IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 35

 


SCENE 35: -

(Majira ya saa tatu na nusu usiku, Raymond na Angelina wapo nyumbani wanaonekana wametulia na wana Amani, wanaangalia runinga huku wameegemeana kwa mapenzi makubwa)

Raymond:(anamvuta Angelina na kumlaza kifuani kwake)

Angelina:(bila kubisha anamlalia)

Raymond: pole kwa mateso uliyoyapata hizi siku mbili tatu

Angelina: asante nimeshapoa

Raymond: niliogopa sana nikawa najiuliza sijui nitawahi kukuona tena malkia wangu

Angelina:(anacheka kidogo) Mungu ni mwema nimerudi na nipo nawe

Raymond: kweli Mungu ni mwema…na fadhili zake ni za milele

Angelina: hakika

Raymond:(anakaa kimya huku anamuangalia sana) uliishije huko?

Angelina:(anaguna kidogo) acha tu ndugu yangu yaani niliishi kwa shida kweli yaani hawakunipa chakula wala maji, kila wakija walikuwa wananipiga sana

Raymond:(anasikitika sana) aisee walikutesa…roho zao ni mbaya sana

Angelina: niliona ni muujiza siku ulipokuja

Raymond: nilikaa nje ya nyumba ya kina Christina usiku mzima

Angelina: kweli unanipenda

Raymond: (anamuangalia sana) inamaana huamini mpaka leo kuwa nakupenda mpenzi wangu?

Angelina: nami nakupenda sana

Raymond: asante…nataka nikuoe...hii staili ya kulala kila mtu chumba chake nimeichoka nataka tuwe tunalala wote

Angelina: tutalala wote tukioana

Raymond; nataka nikuoe mapema iwezekanavyo

Angelina: sawa Raymond mimi nipo tayari kuoana na wewe

Raymond: hata mimi…nakupenda Angelina sijui umenipa nini sijawahi kumpenda mwanamke hivi tangu nimeyajua mapenzi

Angelina:(anacheka) huwa inatokea...hata mimi nakupenda sana Raymond yaani siwezi kuishi bila wewe naomba usije ukaniacha kamwe katika maisha yako

Raymond: sitathubutu…. umeniweza baby…yaani umeniweza mpaka ukaniweza tena baby

Angelina:(anacheka)

Raymond:(anashindwa kujizuia, anambusu mdomoni)

Angelina:(anasogea pembeni) hapana Raymond wakati bado

Raymond: nakubusu tu wala sina nia nyingine

Angelina: sisi sote ni watu wazima na tuna hisia tunaweza kupitiwa

Raymond: exactly baby sisi sote ni watu wazima unachoogopa ni nini?

Angelina: mama yangu ananitegemea sana siruhusiwi kujisahau

Raymond: wewe…sio kujisahau bwana…ni mapenzi tu…nakuahidi hakuna kitakachoharibika…hata ukibeba mimba nimeshakuahidi kuwa nitakuoa

Angelina: hapana Raymond…

Raymond: tafadhali...mahusiano yetu ni ya muda sasa kwanini hutaki?

Angelina: tangu mwanzo tulikubaliana kuwa utasubiri mpaka tutakapofunga ndoa

Raymond: ndoa ipo jikoni Angelina naapa sitakufanyia ukatili kwa kukataa mimba au chochote kile

Angelina: hapana Raymond mi naenda kulala tutaongea kesho

Raymond: okay usiku mwema

Angelina:(anaingia chumbani kwake anajifunika shuka mpaka juu kisha anazima taa)

Raymond: Angelina hataki kabisa kuniamini na Zaidi sijui anaogopa nini penzi letu limeshakuwa na linastawi vizuri anachoogopa ni nini?

Angelina:(anatoka chumbani kuelekea jikoni)

Raymond:(anamfuata) Angelina

Angelina:(anajikuta anamkumbatia ghafla)

Raymond:(anamkumbatia pia) sisi ni wapenzi, wenye malengo sio vibaya kufanya mapenzi

Angelina: lakini ni dhambi

Raymond:(ananyamazisha kwa kuweka mdomo wake kwenye midomo ya Angelina)

(wanapitiwa na hisia za miili yao na wanajikuta wanaruhusu hisia zao ziwatawale)

Raymond:(anambeba Angelina na kumpeleka chumbani kwake)

Angelina:(haonyeshi ubishi)

Raymond:(anamlaza kitandani na anarudi anafunga mlango)

 

Post a Comment

0 Comments