IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 4

 


SCENE 4: -

(Siku ya pili tangu Raymond akabidhiwe ofisi na utawala wa hospitali ya wazazi wake, amekaa ofisini kwake akiendelea na kazi zake za asubuhi. wakati huo huku nje Christina anafika ofisini hapo na anapofika anataka kila mtu ajue kuwa amefika hapo, maana anafanya vituko mbalimbali ikiwemo kuongea na simu kwa nguvu kama mwendawazimu)

Christina :( anapita kwa watu bila kuwasalimia)

Pendo :( ananong’ona) yaani huyu dada ...Yaani hana salamu hivi ni nani?

Rachel: nasikia ndo mchumba wa boss wetu

Pendo: loh!!! Mbona anaonekana mtata

Rachel: acha tu ndugu yangu embu tufanye kazi mengine hayatuhusu

Pendo: kwakweli shoga tufanye yetu (anacheka)

Christina :( anaenda mpaka ofisini kwa Raymond na bila kupiga hodi anaingia)

Raymond: (anashangaa kumuona) Christina...Vipi?

Christina: poa…habari za kazi (anakaa karibu kabisa na Raymond)

Raymond: nzuri…tu (hamuangalii)

Christina: (analazimisha Raymond amuangalie) Raymond…hiyo ndo tabia gani mkeo mtarajiwa anaingia na wewe huna muda hata wa kumuangalia

Raymond: Christina please...

Christina: (anamfokea) huna adabu Raymond

Raymond: sikiliza nikwambie kitu unaweza ukawa umenizidi umri lakini Mimi ni mwanaume na natakiwa kuheshimiwa tafadhali naomba heshima iwepo kwa kiasi kikubwa nisije nikajikuta nakukinai na kuacha kutimiza baba anayoyataka kwanza kwa uliyonitendea ilinipasa nikuache kabisa badala unitii wewe unaniletea ubabe

Christina: (anamuangalia usoni) mbona siku hizi una hasira Sana…simu zangu hupokei, yaani kila kitu kimebadilika Sana Raymond kwanini lakini?

Raymond: wewe umekuja Kwa heri au Shari niambie kabisa ili na mimi nijiandae

Christina: najua nilikusaliti Raymond lakini huna sababu ya kunichukia hivyo

Raymond :( ananyanyuka) sio usaliti tu Christina…mambo mengi Sana yananifanya nisitamani kuwa mumeo

Christina: nini Zaidi Raymond, au Kwa kuwa sijui kupika mpaka Leo hii Nina miaka 36?

Raymond: labda na hiyo ni sababu moja wapo ya kunifanya nisitake kukuoa lakini pia…

Christina :( anamkatisha) basi yaishe mume wangu mzuri jamani (anajichekesha) miaka sita tupo kwenye mahusiano leo ndo utake kuniacha baba tupo dakika za mwisho jamani tuoane unataka kuniacha Raymond wangu

Raymond :( anakaa kwenye sofa) by the way Christina Mimi na wewe tuna mazunguzo marefu

Christina :( ananyanyuka kwenye kiti na kwenda kukaa nae kwenye sofa) kuhusu nini mume wangu

Raymond: muafaka wa mahusiano haya tuliyonayo

Christina: yamefanya nini jamani?

Raymond: nataka tuachane Christina…nakuomba

Christina: kisa nini Raymond (machozi yanamlenga) Kama kuhusu usaliti si nishakuomba msamaha yaishe Raymond… (Machozi yanamtoka) nisamehe Raymond mpenzi...jamani si usahau baby hay ani mapito tu jamani kipenzi (anajaribu kumkumbatia)

Raymond; Christina please

Christina: haki ya Mungu tena Raymond nitajifunza kupika nitakuheshimu sitakaa kila saa naanzisha ugomvi na wewe, Raymond…nisamehe mwenzio

Raymond: hapana Christina hata mimi kukuacha sio kwamba napenda ila Christina hatuwezi kuwa pamoja tena Zaidi kama mke na mume, mawazo yetu hata ndoto zetu hazifanani

Christina: nakuahidi mume wangu (anapiga magoti mbele yake) nitabadilika usiniache Raymond…nakuomba baba…nisamehe (anakunja mikono Kama mtu anaeomba kanisani) usiniache Raymond, nakuomba baba

Raymond :( kimya kidogo huku anamuangalia usoni na anaonekana kama mtu anaetafakari jambo Fulani)

Christina: nisamehe baba yaishe, ndoa yetu imeshatangazwa

Raymond: nyanyuka…

Christina :( ananyanyuka)

Raymond: nakupa nafasi ya pili, naomba ujirekebishe

Christina: nitafanya hivyo Raymond

Raymond: futa machozi (anamtolea tishu) acha kulia

Christina :( anamkumbatia) nakupenda Raymond wangu tafadhali kamwe usije ukaniacha mume wngu wewe ni wangu milele na milele mpaka pale kifo kitakapotutenganisha

Raymond: ukiniahidi kuwa utaacha tabia yako ya uzinzi, maana kwa wanaume hujambo Christina na pia ukiniahidi kuwa utaniheshimu basi tutakuwa pamoja siku zote

Christina: mengine tuvumiliane tu

Raymond: jirekebishe

(Kimya kidogo huku Raymond anarudi kukaa kwenye kiti alichokuwa amekaa mwanzoni)

Christina :( anamkaribia) kwahiyo baby...Umenisamehee

Raymond: ndio embu naomba tujaribu tena huu uhusiano tuone unaenda wapi

Christina: sawa mpenzi nakuahidi kuwa sitakuangusha kamwe

Raymond: naomba iwe kweli na si vinginevyo naomba sana, kama haitakuwa hivyo itanilazimu kukuacha bila kukupa nafasi ya pili

Christina: sawa nimekuelewa mume wangu naahidi nitakuwa na wewe na nitakuwa msikivu pia usijali kwa hilo

Raymond: sawa haina shida…

Christina: twende shopping my love

Raymond: yaani wewe unaona kabisa ndo kwanza asubuhi na nina kazi nyingi sana hapa, halafu wewe unafikiria tu shopping embu jaribu kubadilika halafu hiyo tabia yako ya matumizi makubwa ya pesa jaribu kuibadilisha sio nzuri

Christina: Na wewe mtoto wa kisukuma unapenda kweli kukasirika sijui kwanini yaani utaniudhi bwana

Raymond: sio kukasirika nakwambia tu wala sijakasirika

Christina: poa kwakuwa una kazi nyingi ngoja nikuache

Raymond: poa baadae

Christina :( anasimama kisha anambusu mdomoni) baadae baby...

Raymond: poa…

Christina :( anaondoka zake)

Raymond :( anabaki anaendelea na kazi zake) huyu mwanamke huyu yaani sijui tu maana dah!!!sio kwa uvivu na kupenda pesa huko…eeh…(anafumba macho)Mungu nisaidie nipate mwanamke ninayemtaka kila siku nakuomba hicho hicho  maana mpaka sasa umenipa kila kitu kasoro mwanamke atakayenifaa atakayenisaidia kuzifikia ndoto zangu ,nataka mwanamke mwenye hofu yako Mungu wangu na si vinginevyo,nataka mwanamke asiye kunywa pombe,mwenye kujua kuujenga mji na si kujifikiria mwenyewe,Mungu nataka mwanamke asie mzinzi,nataka mwanamke mwenye mapenzi ya dhati na mimi na si mapenzi na pesa na mali za familia yangu,Mungu ulisema ombeni nanyi mtapewa bisheni nanyi mtafunguliwa,kama ulivyowafungulia Paulo na Sila gerezani naomba Mungu na mimi unifungulie hivyohivyo,nina kila kitu naomba mwanamke Mungu wangu…naomba mke Mungu wangu Christina sio mwanamke ninayemtaka nilisema tangu siku ile namfumania christina sio mwanamke kwanza haniheshimu saa nyingine ananitukana mbele za watu (anafumba macho kama mtu anayesikilizia maumivu Fulani) embu fikiria mimi Raymond natukanwa na mwanamke mbele za watu saa nyingine kwasababu nimemnyima pesa au sina pesa huyu ni mwanamke kweli Mungu wangu embu niangalie na mimi

Sekretari :( anagonga mlango)

Raymond: karibu…pita mlango uko wazi

Sekretari :( anaingia) habari za kazi boss

Raymond: salama kwema

Sekretari: nimeleta faili uliloniagiza

Raymond: Asante tafadhali kaendelee na kazi nikimaliza kuliangalia nitakuita

Sekretari: sawa boss (anaondoka zake)

Post a Comment

0 Comments