IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 21

 


SCENE 21: -

(Mr. Bembele na mke wake pamoja na wazazi wa Christina na Christina mwenyewe wanafika nyumbani kwa Raymond wakionekana kuna jambo muhimu sana wanataka kuzungumza nae, wanapofika wanapokelewa vizuri sana na Angelina ambae alikuwa anafanya usafi wa ndani)

Angelina :( anawasalimia Kwa heshima Sana) shikamooni...Karibuni

Mama Christina :( anabenjua midomo)

Shangazi :( anabenjua midomo pia)

Christina :( anabenjua midomo)

Baba Christina :( anaachia tabasamu) marahaba mama

Mrs.Bembele: marahaba mama hujambo

Mr. Bembele: ndo umeamka sasa hivi utasema wewe ndo malkia wa nyumba hii

Raymond :( anatokea chumbani) dad…

Mr. Bembele: huyu mtoto…anajiona malkia wa humu ndani…anaamka saa nne

Raymond :( anaona ampuuzie) karibuni ndani (Kwa Angelina) nenda kaendelee na kazi nyingine achana na hii kazi kwanza utakuja kuendelea baadae

Angelina: sawa (anaondoka)

Mr. Bembele: sema sawa boss

Angelina: sawa boss (anaondoka kuelekea jikoni)

Raymond :( yupo kimya huku anaonekana kukasirishwa Sana)

Mrs.Bembele :( anamshika bega mwanae)

Raymond: karibuni Sana

(Kwa pamoja wanaingia ndani maana muda wote walikuwa wanaongelea nje)

Baba Christina: habari za hapa mwanangu…

Raymond: salama kabisa baba… (Kwa wote) shikamooni

(Wote wanaitikia ikiwemo na christina)

Mr. Bembele: za hapa mwanangu…?

Raymond :( sio Kwa furaha) salama kabisa za huko?

Mr. Bembele: ila mbona unaonekana kutokuwa na raha na mimi mwanangu?

Raymond: wasiwasi wako tu mi mbona nipo sawa

Mr. Bembele: sasa sisi hatutachukua muda mwingi hapa tunajua umechoka na unahitaji kupumzika…

Raymond: sawa nawasikiliza tu…

Mr. Bembele: mwanangu mbona Jana ulimuacha mchumba wako na kuingia na msichana wa kazi ukumbini unajua hiyo haikuwa picha nzuri hata kidogo…unadhani mchumba wako alijisikiaje?

Raymond :( anacheka kidogo) dad…hicho ndo kitu ulichokuja kuniambia? Mi nilichelewa kujiandaa ndo maana nikamwambia Christina atangulie ukumbini na kuhusu kuja na Angelina sikuona haja ya kumuacha…nyumbani

Mr. Bembele: nakuamuru mimi kama baba yako uweke ukaribu Zaidi na mchumba wako na sio msichana wa kazi na pia nimepata habari kutoka hata kwa Ramadhani kuwa upo karibu na msichana wako wa kazi

Raymond: Hilo nalo ni tatizo…baba kwamba kuwa karibu na mtu anayekupikia nalo ni tatizo?

Mrs.Bembele :( Kwa Raymond) baba tulia acha kujibizana na baba yako

Raymond :( kimya)

Mr. Bembele: huyu mtoto anajifanya anajua Sana, una kiburi Sana je hivi ndo unanifanyia baada ya kukupa kila kitu?

Raymond: kwahiyo umenipa kila kitu ili unitawale? Nisiwe na uhuru…okay navirudisha vyote…na huyo Christina simuoi

(Wote waliokuwepo hapo wanabaki mdomo wazi)

Mama Christina: baba usiseme hivyo

Raymond: Mimi Nina uhuru wa kuishi navyotaka…na sitaki kumuoa Christina wala sitaki hii nyumba, kazi, gari wala chochote kile

Mr. Bembele :( anajishusha) mwanangu umepaniki

Raymond: sijapaniki hata kidogo naongea nikiwa na akili timamu ni kwamba sitaki kumuoa Christina na bora mmekuja wote ili niwaambie vizuri kabisa kuwa sina nia ya kumuoa Christina…

Christina: kwanini ulikubali kunivisha Pete ya uchumba?

Raymond: ilikuwa ni presha kutoka kwa baba…sina mpango wa kukuoa Christina

Mrs.Bembele :( anamshika bega) mwanangu

Mr. Bembele: Mama Ray…tafadhali mshawishi mwanao kuwa itakuwa aibu Sana tumeshaalika watu wengi sana

Raymond: watakuja kushuhudia yangu na mwanamke mwingine…baba kosea vyote ila usikosee kuoa au kuolewa utajuta maisha yako yote, sipo tayari kukosea sitaki kujuta mimi baba

(Wote wanabaki wanamshangaa)

Baba Christina: mwanangu…Raymond…mi naona kabisa umechukia Sana, baba yako anavyokusukuma mambo mengi msamehe nay eye ni mzazi anataka kuona mwanae una furaha najua unaongea kwa hasira msamehe baba yako na tusamehe sote

Raymond :( kimya huku ameangalia chini)

Shangazi: tusamehe baba…tumekosa Sisi…yaishe mwanangu

Mr. Bembele: nisamehe mwanangu sitakusukuma tena…ila tu naomba usiuvunje huu uchumba tafadhali

Raymond :( anashusha pumzi kama mtu aliyechoka) sawa haina shida...

Mr. Bembele: Asante mwanangu…

(Kila mtu anaonekana amepata Amani Fulani)

Mrs.Bembele :( anamuangalia Angelina ambae yupo jikoni ambapo mtu kama umekaa sebuleni unamuona aliopo jikoni na aliyopo jikoni anamuona mtu aliyopo sebuleni kwa kifupi kuna uwazi)

Angelina :( anamuangalia Mrs.Bembele kisha anatabasamu)

Mrs.Bembele :( anamuangalia pia kisha anatabasamu)

Mr. Bembele: Mama Ray…twende... (Anaangalia anapoangalia) unaangalia nini?

Mrs.Bembele: hakuna jipya

Mr. Bembele: na wewe unamfurahia huyo dada?

Mrs.Bembele: twendeni

(Wote waliokuja wananyanyuka na kuondoka wakiwa wanasindikizwa na Raymond)

Raymond :( akiwa amewafikisha kwenye magari waliokuja nayo) haya jamani fikeni salama mi ngoja nirudi kulala

(Wanaagana kisha wanapanda kwenye magari na kuondoka)

Raymond :( anarudi ndani anamkuta Angelina anaendelea na usafi anamkumbatia) malkia wangu

Angelina :( anahangaika kujitoa kwake) Raymond…je Kama hawajafika mbali na wakatukuta tupo hivi?

Raymond: hawawezi kurudi hata kwa bahati mbaya… (Anamvuta na kumpakata) natamani nitangaze ndoa yetu hata jumapili hii

Angelina: baba yako atatunyonga…

Raymond: nikikuoa kisiri ataniua?

Angelina :( anacheka Kwa aibu)

Raymond: nakupenda sana mpenzi wangu na ninataka nikuoe Angel…

Angelina: nakupenda pia (ananyanyuka)

Raymond: ukizaa watoto watakuwa wazuri

Angelina :( anacheka huku anaenda jikoni) Asante…nitakuzalia usijali

Raymond: ngoja nikalale…nisije nikajikuta nafanya dhambi hapa (anaingia ndani kwake na kupanda kitandani kisha analala huku jikoni Angelina anaendelea na kazi zake kama kawaida) kesho nitaenda kuongea na Christina jambo Fulani ni muhimu nimuone kesho (anapanda kitandani na kujilaza)

 

Post a Comment

0 Comments