IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 32

 


SCENE 32: -

(Usiku huohuo, Raymond anafika nyumbani Kwa wazazi wake akiwa anaonekana amelia sana maana macho yake ni mekundu sana na yamevimba, anapofika mama yake anamuona kwa dirishani hivyo anatoka nje kumpokea)

Mrs.Bembele: baba…umenipigia simu unalia Sana, mwanangu nini?

Raymond: Angelina…

Mrs.Bembele: kafanyaje? Tena? (Anaingiwa wasiwasi)

Raymond: sijui yuko wapi tangu asubuhi hajulikani alipoenda, nimemtafuta pote mama hayupo, sasa sijui yuko wapi Na anafanya nini, sijui yupo Kwa mwanaume…Mimi sielewi

Mrs.Bembele: usiweke wivu baba Na ndo kinachokuliza, wivu

Raymond: mama yote, wivu na wasiwasi anaweza kuwa yupo kwa mwanaume, lakini pia anaweza kuwa yupo kwenye matatizo

(Baba Raymond anatokea ndani)

Mr. Bembele: kuna nini hapa?

Mrs.Bembele :( anamfuta mwanae machozi)

Mr. Bembele: Analia nini huyo?

(Raymond na mama yake wanakaa kimya)

Mr. Bembele: hamjibu sio? Labda hamjasikia swali…Analia nini huyo? (Kwa Raymond) Wewe Raymond unalia nini?

Raymond :( anakaa kimya)

Mr. Bembele: nauliza tena

Mrs.Bembele: msichana wake amepotea

Mr. Bembele: kwahiyo Kama amepotea yeye Analia kwanini…ni ndugu yako?

Raymond :( kimya)

Mr. Bembele: au mna ajenda gani au hawara yako? Maana Christina ameniambia umeachana nae sasa isije ikawa umemuacha Christina kuambatana na huyo maskini Raymond sitakuelewa

Raymond: ndio ni mpenzi wangu…nampenda sana na ndio nina huzuni hapatikani na wala sijui alipo

Mrs.Bembele: Raymond!!!

Mr. Bembele: Unasemaje???? Nahisi sijasikia vizuri embu ongea tena…umesemaje?

Mrs.Bembele: jamani acheni kugombana yaani kila mkionana mnagombana tu

Mr. Bembele: sikukusomesha uje utembee na takataka kama huyo housegirl wako, na wala sikukupa kazi na kukujengea nyumba ya kifahari uje utembee na takataka

Mrs.Bembele: baba Ray

Raymond: una bahati wewe ni baba yangu

Mr. Bembele: ungenifanyaje...Yaani huna adabu wewe ni wa kuniambia hivyo eti ndio ni mpenzi wangu, una mchumba Raymond na tayari nimeshatoa mahari sitatoa mahari kwa takataka nyingine

Raymond :( anaondoka zake huku Analia Sana)

Mrs.Bembele: mwanangu

Mr. Bembele: muache aende…halafu wewe ingia ndani haraka

Mrs.Bembele :( anaingia huku anaonekana ana huzuni Sana)

Mr. Bembele :( anamfuata kwa nyuma)

(Raymond anapanda gari lake na kuliondoa kwa kasi sana, anaonekana kuwa ana hasira sana, analiendesha gari mpaka nyumbani kwa kina Christina.anapofika anakaribishwa vizuri sana na mama pamoja na shangazi yake Christina)

Mama: karibu baba…

Raymond: Asante…shikamoo mama

Mama: marahaba baba…tupo

Raymond :( Kwa shangazi) shikamoo

Shangazi: marahaba baba karibu

Raymond: Asante…namuulizia Christina

Mama: yupo chumbani kwake…

Raymond: naomba uniitie

Shangazi: pita tu mbona ulikuwa unaingia tu

Raymond :( anaona asibishane na mtu anaelekea chumbani kwa Christina, baada ya hatua mbili tatu anafika mlango wa chumba cha Christina) hodiiii

Christina: karibu (ananyanyuka kivivu anaenda kufungua mlango) karibu (anashangaa kumuona Raymond)

Raymond: habari yako

Christina: marahaba…

Raymond: nimekuambia habari yako

Christina: ah salama jamani karibu

Raymond :( anamuangalia kwa umakini) mbona kama umeogopa na kupagawa kuniona

Christina: wasiwasi wako tu wala sina wasiwasi sema tu sikutegemea kukuona

Raymond: isiwe kesi (anasimama kimya kwa muda)

Christina: karibu (anamruhusu kuingia)

Raymond: Christina

Christina: abee...

Raymond: Angel yuko wapi?

Christina :( anacheka kidogo) wewe Raymond Mimi nitajuaje mitoko yake? Siishi nae mimi kwahiyo nitajuaje …sijui alipo

Raymond: are you sure?

Christina: iam sure Raymond I mean nitajuaje mpenzi wako ana madanga gani…Kama haonekani labda kaenda kwa madanga

Raymond :( anamuangalia Sana)

Christina: ndo hivyo Kama haonekani basi kaenda kwa wanaume zake

Raymond: mbona unaongea Kwa uhakika Zaidi utakuwa umempeleka nini? Au unajua alipo

Christina: eeh…eeh...Samahani kaka tena wewe na huyo mwanamke wako mnikome, eti chochote kibaya kikimtokea mimi…yeye ni mtu mzima anapoteaje kwa mfano, si atakuwa ameamua kutoweka…mimi usiniulize maswali ya kijinga

Raymond: poa Asante kwa muda na ushirikiano wako

Christina :( huku anaangalia pembeni) karibu

Raymond :( anaondoka)

Christina :( anabaki anafyonza)

Raymond :( anafika nje walipo mama na shangazi yake Christina)

Mama: vipi baba

Raymond: asanteni…Mimi naondoka

Shangazi: haya karibu

Raymond :( anaondoka)

Mama: macho yamemvimba au namuona vibaya…yaani anaonekana amelia Sana

Shangazi: atajijua

Mama: sijui ana shida gani

Shangazi: wewe anakuhusu nini? Kwani ndugu yako?

Mama: kwakweli hayanihusu…ngoja nikae kimya mie (anakaa kimya)

Shangazi :( anabaki kimya pia)

Post a Comment

0 Comments