IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 25

 


SCENE 25: -

(Christina anafika nyumbani Kwa Raymond akiwa amefura kwa hasira)

Christina :( baada ya kufunguliwa geti anashuka kutoka kwenye gari lake na kumfuata mlinzi getini) Raymond yuko wapi?

Ramadhani: salamu kwanza bwana…

Christina: unataka kuila au? Au umesikia ndo itakutoa kwenye umaskini? (Anabenjua midomo) okay…habari yako?

Ramadhani: Raymond yupo bustanini huko amepumzika…kwani vipi?

Christina: hayakuhusu (anaondoka na kuelekea bustanini alipo Raymond baada ya hatua chache sana anafika alipo Raymond) Raymond

Raymond :( anageuka maana alikuwa amegeukia upande mwingine) naam…

Christina :( anakaa kiti pembeni ya Raymond) habari yako…

Rayymond: salama…shikamoo

Chrristina: marahaba…za hapa

Raymond: salama…tu...Tupo (anampigia Angelina simu) njoo na (kwa Christina) unatumia kinywaji gani?

Christina: maji Tu...

Raymond: njoo na maji kuna mgeni

Angelina: sawa

Christina: siku hizi Mimi ni mgeni?

Raymond: usichukulie hivyo…Christina…basi nisamehe Kwa kukuita mgeni

Christina :( anaguna huku anabenjua midomo) sawa bwana kwahiyo hausigeli kanishinda?

Raymond: umejuaje?

Christina: huu mji mdogo Sana unaweza ukasema unajificha ila watu wanakuona

Raymond: siwezi kukataa Christina …Kama tayari umeshajua…basi ni kweli kabisa nipo kwenye mahusiano na msichana wangu wa ndani, sasa sitamuita msichana wangu wa kazi ni mpenzi wangu

Christina :( anapandwa na hasira ila anajikaza zisionekane)

Raymond: Na ninampenda Sana kwakweli…nampenda na ninataka awe mke wangu…

Angelina :( analeta maji na kumpa Christina)

Christina :( anayapokea ila kwa makusudi kabisa anaiachia glasi)

Angelina: samahani Sana…

Christina: adabu mbaya (Kwa ukali) unashika maji Kama sijui unashika nini wewe mwehu nini?

Angelina :( anajisikia vibaya)

Raymond :( Kwa Angelina) it is okay baby…nenda ndani kalete mengine haina shida

Angelina :( anaondoka na baada ya muda kidogo analeta maji)

Christina :( anayapokea Kwa hasira na kuyaweka mezani)

Raymond :( Kwa Angelina) nenda kaendelee na kazi zako baby

Christina :( anatamani mpaka kulia)

Angelina :( anaondoka zake)

Christina: why Raymond...?

Raymond: why nini?

Christina: umeniacha na kuwa na msichana wa kazi?

Raymond; mapenzi Christina…mapenzi

Christina: hiyo sio vizuri jamani

Raymond: naomba unisamehe…ila tangu nimekukuta na Peter moyo wangu ulikataa kabisa kukusamehe na nilijilazimisha kuwa na wewe tu kwa sababu baba anataka niwe na wewe…lakini siku nimemuona Angelina nafsi yangu ilikiri wazi kuwa nampenda sana na siwezi kumuacha milele nay eye ndo kipenzi changu haijalishi yeye ni nani na anatoka katika familia gani nachojua tu kwamba nampenda sana na nitafanya kila kitu awe mke wangu...She completes me and she is the woman of my life

Christina :( anajikuta anapiga magoti mbele ya Raymond)

Raymond: hapana Christina usifanye hivyo… (Anamnyanyua)no don’t do that please

Christina: umenivisha Pete ya uchumba juzijuzi tu…kila mtu yupo tayari Kwa ajili ya harusi yetu

Raymond: wataambiwa wataelewa tu

Christina: nini kitatokea Kwa wazazi wangu hiyo aibu tutaificha wapi?

Raymond: nisamehe Christina naomba unisamehe Sana

Christina: Raymond marafiki zangu wameshashona sare tayari kabisa Kwa ajili ya harusi…

Raymond: siwezi kuriski furaha yangu ili uwafurahishe marafiki zako...please understand

Christina; naomba unioe utanipa talaka huko mbeleni

Raymond: dini hairuhusu hata kidogo…we nyanyuka tu Na ukae upate maji yako…naomba tuwe marafiki…

Christina: Raymond

Raymond: wewe nyanyuka tu…

Christina :( ananyanyuka na kukaa kwenye kiti) Raymond, amekupa nini huyu binti?

Raymond: hata mimi sijui (anatabasamu kidogo) ila alichonipa namuomba aongeze yaani kama ni dozi naomba iwe hata mara saba maana najisikia vizuri sana kuwa in love nae…

Christina: iam not joking...Iam being serious Raymond

Raymond: hata Mimi sitanii…nipo very serious au unaona nacheka?

Christina: what happened to us? Tulikuwa tunapendana Sana

Raymond: tusiyazungumzie hayo tena maana umeniuliza Hilo swali atleast mara arobaini na nimechoka kukujibu ila kama unataka nikujibu basi ni kwamba ulikuwa unanisaliti mara nyingi sana katika mahusiano yetu sio mara moja na mara nyingine ulionyesha wazi kuwa unataka pesa zetu…sasa wewe sio mwanamke nayemtaka

Christina: nakuahidi kuwa nitakuwa ni mwanamke unaemtaka Raymond

Raymond:umechelewa sana…na sikupanga kwamba eti hausigeli atakaekuja nitafanya awe mpenzi wangu…huyu dada ana undugu na mpenzi wa Edmond…can you imagine nilivyokuwa naogopa kumwambia hata Edmond kuwa nimempenda sana shemeji yake…hata Edmond alidhani nimempenda au nilipanga kwamba akiniletea msichana nitamtongoza na kumfanya awe hawara jibu ni hapana sikupanga na wala sikutaka kabisa awe mpenzi wangu ila moyo uliipinga akili…na akili ikakiri kwamba moyo umeshinda na nipo tayari hata kusimama mbele ya baba yangu na kumwambia kuwa nina mwanamke nampenda sana na huyo mwanamke ni hausigeli wangu

Christina :( anadondosha machozi)

Raymond: hata akinifukuza kwenye hii nyumba ni sawa nitaenda popote na Angelina as long as nipo na Angelina basi hakuna nitakachoogopa…

Christina: unadhani baba yako atakubali?

Raymond: I don’t care…nampenda Angelina na hata mama yangu anajua Hilo tangu mara ya kwanza naanza kuhisi kumpenda sana Angelina nilimwambia mama na mama akanipa ushauri na support yake

Christina :( ananyanyuka na kuondoka zake huku Analia) sitaki kukusikiliza tena Raymond… (Anapanda gari lake kisha analiondoa kwa hasira)

Raymond: sikutaka kumuumiza mtu yeyote…nataka kuwa na Amani tu…jamani hata iweje siwezi kumuacha Angelina...Nampenda sana (anaingia ndani na kumkuta Angelina anaosha vyombo anamkumbatia kwa nguvu) mke wangu

Angelina: nimemuona Christina Analia kila kitu kipo sawa?

Raymond: ndio (anambusu shavuni) usipike jioni twende tukale nje…

Angelina: we nidekeze tu... (Anacheka kisha anaendelea na kazi yake)

Raymond :( anacheka kisha anaingia chumbani kwake)

Angelina :( anatabasamu) Asante Sana Mungu wangu mwema…naliinua jina lako mfalme…wewe unasatahili sifa zote (anatabasamu kisha anaanza kuimba pambio ili kumtukuza Mungu wake) nina amani na huyu mwanaume…nampenda sana Raymond

Post a Comment

0 Comments