IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 22

 


SCENE 22: -

(majira ya saa kumi na mbili jioni, mara baada ya kazi Raymond anaamua akamuone Christina ili azungumze nae mawili matatu, anapanda gari lake kisha analiondoa kuelekea katika jumba la kifahari la kina Christina baada ya mwendo wa kama nusu saa anafika nyumbani hapo, anawakuta Christina na mama zake wamekaa barazani wakizungumza umbea kama kawaida yao, anawasalimia kwa heshima kubwa)

Raymond :( anatabasamu kidogo) shikamoo mama, shikamoo shangazi…

Mama na shangazi :( wanaitikia) marahaba baba…karibu

Raymond: Asante (Kwa Christina) habari za hapa?

Christina: nzuri karibu (ananyanyuka na kuelekea ndani) karibu ndani

Raymond :( anamfuata ndani) Asante… (Anaingia ndani)

Christina :( anakaa kwenye sofa)

Raymond :( nae anakaa kwenye sofa)

Christina :( anajaribu kumkalia)

Raymond: hapana…sipo tayari Kwa sasa

Christina: una maana gani?

Raymond: naomba utulivu…

Christina: okay…ungependelea kinywaji gani…my love?

Raymond: no thank you…nipo sawa…

Christina: at last…tupo pamoja baada ya muda Mrefu… (Anacheka kidogo lakini tabasamu linapotea mara baada ya kugundua kuwa Raymond hayuko nae yaani ana mawazo mengine) vipi Raymond uko sawa baby?

Raymond :( kimya huku anaonekana hajui aanzie wapi)

Christina: talk to me baby…whats wrong.

Raymond :( kimya)

Christina: kuna sehemu nimekuudhi?

Raymond: hapana hakuna sehemu uliyoniudhi ila kuna jambo nataka kukuambia na sijui nianzie wapi

Christina: kuwa huru baby…nakusikiliza…

Raymond: iam ni love with someone else… (Kimya kidogo) sijui ilianzaje but kuna mwanamke nampenda Sana na siwezi kuficha tena kwa watu nataka niwe nae…yeye ndo ananipa Amani ya moyo…nampenda sana

Christina :( anakasirika Sana huku machozi yanamlenga) you cannot be serious Raymond…

Raymond: Kwa bahati mbaya nipo very serious…nipo very serious Christina

Christina :( Analia) tumekaa pamoja miaka mingi sasa tunakaribia kuwa mke na mume unaniambia kuwa una mwanamke mwingine na unampenda sana…

Raymond: iam so sorry sikupanga yote haya mama, yaani hata Mimi naumia kila nikatafakari…naona nimekufanyia unyama ila imetokea na kila siku nampenda zaidi ya jana…

Christina: hatuwezi kuachana Raymond…

Raymond :( Kwa mshangao) kwanini?

Christina: our wedding is around the corner watu watanifikiriaje Mimi na familia yangu…basi nioe utanipa talaka mbele ya safari…

Raymond: iam so sorry siwezi kufanya hivyo hata nikitaka…haiwezekani namuoa huyo dada ambae nafsi yangu imeniridhia…iam so sorry Christina

Christina: (bila kutarajia) iam pregnant…

Raymond :( kwa mshangao) what?!!!

Christina: yes…Nina ujauzito wako Raymond

Raymond: mbona hukuniambia mapema Leo ndo unaniambia?

Christina :( anafuta machozi) nilitaka iwe surprise…ila leo umenijia na hili nimeona tu nikuambie tu

Raymond: Ina muda gani?

Christin: miezi miwili...

Raymond: lakini mbona hiyo miezi miwili hatukutana kimwili tumekutana juzi tu…inamaana Kama mimba labda ina mwezi hivi na sio miwili au umechanganya...

Christina :( anajiumauma) kitu Kama hicho sina uhakika…

Raymond: okay nionyeshe matokeo au kipimo cha mimba si umepima?

Christina: sijui niliyaweka wapi…

Raymond: una uhakika una ujauzito?

Christina: ndio unaona nakudanganya au?

Raymond: iam a doctor kesho njoo hospitali kwangu nitakupima

Christina: inamaana huniamini au?

Raymond: hapana sio hivyo nachotaka ni kujua hiyo mimba ina muda gani…maana wewe mwenyewe hujiamini na wala huna uhakika

Christina: okay mi nitakuja kesho kupima ila je ikiwepo itakuwaje?

Raymond: sitaukimbia wajibu wangu Kama baba wa huyo mtoto

Christina: kwahiyo tutaoana?

Raymond: hapana hatutaoana…tutakuwa tu wazazi wenza…na mwanamke wangu nitamwambia juu ya hilo

Christina: huyo mwanamke ni nani?

Raymond: sitapenda kumuweka wazi kwanza mpaka pale baba atakapomkubali…

Christina: you are such an animal and I hate you so much…

Raymond: iam sorry I love her too much...Yaani mpaka nimeamua kukuambia Ni kwamba I cannot control my feelings anymore

Christina :( anasikitika huku Analia) ninakupenda Sana Raymond…

Raymond: iam so sorry...
Christina: haina shida lakini

Raymond: okay (huku ananyanyuka) kesho usisahau kuja ofisini kwangu tuangalie hiyo mimba ni ya muda gani…

Christina: sawa…

(Kwa pamoja wanatoka nje walipo mama na shangazi yake Christina, Raymond anawaaga kisha anapanda gari lake na kuondoka)

Christina :( anaguna)

Mama: mwenzetu vipi?

Christina: acha tu…

Shangazi: tatizo nini?

Christina: Raymond ameachana na mimi

Mama: kisa nini?

Christina: eti anampenda mwanamke mwingine...

Shangazi: halafu alivyo ana dharau mshenzi huyu…anakuambia kabisa yaani mtoto hana haya huyu (anafyonza)

Christina: kizaazaa kinakuja nimemdanganya kuwa Nina mimba…huku sina na wala sijui naitoa wapi sasa hivi...

Mama: we endelea tu kumdanganya mpaka pale tutakapopata ufumbuzi mwingine…

Christina: amesema kesho niende akanipime

Shangazi: usiende

Mama: asipoenda atakuja hivi unamjua Raymond unamsikia?

Shangazi: sasa tufanyeje

Christina: kwa sasa sijui cha kufanya natamani ardhi ipasuke niingie ili hiyo kesho nipate kisingizio kuwa ardhi ilipasuka nikaingia...

(Shangazi na mama wanacheka sana)

Post a Comment

0 Comments