IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 20

 


SCENE 20:

(majira ya saa moja jioni, Raymond anaingia ukumbini akiwa na Angelina na wamependeza sana, ukumbi umependeza watu wamefurika kuna onekana kuna vyakula na vinywaji vya kutosha, kuna muziki na burudani ya kutosha na kila kitu kinaonekana kinaenda vizuri, wakati Raymond na Angelina wanaingia, baadhi ya wafanyakazi wa ofisi ya Raymond wanawaona na wanajikuta wanavutiwa na muonekano wa wawili hao)

 Rachel: jamani ona bosi Raymond alivyopendeza jamani mpaka raha mpaka nimependa

Pendo: tena huyo dada ndo kamfanya apendeze Zaidi…dada mzuri huyo

Rachel: Ni nani?

Pendo: msichana wake wa kazi shoga yangu

Rachel: wow…mbona mzuri kuliko yule shoga kidawa yaani ni Mrembo hatari…duh Raymond si amchukue

Pendo: si ajabu keshajichukulia…

Christina :( ambae yuko hapo muda wote miongoni mwa watu) yaani Raymond ana dharau Sana huyu mwanaume yaani ameniambia nitangulie kumbe anakuja na dada wa kazi jamani?

(Wakati huo Raymond hata hajali)

Mrs.Bembele :( anamfuata Raymond na Angelina) sikujua kuwa mnaendana hivyo yani mmependezeana...Mungu awatunze

Raymond: Asante mama, tumependeza eeh

Mrs.Raymond: sana

Angelina :( anacheka Kwa aibu)

Mr. Bembele :( nae anakuja) Raymond ndo nini hiki?

Raymond: sijaelewa dad…nini?

Mr. Bembele: mchumba wako amekuja peke yake halafu wewe upo hapa na hausigeli

Raymond :( anacheka kidogo ingawa sio kwa furaha) yaani dad…hicho ndo kitu cha kunigombezea mimi? Angelina ninaishi nae na nilitaka nije nae kwahiyo ningemuacha nyumbani kisa ni hausigeli

Mrs.Bembele :( anampooza Raymond) basi baba…msigombane…ona watu wanawaangalia Sana…mtazungumza

Mr. Bembele: naomba uende kwa Christina na uwe nae hii sherehe ni yako na christina sio na huyu housegirl

Angelina :( anaangalia chini)

Mrs.Bembele: Raymond nenda tu mwanangu …nenda baba

Mr. Bembele: sasa hivi…

Raymond :( anaondoka huku anamuangalia Sana Angelina)

Mrs.Bembele :( anamshika mkono Angelina) twende mwanangu

Mr. Bembele: aende wapi abaki hapa…na kwanza yeye si kijakazi? christina amejisikia vibaya sana, kila mtu alikuwa anawasifia walipoingia (kwa Angelina) wewe si unajua kuwa Raymond ni mchumba wa mtu?

Angelina: ndio baba…

Mr. Bembele: usiniite baba…Mimi sio baba yako, siwezi kuwa baba yako wewe maskini

Mrs.Bembele: kwani yeye kasema wewe ni baba yake si kakuita tu kiheshima

Mr. Bembele: Gloria kwanini unapenda Sana kumtetea huyu kijakazi aliyekuja kuharibu sherehe Za watu?

Mrs.Bembele: hajaharibu sherehe za watu, basi fanya unavyotaka

Mr. Bembele: haraka (Kwa Angelina) nenda kagawe vinywaji na hilo gauni zuri sijui nani kakununulia au umepewa na mkwe wangu

Mrs.Bembele: jamani baba Raymond ni maneno gani hayo makali unayoongea kwa binti wa watu?

Mr. Bembele: huna mamlaka ya kunihoji…

Mrs.Bembele: Nina mamlaka baba Ray…usishau mimi ni mkeo

Mr. Bembele :( Kwa Angelina) unaona wewe binti unayoyasababisha ugomvi kwenye familia yangu,mke wangu na mwanangu wote wanakutetea wewe umetoka na uchawi gani Ngara?

Angelina :( kimya)

Mrs.Bembele :( Kwa Angelina) nenda mwanangu ukafanye kazi zako

(Angelina anaondoka na kwenda kugawa vinywaji)

Pendo:(anamuona Angelina anagawa vinywaji) jamani Mrembo anagawa vinywaji(anamfuata)wewe kuna watu wamewekwa kwa ajili ya hii kazi wewe tena umeingia na boss kazi yako ni kufurahia maisha, halafu wewe na bosi mmedamshi kweli yaani hivi mmejiona?

Angelina :( anacheka kidogo)

Pendo: acha kuhudumia shoga yangu tukae wote

Mr. Bembele :( anajitokeza kwa nyuma yao) unamwambia aache kuhudumia wewe kama nani?

Pendo: He!!!Makubwa!!!

(Upande alipo Raymond na Christina)

Christina: yaani wewe mwanaume una dharau Sana…yaani umeniacha nije peke yangu halafu wewe ukaja na msichana wa kazi…

Raymond :( anampuuzia)

(Edmond na mpenzi wake wanaingia ukumbini hapo na Raymond anawaona bila kupoteza muda anawandea)

Raymond: karibuni jamani mmependeza

Edmond: hatukuzidi…

Catherine: habari za jioni shemeji

Raymond: salama shemeji yangu karibu Sana hapa kwetu

Catherine: Asante (anaangalia angalia huku na huku kama mtu anayetafuta kitu) simuoni Angelina hajaja?

Raymond: yupo na mama yangu… (Anaangalia angalia huku na huku anamuona Angelina amebeba trei la vinywaji anapita kwa watu na kugawa vinywaji) what???!!!My woman? Anagawa vinywaji? (Anamfuata)Angelina kwanini unafanya hivi?

Angelina: niache Raymond tafadhali hii ni kazi yangu na sitaki ugomvi…we endelea na sherehe imepangwa kwa ajili yako na mchumba wako

Raymond: lakini…

(Anakatishwa na tangazo Fulani linalotangazwa na baba yake)

Mr. Bembele: jamani habari za jioni mabibi na mabwana…ninatumaini mnafurahia usiku huu mtulivu

Watu: Sana

Raymond :(macho yote kwa Angelina ambae anaendelea kugawa vinywaji)

Mr. Bembele: nimeomba utulivu ila naona wapo wadada wengine sijui wamelelewa vipi na wazazi wao bado wanafanya mambo yao kama wewe binti unaegawa vinywaji huwezi kujiongeza kuwa kuna mtu yuko hapo mbele anahitaji utulivu?

Christina :( anacheka Sana)

Shangazi yake Christina: acha kucheka shoga yangu

Christina :( anaacha) yaani amepewa la usoni

Shangazi: we acha tu (anacheka pia)

Raymond :( anachukia Sana)

Mrs.Bembele :( nae anaonekana kuchukia)

Mr. Bembele: tabia za kimaskini hizo (anajichekesha kidogo) tuendelee tafadhali na endeleeni kufurahia maisha yenu binafsi… (Anashuka na kuendelea na shughuli nyingine) cheers to my son and his fiancée

Watu: cheers (wanagonga glasi)

Raymond :( anamfuata Angelina) Angel…nakupenda sana na naomba hilo uliweke kichwani kuwa nipo kwa ajili yako mpenzi wangu nakupenda mno…tafadhali kama hutajali naweza kukupeleka nyumbani tukawe na sherehe yetu wawili tu mimi na wewe baby…

Angelina: acha niendelee na kazi zangu… (Anaondoka alipo Raymond)

Raymond :( bado anamfuata Angelina) najua umejisikia vibaya sana kwa alichosema baba mbele za watu naomba unisamehe mimi Angelina

Angelina: nimeshakusamehe naomba uende kwa mchumba wako

Edmond na Catherine :( wanawaangalia Angelina na Raymond)

Edmond: yaani hili penzi lina vita Sana, sijui Kama litafika mbali

Catherine: wenyewe tu wanatakiwa wawe na msimamo wasipokuwa nao lazima wataachana tena hivi karibuni

Edmond: yaani mzee Bembele hampendi kabisa Angelina

Catherine: yaani… (Anatikisa kichwa ishara ya kusikitika)

Edmond: embu tuendelee na mambo yetu

(Watu wanaendelea kufurahia sherehe ile, wengine wanakunywa, kuna wanaocheza, wanaokula, wanaocheka, huku Angelina akionekana kufanya kazi yake kiufasaha, huku Raymond akionekana hana raha na sherehe hiyo)

Raymond: Angel…please baby

Angelina: please ndo nini sijasoma Mimi

Raymond: naomba unisikilize

Angelina: nenda kwenye sherehe

Raymond: twende nyumbani

Angelina: kamwambie mchumba wako (anaondoka zake)

(Raymond anabaki akiwa mnyonge Sana)

Post a Comment

0 Comments