IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 29

 


SCENE 29: -

(jioni njema na Ya kuvutia kuna hali Fulani ya utulivu unaendelea, jua kwa mbali linaanza kuzama, kila kitu kinaonekana katika utulivu, watu wanatoka katika mahangaiko yao ya kila siku, Raymond na Angelina wamekaa bustanini, wanafurahia faragha yao)

Raymond :( anamshika Angelina mashavu) yaani siamini Kama tupo wote Mimi na wewe mpenzi wangu maana dah…acha tu

Angelina :( anacheka kidogo) usijali mpenzi Mimi na wewe milele penzi letu litadumu milele

Raymond :( anamuangalia kisha anatabasamu) sijui ulikuwa wapi miaka yote kwanini hukutokea siku nyingi uuponye moyo wangu? Maana nilikuwa nateseka mwanamke niliyekuwa nae nae hakuwa mtu mzuri hakuwa na mapenzi na mimi

Angelina: nimekuja sasa na ninaahidi sitakuacha labda wewe uniache

Raymond: unasema kweli baby?

Angelina: nakwambia kweli

Raymond :( anamuangalia usoni) nakupenda Angelina wangu wewe ni mwanamke wa ndoto zangu

Angelina: Na wewe ni mwanaume wa maisha yangu nakupenda na ninakuheshimu sana Raymond….

Raymond: nataka nikawaone wazazi wako…ulisema una mama tu huna baba

Angelina: ndio

Raymond: nataka nikamuone mama yako mpenzi wangu

Angelina: nitafurahi Sana mpenzi wangu…

Raymond: hivi umeshawahi kumwambia kuwa una mahusiano na mimi?

Angelina: bado sijamwambia

Raymond: kwanini?

Angelina: Nitamwambia, ila tu naona Kama hatafurahi akisikia kuwa nimekuja mjini badala ya kufanya kazi mimi nimeamua kuwa na mwanaume

Raymond: lakini Mimi si mwanaume yeyote Angelina Mimi ni mwanaume ninayekupenda kwa dhati na lengo langu ni kufunga ndoa na wewe

Angelina: sijakataa na wala sibishi juu ya nia yako lakini acha kwanza tukae kidogo mama tutamwambia tu

Raymond: au una mtu wako nyumbani kwenu?

Angelina: hapana sina mtu wala nini nipo Mimi na wadogo zangu na mama yetu sina mwanaume

Raymond: sawa (kimya kidogo huku anamuangalia Kwa uchu kidogo)

Angelina: vipi? Mbona unaniangalia hivyo?

Raymond: kila siku huwa naombea kurudi nyumbani mapema ili nikuone huwa upo moyoni mwangu na akilini mwangu kila saa mpenzi wangu

Angelina :( anacheka Kwa aibu kidogo)

Raymond :( anamsogelea na kutaka kumbusu mdomoni)

Angelina :( anaogopa)

Raymond: usiogope Angelina…

Angelina: hapana unataka kufanya nini Raymond?

Raymond: nataka tu kukubusu na si vinginevyo

Angelina: lakini haya mambo tuliongea na kukubaliana kuwa hatutakuwa tunayafanya mpaka siku tutakapooana

Raymond: hata busu? Mimi nilikubali kuwa hatutafanya tendo la ndoa mpaka tuoane lakini sasa hata busu…sisi ni wapenzi Angelina sio kaka na dada

Angelina: kila kitu kisubiri Raymond…nilijiahidi kuwa mwanaume atakaekuwa wa kwanza ndo atakuwa mume wangu

Raymond: Mimi nitakuwa mumeo Angelina

Angelina: mpaka siku ifike ndo nitalala na wewe

Raymond: acha hizo baby Mimi nimekuahidi nitakuoa nakupenda Angel

Angelina: umeniahidi utanioa ndio ila sina uhakika juu ya maneno yako je kama unanidanganya?

Raymond: siwezi kukudanganya Angelina nimeshakuonyesha upendo na nia yangu kwako, nimeshakutambulisha kwa mama yangu huamini nini Angelina

Angelina: kunitambulisha kwa mama yako sio tija Raymond unaweza kunitambulisha na mwisho ukaniacha solemba…mfano Christina wewe si mpaka watu walikuja kushuhudia mnavalishana pete ya uchumba hapa? Lakini mbona Leo hii umemuacha?

Raymond: usijifananishe na Christina mapenzi yetu yalishaisha…

Angelina: ulimaliza mapenzi na mwanamke uliyempenda miaka mingi sana sembuse mimi uliyenijua juzi tu…, mimi kiukweli subiri kwanza ukinioa tutafanya tendo la ndoa mara nyingi unazotaka kwa sasa hapana

Raymond: hapana Mimi nataka busu tu

Angelina :( ananyanyuka Kwa jazba) au ndo maana unaniongelesha maneno mazuri kumbe lengo lako utembee na mimi kisha uniache kama Christina?

Raymond:(ananyanyuka na kujaribu kumshika) calm down baby…sio nataka kukuacha na wala sina hiyo nia mimi ni mwanaume nina mahitaji yangu ya kimwili lakini kama hauko tayari sijakulazimisha Angel unaweza tu ukaacha sio lazima na pia mimi mbona nilikubaliana na wewe

Angelina: hapana Raymond naogopa maumivu ya moyo Nina moyo mdogo sana siwezi kuvumilia siku ukiniacha tena baada ya kuniachezea usichana wangu na kuniacha

Raymond: si basi Kama umekataa?

(Huku getini Ramadhani anasikia majibizano Yao)

Ramadhani :( anacheka) enhe!!!!leo ndo leo wameanza kugombana wenyewe humu ndani(anacheka)sijui watakuwa wanabishana nini sijui Yanga na Simba au namba za nida zinatoka lini maana duh, inshu ya nida iko moto mpaka watu wanakaa kwa kupaniki (anacheka sana) embu ngoja nikawacheki (anaenda bustanini walipo Angelina na Raymond) leo pamenuka halafu (anaangalia vizuri) mwanamke nae mbabe

Raymond: Angelina ya nini marumbano mpenzi Kama haiwezekani hakuna anayekulazimisha Kwa lolote kufanya usilolitaka

Angelina: ndo maana unaniambia unanipenda kumbe unawaza mambo yako ya ajabu

Raymond:(anashangaa) ningekuwa wa hivyo Angelina kwa muda tuliokaa kama wapenzi ningetaka ningekubaka tu humo ndani na hakuna ambae angejua na usingenifanya lolote...nakupenda na ninakusikiliza unachotaka basi hakuna mjadala wa kuumiza kichwa

Angelina :( anazidi kuwa mbishi maana akili yake imeshaamini Raymond hampendi anataka kumchezea tu) hunipendi Raymond si useme tu wazi kuwa naomba tusaidiane maisha mimi kwa kuwa sasa hivi sina mpenzi naomba nitimize haja za mwili wangu kwako basi (Analia) lakini sio kukaa unanidanganya

Raymond: sipendi kuona machozi yako Angelina na isitoshe tumekaa hapa nje tukiwa na lengo la kupumzisha akili zetu na miili yetu baada ya kazi nyingi za siku hii lakini wewe unataka kunichanganya tu sijui lengo lako ni nini

Ramadhani: ngoja nikawaulize naona watu wanalia tu (anaenda) jamani za jioni

Raymond: salama vipi?

Angelina :( anafuta machozi) salama shikamoo

Ramadhani: marahaba, kuna tatizo?

Raymond: Ni kutoelewana tu kidogo baina yangu na mwenzangu…. hakuna tatizo

Ramadhani: basi poa, maana nimesikia sauti mpaka getini kule nikaona labda mambo yamekuwa mambo

Raymond: hapana

(Ramadhani anaondoka, huku Raymond anajaribu kumbembeleza mwenzie anayeonekana kukataa kabisa kumsikiliza)

Raymond: basi nisamehe, sitazungumzia tena mapenzi na tendo hilo tena nisamehe mpenzi wangu

Angelina :( anamuangalia kisha anakumbatia) sipendi kugombana na wewe Ray

Raymond :( anamkumbatia pia) nakupenda Angelina

Angelina: nakupenda Raymond

Raymond: wewe kumbe mkali ee (Anacheka)

Angelina: (anacheka)

Post a Comment

0 Comments