IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 34

 


SCENE 34: -

(Majira ya saa sita mchana, Raymond, Edmond na Catherine wapo hospitali wakisubiri kusikia hali ya Angelina inavyoendelea, wamekaa huku kila mmoja wao anaonekana ana mawazo sana ila zaidi Raymond)

Edmond:(anamshika bega) tulia Mond, atakuwa sawa

Raymond: wewe unasema tu maana kwanza umemkuta ana afadhali kidogo…hajala siku karibia tatu hali yake sio nzuri…ana vidonda mwili mzima na sijui kama umeviona hivyo, walikuwa wanampiga usiku na mchana, kama dozi

(Mr. Bembele anawasili mahala hapo)

Raymond:(anakunja uso ghafla na kuangalia pembeni)

Edmond: vipi? mbona umegeuka ghafla (anaangalia mlangoni anamuona Mr. Bembele) oh baba...shikamoo

Mr. Bembele:(kwa upole) marahaba baba…

Edmond:(anashangaa sana)

Raymond: unafanya nini hapa Mr. Bembele?

Catherine:(kwa Mr. Bembele) shikamoo baba

Mr. Bembele: (kwa Catherine) marahaba mama hujambo?

(Edmond na Catherine wanaangaliana)

Mr. Bembele:(kwa Raymond) naomba tuzungumze mwanangu

Raymond: mimi sio mwanao…sio mwanao kabisa Mr. Bembele maana kama ningekuwa mwanao sidhani kama ungenifanyia yale uliyoyafanya

Mr. Bembele: nisamehe mwanangu jamani nimekosa sitarudia tena

Raymond: maji yakishamwagika hayazoleki

Edmond: Mond?

Raymond: wewe niache tu Mond…huyu mzee alichonifanyia ni Mungu mwenyewe anajua kwanini alifanya hivyo

Edmond: amefanyaje?

Raymond:(kimya kidogo) acha tu… (anaenda kusimama mbali kidogo na wote)

Mr. Bembele:(anamfuata) mwanangu…baba yangu (anamshika bega)

Raymond: Don’t touch me please!!!by the way Go to your lover

Mr. Bembele: mwanangu…ningetaka kubaki huko ungeniona huku? nimekutafuta mpaka nimekupata

Raymond: najua kuna vitu unanidai (kwa hasira) haki ya Mungu ningekuwa na uwezo ningevirudisha vyote ubaya ni kwamba siwezi sasa naomba uniache nisije nikaongea maneno mabaya ukanipa laana wewe baba wewe…katika hali ya kawaida kweli baba unatembea na mwanamke niliyetembea nae…yaani tunachangia baba…baba, Ee Mungu dunia inaenda wapi hii? baba na mwana tunaingiliana?

Mr. Bembele: nisamehe sana baba yangu nisamehe mwanangu nakuomba baba yangu

Raymond: hapana…hapana…wewe nenda tu na sitaki kukuona tena

Mr. Bembele: usimwambie mama yako nampenda mke wangu

Raymond: siwezi kumwambia mama yangu upuuzi huo ataumia sana…

Mr. Bembele:(anashusha pumzi) asante mwanangu…mpenzi wako anaendeleaje?

Raymond:(anashangaa) mpenzi wangu gani?

Mr. Bembele: Angelina

Raymond:(anashangaa kisha anacheka kidogo) umeanza lini kumpenda Angelina wewe si ulikuwa unamwita takataka?

Mr. Bembele: sitamuita tena

Raymond:(anaguna kidogo) okay bado sijajua maendeleo yake dokta katuambia tukae hapa nje atatuambia

Mr. Bembele: najua mimi ndo chanzo cha matatizo yake

Raymond:(anakaa kimya)

Mr. Bembele: nitalipa bili yote

Raymond: usijisumbue…nitalipa, Mimi ndo nimemleta hapa kwahiyo nitalipa mimi

Mr. Bembele:na mimi ndo nimesababisha yote haya

Raymond:no need…halafu Zaidi usijifanyishe kuwa una mapenzi na malkia wangu ili nisiseme chochote kwa mama, usijali ndugu yangu sitamwambia mama wala hakuna atakayejua kuwa wewe na Christina mna mahusiano

Mr. Bembele: tulikuwa na mahusiano ila kwa sasa nimeyavunja nawapenda sana wewe na mama yako

Raymond: kwahiyo unataka nikupigie makofi kuwa hongera umefanya vyema baba

Mr. Bembele: Raymond nitafanya kila kitu ili mwanangu unisamehe nitatoa mahari kwa kina Angelina mwanangu utamuoa Angelina mwanangu nisamehe baba

Raymond: stop (anaangalia mlangoni) mama anakuja…na sijui utamjibu nini akikukuta hapa

Mr. Bembele:(anakaa kimya)

(Mrs.Bembele anawafikia)

Mrs.Bembele: vipi?

Mr. Bembele: poa…za huko?

Raymond: shikamoo mama

Mrs.Bembele: marahaba mwanangu mzuri (kwa Mr. Bembele) za huko nzuri, Raymond amenipigia simu ameniambia Angelina amepatikana lakini hali yake ni mbaya sana, kwahiyo nikaamua kuja hapa kumuona

Raymond:(anamuangalia baba yake)

Mr. Bembele:(anajitahidi kuwa wa kawaida) okay haina shida

Mrs.Bembele: pamoja na hayo yote sikutegemea kukukuta huku

Mr. Bembele:(anashikwa na kigugumizi)

Mrs.Bembele: sitaki kujua sana maana nyinyi ni damu moja labda mmeoneana huruma mkaamua kuja kupeana ushirikiano… (anacheka kidogo) kwahiyo Angelina yuko wapi?

Raymond: bado hajatoka chumba cha matibabu...

Mrs.Bembele: sawa…Mungu amsaidie atoke salama

Mr. Bembele: Glory, nakupenda sana mke wangu

Mrs.Bembele:(anashangaa kidogo) umekuwaje? kwani huu ni muda wa kuambiana nakupenda jamani…anyway (anacheka huku anamuangalia Raymond) nakupenda pia mume wangu

Raymond:(anacheka kidogo)

Mrs.Bembele: (kwa Raymond) bora baba umecheka maana ulivyokuwa umenuna(anaguna)

(Daktari anatoka)

Daktari: hali ya mgonjwa imeimarika kidogo

(watu wote waliopo hapo wanashusha pumzi)

Raymond: tunaweza kumuona?

Daktari: karibuni (anawaruhusu kisha anaondoka)

(wanaingia chumba alicholazwa Angelina)

Raymond:(anambusu shavuni) pole my queen

Mrs.Bembele: pole mama

Catherine na Edmond: pole Angelina

Mr. Bembele: pole Angelina

(wanashangaa)

Angelina:(kwa shida) asanteni

Raymond: utapona…

Angelina:(kwa sauti ya chini sana) asante

(wanaendelea kumfariji huku kila mmoja wao akionyesha huruma kwa majeruhi huyo)

Post a Comment

0 Comments