IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 24

 


SCENE 24: -

(Ni asubuhi nyingine njema kama ilivyofanywa Na bwana, watu wanaonekana kuanza kazi zao za siku Kama ilivyo kawaida, Angelina yupo jikoni anaandaa chai huku anaimba wimbo mmoja wa kumsifu Mungu)

 Raymond :( anakuja nyuma yake na kumkumbatia) wow una sauti nzuri sana bibie… (Anacheka kidogo) umeamkaje lakini?

Angelina: salama… (Anamsukuma) wewe wazazi wako wakija ghafla je…?

Raymond: I do not care…yaani hata sijali kwakweli

Angelina: yaani wewe…litakukuta jambo si unawajua wazazi wako tena hasa baba yako

Raymond: hata sijali mwenzio Asante kwa upendo…wako (anataka kumbusu)

Angelina :( anachengesha) Raymond ulisema utasubiri…

Raymond :( anacheka) haidhuru kitu ila uko sawa bwana… (Anacheka) haina shida mke wangu…

Angelina: kaa hapo nikuletee chai…

Raymond: hapana we huoni nimeshajiandaa nataka tutoke nikupeleke shopping ukanunue nguo, viatu na simu mpya nataka uwe mke wangu na nitafanya kila kitu uwe wa hadhi yangu…usiichukulie vibaya hiyo…haya cha kufanya nenda kavae tutoke mke wangu

Angelina :( anacheka Sana) sawa nipe dakika kadhaa nikaoge na kubadili nguo…

Raymond :( anaguna) sasa hapo nitalazimika kukaa na kunywa chai maana nyie kuoga na kuvaa ni mnachukua miaka hata mia… (Anachukua chai na kujitengea mezani na kuanza kunywa)

Angelina :( huku anaingia chumbani kwake) nipe dakika 20 tu

Raymond: sidhani Kama hizo dakika 20 utakuwa tayari

(Angelina anaingia chumbani na kuanza kuoga na baada ya muda kidogo anamaliza kuoga, anavaa harakaharaka kisha anatoka na kumkuta Raymond bado anakunywa chai)

Angelina :( anatabasamu) mi si nilikuambia? Nachukua dakika chache sana kumaliza maandalizi

Raymond :( anamalizia kunywa chai) haya twende au tusubiri unywe na wewe?

Angelina: hapana…twende tu (anatoa vyombo alivyotumia Raymond) haya tayari twende tu…

Raymond :( anachukua funguo wa gari, kisha yeye pamoja na mpenzi wake wanatoka nje na kupanda gari) baby uko poa? (Anamfunga mkanda kisha analiwasha gari)

Ramadahani: naona mnaenda matembezi

Raymond :( anatabasamu) baadae kidogo

Ramadhani :( anafungua geti na kuruhusu gari liondoke)

(Raymond na mpenzi wake wanaondoka kuelekea duka la nguo moja maarufu, njiani wanaongea mambo mengi na angelina anaonekana kuifurahia safari hiyo. Baada ya mwendo wa karibia nusu saa hatimaye anafika dukani)

Raymond :( huku anashuka kwenye gari) haya tumeshafika baby...

Angelina :( nae anashuka kutoka kwenye gari)

(Wanaingia ndani ya duka na kuanza kuchagua nguo)

Angelina: nisaidie kuchagua nguo maana Mimi hata sijui kuchagua

Raymond: usijali mpenzi wangu, Mimi mjanja ndugu yangu (anacheka kidogo) hapa umefika

Mdada wa mapokezi :( anatabasamu)

Raymond :( Kwa dada) vipi dada mbona unanicheka?

Mdada: hapana sikucheki nakuangalia tu unavyompenda mke wako…

Raymond: Ni malkia wangu ni lazima nimpende

Mdada: hiyo ni kweli yaani hadi raha mnaonekana mnapendana sana (anatabasamu) basi endeleeni kuchagua…

Raymond :( anaendelea kumchagulia nguo Angelina wake)

Angelina :( anaonekana kufurahia)

Raymond: mke wangu…chukua hii ukajaribu tuone itakukaaje? (Anamuita mhudumu) njoo uende ukamsaidie malkia wangu kuangalia hii nguo

Mhudumu: sawa haina shida (anamuongoza Angelina mpaka chumba cha kubadilishia nguo)

Raymond :( anaendelea kuchagua nguo)

Mhudumu :( yupo ndani na Angelina) imekukaa vizuri sana

Angelina: ila ni fupi sana...

Mhudumu: kamuonyeshe mumeo…atafurahi yaani imekupendeza Sana

Angelina: hapana ni fupi sana

Mhudumu: si unaenda kumuonyesha mumeo?

Angelina :( anajikuta anaona aibu)

Mhudumu: twende bwana

(Wanatoka)

Raymond :( anageuka na anakutana na Angelina akiwa ndani ya gauni moja matata) wow… (Anamuangalia umbo lake lilivyo zuri) umeumbika jamani

Mhudumu :( anacheka) yaani unavyomuangalia…Kama sio mkeo...Limemkaaje?

Raymond: amependeza sana jamani nimebahatisha…

(Mdada WA mapokezi na mhudumu wanacheka)

Raymond: hili tutalichukua…

(Wanaendelea kuangalia nguo nyingine na viatu na wakati huo mmoja wa marafiki wa Christina anaingia katika duka lile, anaangaza angaza lakini ghafla anamuona Raymond akiwa na Angelina)

Rafiki wa Christina: jamani huyo si shemeji? (anamuangalia vizuri) ni yeye…anaonekana yupo kwenye mahaba mazito na huyu binti…mwenzangu ngoja nimuulize shoga yangu huyu…(anaguna)na huu umbea utatuua jamani (anachukua simu na kumpigia Christina, simu inaita na mwisho inapokelewa) shoga mambo vipi?

Christina: poa…kwema?

Rafiki: kwema…shoga yangu nachoona sijui ni kweli au macho yangu?

Christina: kwanini unasema hivyo?

Rafiki: kwani wewe na shem…mmeachana?

Christina: hapana…kwani vipi?

Rafiki: namuona hapa yupo na demu mwingine nakwambia ni full maloveee

Christina: ananisaliti huyo mwanaume mshenzi (anajisemea moyoni) ni nafasi nzuri na ni muda wangu muafaka kumjua huyo Malaya aliyenipokonya danga langu (kwa rafiki yake) embu naomba uwapige picha unitumie whatsapp tafadhali naomba unisaidie

Rafiki: usijali love, nafanya hivyo sasa hivi (anawapiga picha na kumtumia Christina) shoga angalia whatsapp yako

Christina: poa (anakata simu na kuangalia anapigwa na butwaa na haamini anachokiona) what? housegirl? yaani housegirl ndo kanipiku mimi?

Rafiki :( anampigia tena) umemjua huyu dada…

Christina: hapana simjui

Rafiki: njoo shoga yangu…uliamshe

Christina: haina haja (anakata simu) Raymond… (Anajikuta anapiga kelele) mshenzi wewe…nakuchukia (anajikuta anatokwa machozi) yaani hausigeli ndo kanipiku Mimi… nilivyo mzuri hivi (Analia Sana)

(Upande wa kina Raymond wanamaliza kuchagua nguo na viatu, analipa kisha wanatoka na kuondoka zao)

Raymond: twende tukanunue simu nataka simu zetu zifanane...Nataka tuwe na iphone 12

Angelina: ndo ipoje? Hii inanitosha bwana

Raymond: twende bwana (wanapanda gari na kwenda zao)

Rafiki yake Christina: yaani wanaume yaani kasahau kabisa kuwa ana mchumba jamani nyie hawa wanaume (anatema mate kisha anaendelea kuangalia nguo)

Post a Comment

0 Comments