SCENE 23:
(Asubuhi nyingine tulivu na njema, upepo Fulani mwanana unavuma kwa
mbali, Christina anafika ofisini kwa Raymond anapofika anaenda moja kwa moja
mpaka alipo nesi ambae walizungumza nae kuhusu masuala ya ujauzito)
Christina: za asubuhi shoga yangu
Imelda :( nesi)
salama mambo vipi shoga?
Christina: poa…
(Wakati huo Raymond
anatokea ofisini kwake na anaonekana hayuko bize sana na anatembeatembea
kuwasalimia wafanyakazi wake)
Raymond :( Kwa
sekretari wake) yaani Glory...Kwa kuchelewa wewe hujambo
Glory :(
anacheka) jamani Raymond
Raymond :( anatabasamu
huku anaangalia upande alipo Christina) yule si Christina?
Glory: ndo yeye
Raymond :(
anamuita) Tina…
Christina :( anageuka
anaona anayemuita ni Raymond anatoa macho kama mjusi kabanwa na mlango)
Raymond...Nilipita kumsalimia Imelda…nakuja tangulia
Raymond: twende ofisini maana nataka kutoka…kuna
sehemu naenda (anaingia ofisini kwake)
Christina :(
anamfuata)
Raymond: karibu uketi…
Christina :( anaonekana
hana Amani kabisa)
Raymond: vipi? Mbona unaonekana huna raha?
Christina: hapana mbona nipo kawaida?
Raymond: ulisema una mimba eeh…
Christina :(
anakuwa na kigugumizi) …. ndi…o
Raymond: sawa lets comfirm it!!Kama una mimba nitatunza
mtoto na wala sitakimbia majukumu yangu ila nikigundua kuwa
unanidanganya…nitakasirika sana…
Christina: okay haina shida…
Raymond: okay… (Ananyanyuka
na kuchukua kipimo cha mimba na kurudi kukaa, anampa kichupa) kalete mkojo
Christina :(
anaonyesha kutetemeka)
Raymond: vipi? Mbona unatetemeka?
Christina: hapana Raymond…kawaida tu (anachukua kichupa kisha anatoka nje)
Raymond: mbona hata humu ofisini kwangu kuna
choo…ingia humo
Christina :( anaingia
chooni) Mungu wangu (anachukua mkojo)
nitafanya nini Mimi Leo?
Raymond :(
akiwa bado amekaa kwenye kiti chake) najua unanidanganya Christina…
Christina :(
anarudi na mkojo kwenye kichupa kidogo na kumpa Raymond) halafu nilisahau
kukuambia
Raymond: ulisahau nini?
Christina: mimba ilitoka…nahisi Mimi bila kujua
Raymond :( anacheka
kidogo) we nenda tu nje nitakuita baada ya muda…
Christina :( anatoka
akiwa anatetemeka)
Raymond: hata sijisumbui kupima huu mkojo ni kwamba
tu hana mimba… (Anachukua simu ya mezani
na kumpigia sekretari wake) Glory naomba umwambie Christina arudi ndani
namuita…
Glory: sawa boss (anamuita Christina) dokta anakuita
Christina :( anaingia
akiwa mnyonge Sana)
Raymond: mbona u mnyonge Sana? Tatizo nini?
Christina: hamna tatizo
Raymond: kwanini usifurahi kuwa unaenda kuwa mama
Christina :(
anaonyesha kutoelewa kitu) una maana gani?
Raymond: sina maana yoyote ni kwamba umekuja
kwangu…nikupime mimba inamaana unatakiwa ufurahi kuwa hatimaye unaenda kuwa
mama lakini wewe tangu umeniletea mkojo niupime huna raha tatizo nini?
Christina: hakuna tatizo Raymond
Raymond :(
anasimama na kumshika bega lakini ghafla anambinya kwa nguvu na kwa hasira)
kwanini umenidanganya kuwa una mimba yangu?
Christina: Raymond… (Analengwa na machozi)
Raymond :( anapaza
sauti) kwanini lakini Christina
Christina :(
anaanza kulia) sikuwa na njia nyingine ya kukufanya ubaki kwangu Raymond…sikutaka
kukupoteza Raymond nakupenda
Raymond: pumbavu…kabisa…sasa umenipoteza umekaa na
mimi miaka yote hiyo ila inaonyesha kuwa hujui ninachokichukia…nachukia uongo (anamsukuma)
Christina :( anaangukia
kwenye sofa)
Raymond: nilitaka ubaki kuwa rafiki yangu lakini
hata huo urafiki nauvunja siutaki tena…. i hate you
Christina: naomba unisamehe sana mpenzi wangu na
tusahau yaliyopita Raymond…usiniache (ananyanyuka
na kumfuata aliposimama maana muda wote huo wanaongea Raymond alikuwa amesemama)
naomba unisamehe Raymond tuendelee kuwa wapenzi sitajali hata nikiwa spea tairi
(anapiga magoti) nisamehe Raymond
jamani…naomba unisamehe
Raymond: nyanyuka na usirudie kunipigia magoti na
ninakuomba uondoke na ukapumzike…sikusamehe Christina umenikosea sana
Christina: nipe adhabu nyingine ila usiniache Raymond…
Raymond:toka ofisini kwangu wewe ni shetani kama tu
umeweza kunidanganya kitu kidogo…je nikikuoa si utanidanganya mambo mengi na
makubwa?siwezi kuwa mpenzi wako hiyo pete uliyo nayo mkononi ni ya thamani sana
na unaweza kuiweka kama zawadi yangu kwako kuanzia leo sitaki kukuona hata
kidogo usinijue usinipigie wala usinitafute kwa njia yoyote ile mimi na wewe ni
basi kabisa…sitaki tena umenidanganya vya kutosha kuwa umeachana na Peter huku
bado upo nae…leo tena umenidanganya
mimba sijui kesho utanidanganya nini I can’t take that risk…so it is over…haya
nje mara moja…
Christina: nisamehe nakuomba
Raymond :( anachukua
simu ya mezani na kupiga kwa walinzi) naomba mje mmtoe nje kuna mtu analeta
fujo
Christina: imefikia huko Raymond…
(Walinzi wanakuja na kumshika Christina na kumtoa nje)
Raymond:(anakaa
chini huku amejiinamia kwa mbali anasikia sauti nyororo ya kike inamuita
ananyanyua uso na kukutana na kipenzi chake yaani Angelina) Angel…malaika wangu
(ananyanyuka na kumkumbatia) asante
kwa kuja mama nakuhitaji sana wakati huu
Angelina: nimemuona Christina anaburuzwa kuna nini?
Na mbona wewe unaonekana una mawazo Sana
Raymond: nikumbatie mpenzi…nachohitaji ni faraja
yako…nina hasira sana
Angelina :( anamkumbatia)
punguza hasira
Glory :( anaingia
bila hodi anawakuta wamekumbatiana) oh…samahani (anafunga mlango haraka na kurudi ofisini kwake)
Raymond: Christina muongo Sana…Jana nilienda
kumwambia ukweli juu ya penzi letu, akaniambia hawezi kuniacha maana ana
ujauzito wangu…kumbe Ni uongo…
Angelina: wewe umejuaje kuwa Ni uongo?
Raymond: tabia yake tu tangu amefika nikawa
siielewi
Angelina :( anamsikiliza
kwa makini)
Raymond: nilimuuliza na bila uoga akajibu kuwa
ilibidi afanye hivyo ili asinipoteze…nimemuacha simtaki tena katika maisha
yangu mwanamke ni muongo sana huyu…
Angelina: basi…punguza hasira…
Raymond :( anashusha
pumzi kisha anabadilisha mada) nambie sasa umekuja kufanya nini? (Anampakata)
Angelina: kukusalimia tu…nimeona nyumbani sina mtu
wa kuongea nae
Raymond: Safi Sana…usiongee na Ramadhani yaani nina
wivu kama wa ngedere
Angelina :( anacheka
Sana) inabidi upunguze usiwe na wivu mpenzi wangu...Wivu hubomoa
Raymond :(
anacheka pia) serious Nina wivu sitaki ukae peke yako na Ramadhani ni mhuni
sana sitaki kabisa akuzoee wala umzoee sawa ee
Angelina: sawa nakusikiliza wewe mpenzi...Nakuahidi
sitakaa nae karibu nakusikiliza wewe (anatabasamu
kisha anamkumbatia Kwa mahaba mazito mpenzi wake huyo)
Raymond: nikumbatie tena…nafurahi kukuona Angelina
wangu mpenzi
Angelina :( anamkumbatia)
utazoea bwana
Raymond: kumbe wewe sio mshamba Kama nilivyokuwa
naona (anacheka)
Angelina: kwahiyo Mimi mshamba
Raymond: nakutania jamani sio ukweli bwana
Angelina: sitaki bwana
Raymond: nakupenda Sana…na ninakuhitaji sana
Angelina :(
anatabasamu) hata Mimi nakuhitaji Sana Raymond…
(wanaendelea kucheka na kuongea huku kila
mmoja wao anaonekana kufurahia uwepo wa mwenzie na wanaonekana wamezama kabisa
katika penzi zito na wala hawajali kama kuna mtu atakuja na kuwakuta katika
hali ile, ni shangwe kati yao na mara kwa mara wanaangaliana, wanatabasamu,
wanafurahi yaani kwa ujumla ni Amani tu kati yao)
Glory
:( anawachungulia) jamani wanaonekana
wanapendana hao …hapo sasa boss amepata mwanamke sio yule kigagula mwanamke ni
mcharuko huyo kha!!
Angelina:
acha Mimi niende nimekusalimie
Raymond:
tukae wote bwana kwanza leo sina kazi nyingi sana
Angelina:
unaonekana huna kazi maana umekaa tu
Raymond
:( anacheka) kwahiyo nimekaa tu Kama
zombie
Angelina:
zombie ndo nini?
Raymond:
Leo tukaangalie muvi ya zombie utawajua tu... (anacheka kwa nguvu)
Angelina:
wanaonekana kuogopesha Sana
Raymond:
kumbe unawajua
Angelina:
nimehisi tu
Raymond
:( anacheka)
Angelina
:( anacheka pia)
0 Comments