IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 27

 


SCENE 27: -

(majira ya saa kumi na mbili jioni Raymond anarudi nyumbani akiwa anaonekana kuwa amechoka sana na kazi na mizunguko ya siku ile, mara baada ya kuegesha gari lake anaingia ndani ili aungane na kipenzi chake. anaanza kuitia nje ili apate kupokelewa kama ilivyo kawaida yao)

Raymond: baby….

(Kimya)

Raymond: malaika… (Anaingia ndani)

(Kimya)

Raymond :( anashangaa) my love…

(Kimya)

Raymond :( anacheka kidogo) najua unajificha…na sijui kwanini unajificha…anyway nimekuzoea basi acha utani my love mi mwenzio nilikuwa na kazi nyingi sana njoo unipoze mwili na moyo wangu (anacheka kidogo)

(Kimya)

Raymond :( huku anakaa) Angelina…

(Kimya)

Raymond:(ananyanyuka na kwenda chumbani kwa Angelina) baby…(hamkuti)ameenda wapi? (anaenda na chumbani kwake) Angelina…. (anakuta droo anayowekea pesa imefunguliwa) nani kafungua droo yangu (anaangalia kitandani) mbona box langu lipo kitandani (anafungua ndani anagundua kuwa pesa zimepungua) kuna mtu amechukuwa pesa zangu…Mungu wangu isije ikawa mke wangu ametekwa na majambazi wamechukua pesa… (anatoka nje haraka) Ramadhani…

Ramadhani: naam boss…

Raymond: Angelina yuko wapi?

Ramadhani: katoroka…kabeba mizigo yake akaondoka

Raymond: haiwezekani…Angelina hawezi kunifanyia Mimi hivyo

Ramdhani: boss unamuamini Sana…unasahau kuwa na yeye ni mwanadamu

Raymond: sijasahau na wala sio kwamba sijui kuwa Angelina ni mwanadamu na anaweza akafanya dhambi ila sidhani tu kama anaweza kutoroka na kuniibia pesa zangu

Ramadhani: makubwa…kaiba pesa?

Raymond :( hajibu kitu na badala yake anachukua simu yake na kumpigia Angelina) pokea simu malaika…wangu

Ramadhani: hawezi kupokea simu maana anajua amefanya dhambi…mtoto mbaya huyu…kwanini lakini unawaza Sana si umuache aende?

Raymond: Ni kwamba hujui kuwa Angelina ni mwanamke nimpendae kwa dhati au unataka kunisumbua akili yangu?

Ramadhani: duh…pole Sana boss jamani…nakuonea huruma Mimi mpaka natamani kulia

Raymond :( anampigia simu Edmond simu inaita Kwa muda na mwisho inapokelewa) brother

Edmond: wewe umemfanya nini Angelina? Nilitaka nikupigie… yaani wewe umemfanya nini huyu mtoto?

Raymond: sijafanya chochote kibaya…. kwani vipi?

Edmond: Mimi ni kama kaka yako lakini hata siku moja hukuwahi kuniambia kuwa una mwanamke umezaa nae na unamhudumia

Raymond :( anashangaa Sana) what are you talking about?

Edmond: Angelina yupo Kwa Catherine Analia na aachi kulia anataka kurudi kwao…anasema umemdanganya na hataki kukuona tena milele

Raymond: embu nakuja… (Anakata simu na haraka anapanda gari na kuondoka) my God…

(Anaendesha Kwa muda na baada ya kama dakika kumi na tano anafika nyumbani kwa Catherine, bila kupoteza muda anaingia ndani)

Catherine: karibu shemeji yangu…

Raymond: habari shemeji…

Catherine: Safi

Edmond :( anakuja akitokea chumbani) hey…Mond

Raymond: yes Mond...Nambie…Angelina yuko wapi?

Catherine: yupo chumbani

Raymond :( anawaacha hapo na kukimbia chumbani, anamkuta Angelina amekaa kinyonge sana huku macho yake yanaonekana kuvimba sana) baby…

Angelina: usinishike tafadhali …siamini Kama unaweza kuwa ulikuwa unanidanganya muda wote huu…

Raymond: hapana Angelina sijawahi kukudanganya kwa chochote nilipokuambia kuwa nakupenda nilimaanisha kuwa nakupenda Angelina…niliposema kuwa nataka kukuoa nilimaanisha kweli nataka kukuoa amini tu mpenzi wangu

Angelina: Na huyo kipenzi chako unayemhudumia…. mwenye mtoto wako…

Raymond :( anashusha pumzi) sina mwanamke wala mtoto nje Angelina…sina mwanamke ninayemhudumia ningekuwa nae basi ningekuambia mpenzi wangu tafadhali niamini…naomba Angelina usiniache ukiniacha haki ya Mungu tena nitajiua nakupenda Sana mpenzi wangu tafadhali naomba turudi nyumbani kwetu na tuendelee na maisha yetu kama kawaida

Angelina :( ananyanyuka) hapana…Mimi sikutaki tena…Raymond Mimi na wewe mapenzi basi…najuta hata nini kilinifanya nikukubali umeniumiza sana

Raymond :( anakuwa mnyonge sana) Angelina…

Angelina: nataka niondoke na kwenda nyumbani Raymond…sitaki tena nipe mshahara wangu niende kwa mama na wadogo zangu nilitumwa kuja kufanya kazi na sio kuendekeza mapenzi… (anaanza kulia) hii ni laana mama yangu alinituma nije nifanye kazi mimi nimekuja kuendekeza mapenzi…(Analia)nimejuta

Raymond :( machozi yanamtoka) sio hivyo Angelina wangu…na sijui ni nani amekuambia uongo huo…na nia yake ni kututenganisha tusimpe nafasi…Angelina tafadhali naomba unisikilize…

(Edmond na Catherine wanakuja chumbani hapo)

Catherine: Angella kaa utulie mdogo wangu nakuomba ukae chini kwanza tuongee huku umetulia

Angelina :( anatii na kukaa chini)

Edmond: shemeji…hiyo habari uliyoambiwa ni ya uongo…Raymond hana mtoto wala mke nje na kama angekuwa nae mimi ningejua mimi nay eye hatufichani…

Angelina :( anaanza kutulia)

Edmond: huyo aliyekuambia ni muongo sana na ni muuaji anataka kuua penzi lenu na Raymond anaona kabisa nyie mnapendana sana na anafanya kila kitu ili awagombanishe msimpe nafasi hiyo…Raymond anakupenda na atabaki anakupenda hivyo milele…muamini na acha kusikiliza maneno ya watu nje…umesikia shemeji yangu wa pande zote mbili?

Angelina :( anaonekana ameanza kuelewa)

Raymond :( anashusha pumzi na anaachia tabasamu tulivu)

Angelina: sawa nimeelewa…lakini Raymond anatakiwa kuniambia ukweli Kama kweli ana mtoto nje au lah

Raymond: sina Mimi mtoto…na ninajua kuwa ni Christina ndo amekuambia kuwa nina mtoto nje

Angelina: ndio...ILA umejuaje kuwa ni yeye?

Raymond: najua tu maana hata yeye alikuwa anahisi kuwa Nina mwanamke nje na mpaka akamwambia baba yangu na walimsumbua sana (kwa Edmond) si unakumbuka

Edmond: nakumbuka duh kumbe kwasababu ya ile (anacheka kidogo) …ilikuwa gumzo…

Raymond :( anamgeukia Angelina) nakupenda Sana kipenzi changu na ninakuahidi sitakusaliti kwa vyovyote vile…

Angelina: Asante…mpenzi wangu

Edmond: ooooh… (Anapiga makofi)

Catherine :( analeta begi la Angelina) rudi na mpenzi wako nyumbani kwenu mkayajenge na mpange siku ya ndoa tumechoka kusubiri…

(Wote wanacheka kisha Angelina na Raymond wananyanyuka na kuondoka zao)

Catherine: mapenzi bwana Angelina amekuja hapa analalamika ona alivyoondoka (anacheka)

Edmond :( anacheka pia) kwakweli mapenzi Yana nguvu Sana (anacheka Sana)

 

Post a Comment

0 Comments