IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 30

 


SCENE 30: -

(Asubuhi majira ya saa tano, Angelina yupo njiani anaonekana kuwa ametoka sokoni kwani ana kikapu kilichojaa mbogamboga, akiwa njiani anakuwa anaongea Na simu)

Angelina :( anacheka) yaani hapa nilipo ndo natoka sokoni Leo nimechelewa Sana kutoka sokoni

Raymond: ulikuwa unafanya nini muda wote?

Angelina: Leo nilikuwa Nina mahemezi mengi Sana

Raymond: yaani wewe (ananyamaza kidogo)

Angelina: sasa mbona huongei?

Raymond: nakumbuka hasira zako Jana (anaguna) nilihisi utanishushia kipondo

Angelina: ah wapi siwezi kufanya hivyo sijalelewa hivyo

Raymond: vizuri Sana my dear

Angelina: Leo nitakupikia chakula ukipendacho…nimenunua nazi Kama ugomvi

Raymond :( anacheka Sana) eti Kama ugomvi…sasa unagombana na nani mimi nipo kazini labda ukagombane na Ramadhani

Angelina: nagombana na wewe

Raymond: Mimi utanionea maana sina hata hizo nguvu za kugombana Na mtu

Angelina :( anacheka) Kwahiyo unaniletea zawadi gani jioni

Raymond: midoli

Angelina: Akha!!Sasa Mimi midoli ya kazi gani jamani kwani Mimi mtoto?

Raymond: ndio wewe mtoto…. nakuitaga baby unaitika wewe unajua maana ya baby?

Angelina: nitajulia wapi sikusoma?

Raymond: umeanza sasa kujishusha unanikera Angel

Angelina: ndo ukweli huo

(Gari ndogo aina ya Mark II linakuja kuegesha pembeni yake)

Angelina: embu ngoja nifanye kazi za jamii

Raymond: nini tena?

Angelina: nahisi kuna watu wamepotea njia wanataka kuniuliza kitu

Raymond: poa we fanya kazi za jamii ila ukimaliza tu naomba unipigie tena napenda kushinda nasikia sauti yako

Angelina: (anacheka kidogo) sawa

Raymond: nakupenda Sana Angelina

Angelina: nakupenda pia

Raymond: bye

Angelina: bye (anakata simu kisha analisogelea gari lile)

(Kuna mtu anashusha kioo na Angelina anapoangalia vizuri anaona ni Christina)

Angelina: shikamoo dada Christina

Christina: marahaba…mbona unatembea Kwa miguu bwana’ako hajakununulia gari?

Angelina :( anacheka kidogo) bado

Christina: panda nikupe lifti mpaka kwako, maana ishakuwa nyumba yako

Shangazi :( nae yupo kwenye gari) hongera yake

Angelina :( huku anapanda kwenye gari) shikamoo mama

Shangazi: marahaba

(Christina analiondoa gari kwa kasi kubwa mahali pale)

Angelina :( hana Amani)

Christina :( anamuangalia kupitia kioo cha mbele) vipi Angelina mbona unaonekana huna Amani? Shida nini?

Angelina: hapana dada mbona Mimi Nina Amani tele

Shangazi: vizuri

Christina :( anaipita nyumba ya Raymond)

Angelina: dada Mimi nimefika

Shangazi: eti nimefika…kwako pale?

Angelina: kwani nini tatizo?

Shangazi: mwisho wa ubaya ubaya tu wewe umeiba mume wa mtu halafu unachukulia poa…tunakupeleka tunapotaka sisi

Angelina: (anajaribu kupiga kelele)

Shangazi :( anamuonyesha kisu) nitakutoa utumbo sasa hivi kimya…(anafyonza)

Christina :( anacheka Sana) muoga kweli halafu vya watu unakula tena bila uoga mshenzi mkubwa

Angelina: nisameheni

Shangazi: tumeshakusamehe lakini ni lazima tukuonyeshe kitu ili ukome usirudie tena mwehu wewe

Angelina: Kama ni Raymond mchukueni tu mimi roho yangu niachieni jamani mimi nategemewa na familia yangu

Christina: familia yako ilikutuma uje utafute riziki na sio kutafuta mabwana za watu mshenzi wewe

Angelina: tafadhali nisamehe Sana dada Christina

Shangazi: lazima ufundishwe adabu…

(Gari linaenda kwa mwendo wa kasi sana)

Angelina :( anapiga kelele) nawaomba Sana msinidhuru Mimi jamani nitaachana na Raymond, ni kweli nimefanya kosa kwa kuingilia mapenzi ya watu nisameheni

Christina: kila afanyae kosa ni lazima aadhibiwe hivyo basi ulifanya kosa lazima uadhibiwe

Angelina: nisamehe Nina mama na wadogo zangu ambao wananitegemea sitaki kufa

Shangazi :( anamzaba kofi moja kubwa la kutosha) kelele…ulitumwa ufanye umalaya?

Christina: embu niambie umelala nae mara ngapi?

Angelina :( huku Analia Sana) sijawahi kulala nae haki ya Mungu tena sijawahi haki ya Mungu siwadanganyi

Shangazi: muongo huyu…

(Wanafika katika jumba moja chakavu ila lina madirisha na milango na bati)

Shangazi: tumefika

(Christina anashuka kisha anamvutia Angelina nje na kumsukumia ndani ya jumba hilo chakavu)

Angelina :( Analia Sana na anakumbuka kuwa ameshika simu anajaribu kumpigia Raymond)

Shangazi: wewe jaribu uone (anamnyang’anya simu) pambana na hali yako Malaya wewe

Angelina :( Analia Sana)

Christina:(anacheka sana) kutesa kwa zamu, yaani mimi Raymond ananiaacha mimi eti (anamuiga Raymond) I am in love with my housegirl…. Loh!!!Yaani wewe takataka ni wa kunipokonya mimi tonge mdomoni na sasa sitakuacha hivihivi ni lazima nikuue

Angelina: hamna dada nisamehe…nimekosa (anapiga magoti) usiniue…

Christina :( anatoa kitu Kama mkanda kutoka kwenye mkoba wake na kuanza kumchapa Angelina mara nyingi sana)

Angelina: mama, nakufaaaa (Analia Kwa nguvu Sana)

Shangazi: kufa Malaya wewe

(Wanamchapa Kwa zamu mpaka Angelina anapoteza fahamu)

Christina: shenzi Sana… (Kwa shangazi) tufunge milango tuondoke tutarudi baadae

(Wanafunga milango na madirisha kisha wanaondoka wakimuacha Angelina bado amezirai)

 

 

Post a Comment

0 Comments