IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 33

 


SCENE 33: -

(Asubuhi ya siku ya pili yake, kuna ubaridi ulioambatana na umande, Christina anafika katika jumba alimomuachana Angelina)

Christina :( anamuamsha kwa kumpiga teke) oya unalala lala nini hapa?

Angelina :( anaonekana ni dhaifu sana) nina njaa…tangu nimekuja sijala, nisamehe nimekosa

Christina :( anacheka Kwa dharau) pole kwa kuumwa njaa Angelina

(Kuna mtu anaingia)

Christina: baby…karibu nilijua huji Leo

Mtu :( Ni baba mzazi wa Raymond)

Angelina :( anashangaa Sana maana tangu ametekwa hakuwahi kumuona mtu wa pili, anashangaa kumuona baba mzazi wa Raymond) baba Raymond???!!!

Christina :( anambusu mdomoni)

Mr. Bembele: hajafa tu huyu takataka

Christina: nilitaka uje tumuue Kwa pamoja (anaacheka Kwa kejeli)

Mr. Bembele :( anamuangalia Christina kisha anambusu) Ni lazima afe maana ameshajua siri yetu ya muda Mrefu Sana lakini pili sitaki mwanangu aoe takataka…nataka akuoe wewe baby ili niendelee kukuona sio mbaya tukila baba na mtoto (anacheka sana) asante mpenzi wangu kwa kuniambia kuhusu Raymond na huyu kinyago nataka nimuue kabla Raymond hajaamua maamuzi ya kijinga

Christina :( anacheka Sana) oh baby jamani (anamuangalia Angelina) sijui Raymond ameona nini kwa huyu takataka

Angelina :( anasikitika Sana) mnachofanya sio sahihi nyinyi ni wakwe (anasikitika sana)

Christina: unasikitika nini?

Mr. Bembele: anasikitika kuwa anaenda kufa muda si Mrefu (anatoa bastola na kutaka kumpiga)

(Kuna mtu anakuja Kwa nyuma na kumuamuru aache kufanya anachotaka kufanya)

Mtu: embu subiri

(Christina na Mr. Bembele wanageuka na kuangalia ni nani wanakuta ni Raymond)

Christina :( Kwa mshangao) Raymond

Raymond: hujakosea…ni mimi

Christina: what are you doing here?

Raymond :( anacheka kidogo) kumbe ndo mchezo wenu…

Christina :( anashangaa Sana) what are you doing here? Umejuaje nipo huku?

Raymond :( anamuwahi Angelina) my queen

Angelina :( anaonekana ni dhaifu sana na mwili wake una vidonda vingi sana)

Raymond: nyinyi wawili…ni watu wa ajabu sana...Nimekuja muda Mrefu ilibidi nisimame niangalie vitendo vyenu vya aibu…sikutegemea kama Christina ungefika muda ukatembea mpaka na baba yangu mzazi? ili iweje…kwahiyo kumbe ulipokuwa unaniambia kuwa unanipenda kumbe bado ulikuwa unanidanganya? (anasikitika sana)

Christina :( amepigwa butwaa na haamini anachokiona)

Raymond: Na wewe baba…kumbe ndo maana unataka nimuoe Christina ili uendelee kumuona

Mr. Bembele :( hana cha kusema amebaki kimya Kama kuku aliyemwagiwa maji)

Raymond: mnataka kumuua mwanamke pekee anayenipenda Kwa dhati

Christina :( anajikuta anaona aibu)

Raymond: by the way naomba nikujibu swali lako wewe Christina…umeniuliza nimejuaje kuwa uko hapa…Jana baada ya kuongea na wewe sikuondoka nikabaki palepale kwenu, nilijificha tu…nikalala ndani ya gari langu, alfajiri ilipofika nilishtuliwa na mlio wa gari lako nikaamka na kukufuata hapa…

Christina :( anabaki anashangaa)

Raymond: nampenda Sana Angelina na ukweli utakaobaki kuwa hivyo…she is my queen na jinsi nilivyoona leo sidhani kama nitawahi kukurudia hata kwa dawa…nakuchukia sana Christina…nakuchukia sana Mr. Bembele

(Mr. Bembele na Christina wanabaki wamepigwa butwaa)

Raymond: now if you excuse me…I need to take my queen to the hospital… (Anambeba Angelina)

Angelina :( Kwa sauti ya chini) nasikia njaa…

Raymond: nitakupa chakula malkia wangu (anatoka nje na kuelekea kwenye gari lake, anamuweka vizuri kisha anapanda na yeye na kuliondoa gari kwa kasi sana)

(Huku ndani Kwa Christina na Mr. Bembele)

Mr. Bembele: Loh!!!Aibu gani hii mwenzenu

Christina: baby…don’t worry sio kwamba eti anakuchukia kweli ni hasira

Mr. Bembele: usiniite baby wako maana Mimi sio baby wako Christina, sijui imekuwaje mpaka nikaingia kuzini na wewe

Christina :( anamshangaa) nini kimekupata baby mbona sikuelewi?

Mr. Bembele: mwanangu amenitamkia kuwa hanipendi na yote sababu yako Christina

Christina: sasa Mimi nimefanyaje wewe baba...Kwani Mimi ndo nilikutongoza? Si wewe na tamaa zako ndo zilikufanya ukanifata

Mr. Bembele: Kwa aibu hii ya Leo sidhani Kama nitaendelea na wewe Christina

Christina: unaniachaje na mimi nina mimba yako?

Mr. Bembele: itoe sipo tayari kuipoteza familia yangu niliyoijenga kwa Zaidi ya miaka 30 kwa ajili ya uhusiano wa miaka miwili…sipo tayari naenda hospitali sijui ni hospitali ipi ila nataka kuongea na mwanangu najua nimemuumiza sana baba yangu…na ninajua anaweza kumwambia mama yake sitaki kuwapoteza mke na mwanangu kwa ajili yako Christina

Christina: umenipotezea muda Sana

Mr. Bembele: umejipotezea muda mwenyewe yaani wewe kwa akili zako ulihisi nitakuoa au nitamuacha mke wangu na kuja kwako? ulidhani nitamuacha Raymond wangu na kuja kwako…nimefanya kosa kuchangia mwanamke na mwanangu na kwa hilo ni lazima nimuombe msamaha mwanangu na kumuomba asimwambie mama yake

Christina: miaka miwili Bembele…

Mr. Bembele: hata Kama ingekuwa kumi…sipo tayari kumuacha Glory wangu na kuja kwako wewe Christina najua Gloria wangu ni mzee nampenda hivyo hivyo kuanzia leo sitaki tena mahusiano na wewe kwa muda wote huo ambao tumekuwa tukiwadanganya watu naomba uishie hapa sitaki tena

Christina :( anaongea Kwa jazba Sana) Nina mimba yako

Mr. Bembele: itoe I do not care

Christina: you bastard!!!Umenichezea Kwa miaka miwili Leo hii unaniacha kirahisi hivi?

Mr. Bembele: wewe ulidhanije? kwamba naweza kumuacha wife kizembe na kuja kwako? naipenda familia yangu na hakuna hata kitu kimoja ambacho kinaweza kututenganisha, sasa endelea na maisha yako…hata hivyo nimekulipa sana…nimekununulia magari ulikuwa unnaenda kutalii bure sehemu yoyote uliyopenda sasa unadhani sijakulipa kwa huduma ulizokuwa unanipa?

Christina :( anasikitika) wanaume

Mr. Bembele: ndo hivyo sasa…naomba niondoke Na usinitafute tena nitakuwa busy na familia yangu

Christina :( machozi yanamlenga)

Mr. Bembele :( anaondoka zake)

Christina:(anabaki Analia)nimekosa pote…sio kwa mwana na sio kwa baba…nimefanya nini?tamaa ningejua ningekaa na Raymond…kwa tukio hili hata nifanyaje Raymond hatanirudia…loh,nimekwisha mimi jamani zile raha zote zimeisha na nimebaki na Peter wangu asiyekuwa na pesa wale wenye pesa hawatanitaka tena,nimekosea mimi jamani(anajiinamia)dah..tamaa hizi jamani loh,Christina umeaibika wewe,umalaya umekuponza loh(anafuta machozi ghafla)No…hujashindwa Christina…hakuna mtu anayekuacha mpaka wewe mwenyewe upende kumuacha,pambana mtoto na baba wote ni wako na hakuna atakayekupokonya HAYUPO!!!!sio huyo Angelina wala sio huyo bibi kizee sijui Glory wewe ndo utaamua utataka kumuacha nani na lini na sio wao waamue…sasa wewe babu kizee na wewe Raymond msidhani mniweza mimi Christina(anaamka na kuanza kutembeatembea na kujigamba)siachwi naacha,na kwa nyinyi wawili nitaamua nitamuacha nani na nitabaki na nani na sio nyie kunipangia eti mnaniacha mnaongelea familia wakati mnanitongoza  hamkuwa na hizo familia?jibu ni kwamba mlikuwa nazo ila bado mkanifuata na kunipa ahadi kemkem kuwa mtanitunza leo limevumbuka hili mnajiweka pembeni,NO,NO siachwi kizembe mimi nitapambana mpaka kieleweke..(Anabeba mkoba wake kisha anatoka nje, anapiga hatua chache kisha analiangalia lile jumba kwa nje)Bembele aliniahidi kuninunulia hili jengo halafu leo ananikataa..Nitahakikisha ananinunulia (anaondoka zake)

Post a Comment

0 Comments