

Christina :( anatabasamu kisha anakaa pembeni ya Raymond)

Angelina :( anaondoka)

Christina: binti niletee na mimi kikombe ninywe chai

Angelina: sawa wifi yangu (anaelekea jikoni)

Christina :( anatabasamu)

Raymond :( ananyanyuka na kuelekea jikoni) Angelina… (Anamfikia na kumshika mkono) alilala chumbani kwangu ila sijalala nae, haki ya Mungu tena…sijamgusa

Angelina: haina shida, hata Kama ulilala nae si mpenzi wako? Ni mchumba wako

Raymond: nakupenda Sana wewe Angelina, sitachoka kukuambia hilo baby…nataka mpaka uelewe ni kiasi gani nakupenda Angel

Angelina: ngoja niende nikatenge chai Kwa malkia wa nyumba

Raymond: wewe ndo malkia wa nyumba hii my love nakupenda na nitafanya juu chini nikuoe

Angelina: huku umeshatoa mahari, Kwa hiyo sina cha kutegemea hapo

Raymond: niamini… (Anamshika mikono) Angelina

Angelina: niache Christina anaweza kuja ghafla hapa ikawa msala

(Wanasikia sauti ya Christina)

Christina: wewe dada hicho kikombe unanunua Marekani?

Angelina: naleta dada... (Anarudi alipo Christina) hiki hapa dada…

Raymond :( hana raha)

Christina: njoo baby tunywe chai…Asante kwa jana usiku...Usiku ulikuwa mzuri

Raymond :( anamuangalia Angelina chinichini)

Angelina :( anamuangalia pia)

Raymond :( anapandwa hasira) Christina kuna haja gani ya kuongea hayo mbele za watu...na unaujua ukweli

Christina: si ninaongea tu my love kwani kuna uongo hapo? Mimi na wewe ni mtu na mtu wake na ni lazima watu waelewe kuwa lazima tuwe na muda mzuri pamoja… (Anamuagalia Angelina) au ninasema uongo binti

Angelina: Ni kweli dada unachosema...hujakosea dada

Raymond :( ananyanyuka kwa hasira na kwenda zake chumbani kwake)

Christina: yaani Raymond ana hasira huyu

Angelina :( anacheka kidogo kisha anaelekea nje kuendelea na kazi nyingine)

Raymond :( yupo chumbani kwake) damn this woman!!!!Yaani ana mpango wa kuniharibia penzi langu na Angelina (simu yake inaita) nani tena (anaiangalia kisha anapokea) dad…

Mr. Bembele: mwanangu…hujambo

Raymond: sijambo shikamoo?

Mr. Bembele: marahaba…sasa nilitaka kukuambia kuwa ofisi imekuandalia sherehe kidogo Kwa ajili ya kukupongeza Kwa kupata mchumba lakini pia kumaliza chuo

Raymond: dad, sherehe tena? Naanza kuchoka na hizi sherehe jamani...zimekuwa nyingi wewe huoni? Kunipongeza si tayari baba umeshanipongeza au mimi ndo sielewi?

Mr. Bembele: relax sio mimi niliyeandaa ni wafanyakazi wako

Raymond: lini na saa ngapi?

Mr. Bembele: kesho jioni

Raymond: sawa dad…hakuna shida nitakuwa hapo… (anakata simu)

Post a Comment

0 Comments