IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 36

 


SCENE 36: -

KESHO YAKE ASUBUHI

(Raymond ameamka ila hafanyi chochote Zaidi ya kumuangalia Angelina, baada ya kujigeuzageuza hatimaye Angelina nae anaamka)

Raymond:za asubuhi?

Angelina:(anajinyoosha) Mungu wangu nililala chumbani kwako?

Raymond:(anatabasamu) kwani vibaya?

Angelina: vibaya ndio...Mungu wangu…jana tuliruhusu hisia zetu zitutawale

Raymond: sio dhambi…na wala sio vibaya

Angelina: Mungu wangu…halafu umechelewa sana kazini

Raymond: sitaenda kazini…nitawaambia kuwa naumwa

Angelina: kwanini?

Raymond: nataka kukaa na wewe

Angelina:(anacheka) jamani

Raymond: asante Angelina

Angelina: asante ya nini?

Raymond: kwa kila kitu kuja katika maisha yangu…sasa naona nuru nilikuwa naona giza sasa naona mwanga wa kutosha...asante pia hata kwa kunipa nafasi ya kuwa mwanaume wa kwanza kwako

Angelina:(anatabasamu kidogo)

Raymond: asante pia kwa Imani yako nakuthamini sana Angelina

Angelina:(anaona aibu)

Raymond: usione aibu bwana

AAngelina:(anachukua nguo zake kisha anashuka kitandani)

Raymond: unaenda wapi?

Angelina: naenda kuandaa chai

Raymond: I love you…nakupenda Angelina

Angelina:(anaona aibu anaondoka zake anaingia chumbani kwake)

Raymond:(anabaki anatabasamu)

Angelina :(yupo chumbani kwake) hapana Angelina ulichofanya sio kizuri yaani umekubali kufanya tendo linalofanywa na wanandoa kabla ya ndoa? inamaana umekuwa mjinga namna hiyo?

Raymond :(bado amekaa chumbani kwake) najua hukutaka ila jana hisia zilikuzidi nguvu mke wangu

Angelina :( akiwa jikoni) Mungu wangu nimekosea Sana…nikibeba mimba je? Nitamwambia nini mama jamani?

Raymond :( yupo chumbani) ngoja nikamuone anafanya nini? (anashuka kitandani na kwenda jikoni)

Angelina: Mungu wangu…kwanini nilijisahau?

Raymond:(anafika) ulijisahau nini mama?

Angelina: Raymond tumekosea sana nisingejisahau

Raymond:(anatabasamu) hapana wala sio mbaya baby  

Angelina: hapana Raymond hatukutumia hata kinga

Raymond:(anacheka) He!!!wewe kwahiyo unadhani nina UKIMWI?

Angelina: hapana jamani mi naogopa mimba…wadogo zangu wananitegemea sana

Raymond: tulia…huna UKIMWI labda mimba (anajificha uso)

Angelina: hapana kwakweli sitaki mimba

Raymond:ni mambo ya kawaida hayo kwa watu wanaopendana ni lazima mambo hayo yatokee

Angelina: nilikuambia tusubiri mpaka tutakapokuwa tayari yaani baada ya ndoa

Raymond: nitakuoa

Angelina: unasema tu kunitia moyo

Raymond: hapana sisemi kukupa moyo ninasema kwakuwa nina uhakika

Angelina: ulimvalisha pete Christina ukamuacha sembuse mimi

Raymond: usijilinganishe na Christina hamuwezi kufanana

Angelina: kivipi?

Raymond: wewe ni bora sana na wewe ni mzuri sana kuliko Christina

Angelina sawa haina shida kwahiyo unaniambiaje?

Raymond: tulia mpenzi usiogope …tupo pamoja

Angelina:(anatulia) haya bwana ila kama unanidanganya Raymondo anajua

Raymond: usijali mpenzi

(Wanakumbatiana)

Raymond: nakupenda mpaka nakupenda tena… (anatabasamu)

Post a Comment

0 Comments