IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 26

 


SCENE 26: -

BAADA YA MWEZI MMOJA: -

(Angelina amekaa bustanini peke yake anakunywa kinywaji chake cha baridi huku anaongea na kipenzi chake kwenye simu. Wakati anaendelea kuongea Christina anafika mahali pale na kusimama kama sanamu kabla hajamuita)

Christina :( anamuita kwa utaratibu kama vile mtu ambae ana urafiki nae au anataka urafiki nae) Angelina…

Angelina :( anamalizia kuongea na simu) kata nitakupigia baadae kidogo

Raymond: kuna shida gani?

Angelina: hamna shida kuna mtu tu anagonga geti

Raymond: si umwambie Ramadhani ndo afungue geti? Umekuwa mfungua geti?

Angelina: kaenda kuoga…Bwana kata simu mara moja

Raymond: sitaki mpaka uniambie kuwa unanipenda…

Angelina: haya nakupenda (anatabasamu)

Raymond: nakupenda pia (anatabasamu kisha anakata simu)

Angelina: abeee…dada Christina karibu…

Christina :( anatembea hatua chache na hatimaye anamfikia Angelina)

Angelina :( muda wote huo anamuangalia Kwa wasiwasi)

Christina :( anapomfikia anakaa pembeni ya Angelina) vipi za siku nyingi?

Angelina :( bado ana wasiwasi) nzuri shikamoo dada Christina…

Christina: marahaba… (Anamuangalia Sana usoni kisha anatabasamu) kumbe pesa nzuri sana

Angelina: kwanini?

Christina: umekuwa Mrembo Sana…Raymond anajitahidi Sana kukutunza…yaani hatujaonana mwezi tu lakini umebadilika Sana

Angelina :( anacheka lakini bado ana wasiwasi) dada bwana...Mbona huji siku hizi?

Christina :( anajichekesha) we kwani hujui kuwa sina cha kunileta siku hizi au hujaambiwa na bwana wako?

Angelina: aliniambia tu kuwa mmeachana…

Christina :( anacheka kidogo) yes…tumeachana baada ya kukaa katika mahusiano Kwa muda Mrefu Sana na tulikuwa tumebakiza miezi kadhaa tufunge ndoa ila sijui akaonaje anaona ni bora tu tuachane

Angelina: dah…Mungu ni mwema atakusaidia na wewe utapata mtu mwingine…

Christina: hata Mimi naamini kuwa ipo siku na mimi nitapata mwanaume atakayenipenda na kunithamini

Angelina: kweli kabisa… (Anaguna kidogo) yaani nimekaa hap ahata sijakuuliza unatumia nini?

Christina: maji tu…

Angelina :( ananyanyuka na kwenda ndani kuleta maji)

Christina :( anajisemea moyoni) Kwa akili yako kabisa unaona Mimi nipo hapa kukupa hongera ya kuniibia Raymond au kuunda urafiki na wewe? Umechemsha my dear

Angelina :( anarudi akiwa ameshika glasi ya maji) karibu maji

Christina :( anapokea) Asante (anamuangaliia kisha anatabasamu)

Angelina :( anarudi kukaa alipokuwa amekaa)

Christina :( anakunywa maji kidogo kisha anarudisha glasi kwenye meza ndogo iliyopo mbele Yao) unampenda Sana Raymond?

Angelina: nampenda kweli ni mwanaume anayenipa Amani sana moyoni mwangu…

Christina: na yeye je?

Angelina: ananipenda…mi ndo naona hivyo na ananionyesha pia

Christina: Na huwa mnaambiana kila kitu?

Angelina: ndio…ananiambia

Christina: oh…kumbe unajua kuwa ana mwanamke mwingine anamhudumia kwasababu amezaa nae?

Angelina :( anashtuka Sana) ana mtoto na ana mwanamke? Raymond huyuhuyu?

Christina: ndio...mi nikajua kakwambia Mimi nimekuambia tu kirafiki maana kwanza sina uadui na wewe mama nataka urafiki na wewe na nimeongea na wewe kama vile kimbea tu kama marafiki wanavyoongea

 Angelina:(anashikwa na hasira sana) yaani Raymond ananidanganya mimi…ananiambia hajawahi hata siku moja kumpa mimba mwanamke na kama nitabeba mimba mimi ndo nitakuwa wa kwanza

Christina: ndo hivyo shoga yangu wanaume ni waongo sana wana maneno mazuri ili wapate wanachotaka na wakipata ndo utaona ubaya wao…shoga yangu wanaume ni mbwa hawa jamani

Angelina: hanikuti hapa…ananidanganya Mimi Kama mtoto…

Christina: bora tuujiondokee tu shoga yangu maana mwanaume Kama huyo anakudanganya hivyo siku nyingine anaweza kukudanganya mambo makubwa hata yahusuyo afya yake

Angelina: kweli dada…. hawa wanaume ni wabaya ndo maana mimi sikutaka kabisa kuwa na mwanaume yeyote, sitaki anikute hapa ameniudhi sana

Christina: wewe usiondoke…bwana mwenzio ikijulikana kwamba Mimi ndo nimekuambia atanichukia Sana

Angelina: wewe usijali…sitakutaja ila mimi naondoka hapa sitaki kabisa mahusiano nae…namchukia sana Raymond ameniudhi kumbe nay eye ni muongo ee (anaingia ndani)

Christina :( anacheka Sana) simple tu wala sijahitaji nguvu nyingi za ziada nimekuja nimejifanya rafiki nikasema uongo basi huyoooo anaondoka zake…sasa next plan… (Anatabasamu) lazima niwagombanishe Zaidi na Zaidi

Angelina :( anatoka amebeba begi lake)

Christina :( anamuendea na kujaribu kumzuia) ila mi naona kuwa ungemsubiri tu umuulize anaweza akakuambia ukweli au hata akakanusha uvumi huu

Angelina: sina huo muda wa kumsikiliza…amenidanganya mara moja anaweza kufanya hivyo Mara nyingi atakavyo

Christina: kweli lakini (kimya kidogo Kama anawaza kitu) sasa hapa wewe unaenda wapi?

Angelina :( anafuta machozi maana alikuwa Analia muda wote tangu amepewa taarifa hizo) popote dada… (Anaondoka)

Christina:(anacheka kwa dharau huku anatikisa kichwa)maskini pole yake sana…hana akili hata kidogo(haraka anaingia chumbani kwa Raymond kwa kuwa mlango ule haufungwi inakuwa rahisi kwake kuingia na kufanya chochote)hapa ni kuanza kuchezesha akili tu ili wachukiane milele…(anafika chumbani anafungua bei dogo ambalo Raymond anaweka pesa,anachukua kiasi kingi cha pesa na kuliacha begi hapohapo kitandani)sasa akija Raymond hapa itakuwa virahisi kwake yeye kujua aliyeiba pesa ni Angelina na akakimbia kuogopa msala (anacheka sana)nimeua ndege wawili kwa jiwe moja…najipenda sana…najipenda mimi na akili zangu(anatoka na kuelekea kwa Ramadhani)

Ramadhani :( Kwa furaha) ah shemela…nilikumisi

Christina :( anamfikia) acha unafki wewe…unanimisi au ndo ulifurahi Mimi kuachika na huyo Malaya ambae hana hata akili vizuri kachukua nafasi yangu

Ramadhani: shemeji sio kweli kwamba nilifurahi…

Christina: anyway, sina muda wa kupoteza hapa…kuna jambo nataka unisaidie kama ikiwezekana

Ramadhani: itawezekana tu we nambie

Christina: huyo mshenzi nimemdanganya danganya kuhusu Raymond akaondoka mwenyewe…sasa nataka Raymond akija umwambie kuwa Angelina amekimbia Na ameiba pesa nyingi Sana

Ramadhani: sawa shemela usijali

Christina :( anatoa pesa taslimu Kama laki tano) shika na unifanyie hii kazi vizuri bila kubabaisha

Ramadhani :( anapokea Kwa mikono miwili) Asante Sana shemeji na  ndo maana mimi nilikuwa nakupenda wewe huyo maringo mengi na madeko

Christina: mi naondoka bwana sitaki Raymond anikute hapa

Ramadhani: haya tutaonana na asante kwa hela ya soda

Christina: poa… (Anapanda gari lake kisha anaondoka)

Ramadhani: mi nakula tu pesa…nitafanyaje sasa…kumpenda nampenda Angelina na naona wanaendana kweli na boss ila nifanyeje…sasa nataka hela (anacheka kidogo kisha anaingia ndani kwake)

Post a Comment

0 Comments