IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 28

 


SCENE 28: -

(Siku ya tatu mara baada ya sakata la Angelina kukimbia nyumbani Kwa boss wake wa zamani na sasa mpenzi wake, mchana wakati wa mapumziko ya chakula cha mchana Raymond anaona aende kumtembelea Christina, anapanda gari lake na ndani ya dakika ishirini anafika Nyumbani kwa kina Christina)

Raymond: hodi… (Anagonga mlango)

Shangazi :( anafungua mlango) karibu Sana baba yangu

Raymond: Asante, shangazi shikamoo

Shangazi: marahaba baba hujambo

Raymond: sijambo…Christina yupo…?

Shangazi: yupo, nadhani atakuwa chumbani kwake

Raymond :( anaingia ndani anakaa sebuleni) naomba uniitie nahitaji kuongea nae

Shangazi: jamani baba…si mkeo mtarajiwa huyo ingia tu utamkuta

Raymond: hapana naomba nizungumze nae hapahapa

Shangazi: ah baba kwani kuna tatizo?

Raymond: hakuna tatizo…kila kitu kipo sawa

Shangazi :( anaingia chumbani kwa Christina na kumuita) shoga yangu Raymond amekuja anakuita kanuna huyo umemfanya nini?

Christina: ana stress zake tu hana lolote…anikome Mimi

Shangazi: (anacheka kidogo) anakuita

Christina :( anatoka na kumwendea Raymond alipokaa) Raymond…

Raymond: shikamoo,

Christina: marahaba karibu…

Raymond: Asante…

(Kimya kidogo)

Christina :( anavunja ukimya kwa kumuita msichana wao wa kazi) dada…embu mletee mgeni juisi (kwa Raymond) si utakunywa juisi?

Raymond: ofcourse nitakunywa Asante

Msichana :( analeta juisi na kumpa Raymond) shikamoo...Shemeji

Raymond :( anapokea) Asante, marahaba…

Msichana :( anaondoka zake)

Christina :( Kwa Raymond) niambie

Raymond: Christina, mara ya mwisho Mimi na wewe tunaachana naamini kabisa tuliachana kiroho safi na tukakubaliana tutakuwa marafiki si ndio?

Christina: ofcourse ulisema tuwe marafiki…na tumekuwa marafiki kwa kipindi hicho chote, any problem?

Raymond :( kimya kidogo huku anamuangalia usoni) yes…kuna tatizo

Christina: tatizo gani?

Raymond: unataka kuniambia hujui? i mean comeon Tina yaani wewe unafanya kitu halafu unasahau?

Christina: ndo uniambie sijui

Raymond: nilijua kuwa umekubali kuwa rafiki yangu utatunza furaha na Amani yangu (anakunywa juisi kidogo)

Christina: unaongea kimafumbo Raymond sikuelewi kabisa…

Raymond: naongelea kitendo ulichofanya juzi Christina

Christina: nilifanya nini Raymond? naomba usinilaumu kila mara unapopata majanga Raymond

Raymond: niliona kwenye CCTV juzi ulivyokuja na ulipochukua pesa zangu

Christina :( anainama Kwa aibu)

Raymond: hicho hakikuniuma kitu ulichoniudhi ni kumwambia uongo mwanamke wangu eti nina mtoto na kuna mwanamke ninayemhudumia…namhudumia nani mimi? Yaani…ukahakikisha mpenzi wangu ameondoka nyumbani kwangu yaani dah (anasikitika kidogo) isingekuwa Catherine na Edmond sijui ningempata wapi mke wangu

Christina: eti mkeo, umesahau au unataka kujifanya umesahau kuwa umenichumbia na mahari umenitolea na hapa kila mtu anajua wewe ni mume wangu mtarajiwa, nina haki ya kufanya kila kitu nilichofanya

Raymond: huna haki yeyote Christina Mimi ni mwanadamu na mwananchi mwenye uhuru wa kufanya chochote nachotaka, nimempenda Angelina na ni yeye ndo nitamuoa

Christina :( anaguna) kwahiyo wazazi wako wanajua?

Raymond: hawajui ila watajua siku si nyingi haitakuwa kazi kuwaambia

Christin: nyie wanaume kwanini mpo hivyo? Umenipa matumaini miaka yote huu halafu mwisho wa siku unaniacha solemba

Raymond: acha lawama ili mimi ndo nionekane nina makosa ili makosa yako niyasahau…umefanya kosa kuniingilia na huku tulikubaliana kuachana

Christina: uliniambia kuwa unaniacha ila mimi sikuwa tayari kwahiyo hatukukubaliana wala nini ni wewe ndo uliamua

Raymond: it’s about my heart and what I want…nimempenda Angelina it just happened, sikupanga eti msichana aje na mimi nimpende na kumfanya awe mpenzi wangu…mimi na wewe tuliachana kabla hata uchumba wetu haujatangazwa

Christina :( anacheka) kwanini hukukataa mapema?

Raymond: Kwa wakati huo sikuwa na nguvu maana I was not in love…now iam madly in love with my housegirl na hakuna atakae weza kunitoa kwenye dimbwi hilo sio wewe wala baba yangu…sikuoi and that is final

Christina: Raymond hiyo sio haki

Raymond: huruhusiwi hata kidogo kuniingilia katika mahusiano yangu na mpenzi wangu…nakuonya na naomba unielewe

Christina: Raymond

Raymond :( ananyanyuka na kuondoka zake)

Christina: Raymond bado hatujamaliza kuongea

Raymond :( anaondoka zake)

Christina :( anakasirika Sana)

Shangazi :( anakuja) nini shoga yangu

Christina: anadhani ataniacha kizembezembe? Amechemsha mshenzi huyu yaani anipotezee muda halafu aje aniache eti iam in love with my housegirl…Raymond…unataka kuninyang’anya tonge mdomoni…sitakuruhusu, akitaka kuniacha labda aniue lakini hivihivi…asahau

Shangazi: kumbe kijana mjinga huyu ee

Christina: amekuja kunionya nisirudie kumgombanisha na mpenzi wake

Shangazi :( anaguna) amependa

Christina: ni kwamba sitaruhusu kabisa yeye na huyo mwanamke wawe na mapenzi ya Amani yaani nitawasumbua mpaka wachanganyikiwe, mimi ndo mke mtarajiwa wa Raymond...Hakuna kinyago yoyote atakayeruhusiwa kuwa na mahusiano na Raymond…

Shangazi: ila shoga yangu una dhambi unampenda mwanamume mwingine lakini unamtaka Raymond unajua hata sikuelewi

Christina: nampenda Peter Sana ila namtaka Raymond maana yeye ni atm wangu na nitahakikisha kuwa ATM inabaki kwangu na hakuna mtu mwingine anaimiliki

Shangazi: halafu unajua Raymond analijua Hilo

Christina: atakoma mwenyewe…mi nachoangalia ni pesa

Shangazi: chagua moja…Peter au Raymond

Christina: wote maana Nina shida nao wote (anacheka kwa kejeli)

Shangazi: mtoto mbaya wewe

Christina: lazima nijue namfanyaje raymond kabla haijawa too late

Shangazi: pambana mimi nipo ndani (anaingia chumbani)

Post a Comment

0 Comments