IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 31

 


SCENE 31:-

(Siku inaonekana kwenda ukingoni, jua kwa mbali linaanza kuzama na taratibu watu wanarudi makwao kupumzika mara baada ya mizunguko ya siku nzima, Raymond nae anajisogeza taratibu kurudi nyumbani kwake, akiwa njiani kuna maswali anajiuliza sana)

Raymond: Angelina tangu asubuhi ile nimetoka kuongea nae, sijamsikia kabisa sijui kuna nini, na hivi leo nilikuwa nina kazi nyingi sikupata kabisa nafasi ya kuja kupata chakula cha mchana na mpenzi wangu, au atakuwa bado amekasirika kuhusu ile juzi? anyways ngoja nifike nyumbani nitamuuliza vizuri, hatuwezi kushindwana nae (anaendesha gari lake na baada ya hatua chache anafika nyumbani, anapiga honi kuomba kufunguliwa geti)

(Hakuna anayetokeza)

Raymond :( anajaribu Kwa mara nyingine)

(Hakuna majibu)

Raymond :( wivu unaanza kumpanda) isiwe kuwa wapo ndani pamoja wanafanya Yao…haki ya Mungu nitamuua Ramadhani (anashuka na kwenda kufungua geti mwenyewe)

Ramadhani :( anatokea akiwa amevaa bukta Na vesti)

Raymond :( anajikuta anapandwa hasira) wewe Ramadhani ulikuwa wapi muda wote?

Ramadhani: nilikuwa naoga boss wangu

Raymond: una uhakika? Angel yuko wapi?

Ramadhani: mi si nilijua upo nae boss

Raymond: nipo nae kivipi?

Ramadhan: tangu ameondoka asubuhi hajarudi

Raymond: unajua unachokiongea Mimi sikielewi unamaanisha nini Angel hajarudi toka asubuhi?

Ramadhan: haki ya Mungu tena nakuambia…alitoka kwenda sokoni na akaniaga kuwa anaenda sokoni ila atakuja ofisini kwako kukusalimia…hakurudi nikajua labda ndo kaja huko kwako

Raymond: hapana hakuja…

Ramadhani: leo hujarudi nyumbani hiyo ikanifanya niamini upo nae

Raymond :( anaonekana kuchanganyika) Mungu wangu ngoja nimpigie dada yake (anajaribu kumpigia Catherine) Catherine

(Simu inaita mwisho inapokelewa)

Raymond: shemeji…. mdogo wako yupo huko?

Catherine: hapana…kwema lakini Shem?

Raymond: kwema

Catherine: amekimbia tena? Huku hayupo

Raymond :( anaweka mikono kichwani ishara ya kuchanganyikiwa) Mungu wangu…atakuwa wapi huyu jamani?

Catherine: kwani vipi? Kakimbia au?

Raymond: hapana…yaani sijui

Catherine: ngoja niwasiliane na familia yake

Raymond: si watachanganyikiwa Sana?

Catherine: sasa asipokuwepo kwangu unadhani atakuwa wapi?

Raymond: Mungu wangu…sijui basi sawa waulize au sijui tuache kwanza mama yake si unajua ana presha tusije tujasababisha makubwa

Catherine: yaani…anyway sawa…ngoja nitafute njia kujua Kama amefika nyumbani au lah naweza kwenda kumuuliza hata rafiki yake

Raymond: yupo hapa hapa Dar?

Catherine: hapana…

Raymond: okay shemeji fanya unavyoweza

Catherine: sawa…ila naomba utulie

Raymond: sawa shemeji yangu (anakata simu)

Ramadhani: sasa sijui yuko wapi?

Raymond :( anaonekana amekosa nguvu kabisa) wewe hukumgundua labda Kwa habari ya marafiki?

Ramadhani: hapana kwanza alikuwa hana marafiki Zaidi ya yule dada uliyemuaweka Kwa ajili ya kumtengeneza nywele kila mara akihitaji kutengeneza nywele…

Raymond: labda kaenda Kwa huyo dada

Ramadhani: labda

Raymond :( anaiangalia namba ya yule dada na kuipigia)

(Simu inaita Kwa sekunde kadhaa kisha inapokelewa)

Raymond: nambie mambo vipi?

Dada: poa boss kwema?

Raymond: dah…kwema

Dada: nambie boss wangu

Raymond: Angel upo nae?

Dada: hapana boss…sijamuona tangu siku ile nimekuja kumsuka siku ambayo mlikuwa mna mtoko jioni yake

Raymond: dah!!Poa hamna noma, Asante (anakata simu na kumgeukia Ramadhani) dah hayupo…Angel jamani upo wapi mpenzi wangu…

Ramadhani: labda alichukia ile juzi mlipogombana

Raymond: hapana mbona tulikuwa vizuri hata mpaka Leo asubuhi?

Ramadhan: sasa imekuwaje?

Raymond :( anajisikia kuchoka) Mungu wangu

Ramadhani :( analeta kiti haraka na kumpa akae) boss kaa tafadhali usije ukaanguka

Raymond :( Machozi yanamlenga) sijui kakimbia na mwanaume mwingine

Ramadhani: boss acha kuwaza huko jamani…atakuwepo tu sehemu tu…au karudi kwao labda kakumbuka

Raymond: labda... yaani sijui mwenzenu...Sijui ana shida gani (anaonekana kuchanganyikiwa)

Ramadhani: tulia boss

Raymond :( anajiinamia) sijawahi kupenda mwanamke Kama ninavyomependa huyu mwanamke jamani...Yaani hata Christina sikuwahi kumpenda hivi, can you imagine huzuni iliyo moyoni mwangu sasa hivi sijui Kama yupo au kakimbia na mwanaume au katekwa, au kauawa sehemu (machozi yanaanza kumtoka) sijui yuko wapi

Ramadhani: boss (anampigapiga kifuani) jikaze wewe ni mwanaume unatakiwa ujikaze na haya yote najua inatia huzuni hujui mwanamke wako yuko wapi ila hauna budi kujikaza

(Simu ya Raymond inaita na haraka anapokea)

Raymond: shemeji…

Catherine: nimempigia rafiki yake nyumbani hayupo

Raymond: Oh My God!!!

Catherine: tulia shemeji yangu atapatikana tu

Raymond: hapa sijui yuko wapi, sijui hata Kama ni mzima au kafa, sijui kama kala au hajala na kama amekula nini, yaani sijui chochote jamani Angel (Analia)

Catherine: shemeji tulia jamani na usiwaze huko atapatikana tu, ngoja nije (anakata simu)

Ramadhani: tulia

Raymond :( anaonekana Kama mtu aliyechanganyikiwa) Ramadhani jamani…mwenzenu Angel wangu yuko wapi…Angelina wangu malkia wa himaya yangu uko wapi kipenzi changu

Ramadhani: boss, Angelina atapatikana

(Raymond anasikitika Sana, na hajizuii kulia kukosekana kwa Angelina kumemchanganya sana)

Post a Comment

0 Comments