IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRLN 37

 


SCENE 37: -

(Asubuhi ya siku nyingine tena Raymond yupo ofisini kwake, amekaa anawaza kitu Fulani lakini ghafla anajisikia vibaya na kuanza kulia kama kuugulia)

Raymond :( anaugulia) Ahhh….

Glory :(anakuja anakimbia) boss…

Raymond: mama (anashika tumbo)

Glory: unaumwa wapi?

Raymond: tumbo linauma sana…ah(anainama)

Glory: twende ukalale huku tukuhudumie

Raymond :(kwa sauti ya chini kabisa) muite Angelina

Glory: sina namba yake boss

Raymond:(anampa simu yake) itafute humu

Glory :( anaichukua harakaharaka na kutafuta namba ya Angelina anapiga anapoona anapiga)

(Simu inaita)

Angelina :(anapokea) my dear

Glory: hello Angelina

Angelina: wewe nani jamani? mbona unaongelea kwenye simu ya Raymond?

Glory: mimi ni secretary wa Raymond njoo huku ofisini kwetu Raymond anaumwa sana

Angelina :(anashtuka) Mungu wangu jamani nini tena?

Glory: tumbo na linamuuma sana...yaani linaonekana linamuuma sana jamani…fanya haraka sana

Angelina:(anakata simu na kukimbilia nje anatafuta bodaboda) Mungu wangu jamani mbona hata bodaboda hazipiti

(bodaboda inapita)

Angelina:(anaita) kaka…nipeleke

Dereva: wapi…

Angelina: twende tu…nitakuambia huko mbeleni

Dereva:(anaanza kuendesha na kuiondoa mara moja)

(Upande wa kina Raymond)

Raymond :( anatoka ofisini kwake)

Glory: boss ungekaa kutulia hapahapa

Raymond: niache tu huku sio kuumwa jamani acha watu wanione jamani nisije nikafia ndani humu

Glory: haya ngoja nikusaidia

(Wanatoka)

Raymand :(anashika tumbo) mama…(anaugulia)

Pendo:(anamuona) boss…(anakuja)boss nini?

Rachel :(anakuja pia)

Raymond: aah tumbo…

Pendo: ngoja nimuite Edmond

Raymond: nimeshampigia

(Edmond anafika akiwa na Catherine)

Edmond: nini tena Mond…

Raymond: naumwa tumbo vibaya…nahisi nakufa jamani nimeona niwaite wapendwa wangu wote…

Edmond: sasa si msaidieni jamani yupo hospitali ila hakuna msaada wowote inakuwaje?

(Angelina anafika)

Angelina: jamani…Raymond yupo wapi? (kwa pendo na Rachel) shikamooni

Pendo na Rachel: marahaba

Angelina:(anamuona Raymond anamuendea) Raymond nini tena?

Raymond :(anainuka na kupiga goti moja)

Angelina :(anashangaa) Raymond…

(Edmond na Catherine wanashangaa sana)

Raymond: Angelina

Angelina :(anaogopa sana) kuna nini?

Raymond: nimejifanya naumwa ili uje ofisini…tulipanga mimi, secretary, pendo na Rachel tulipanga tangu asubuhi…nimekuvuta huku ili nikuombe uwe mke wangu… (anatoa mkebe kutoka mfukoni mwake) siumwi hata kidogo ni pozi tu tumetumia…kukuvuta…huku nimeona hapa ni sehemu sahihi kufanya hili

Angelina :( anatabasamu)

Edmond :( anacheka) yaani wewe

Angelina: jamani Raymond

Raymond :( anaufungua mkebe) Angelina naomba uwe mke wangu

Angelina: sawa…nakubali

Raymond:(anamvalisha pete inayoonekana ni ya thamani sana)

(watu wanashangilia sana)

Angelina:(anacheka huku anaiangalia pete ile)

Raymond:(anamkumbatia Angelina) nakupenda sana mke wangu mtarajiwa

Catherine:(anafurahi sana)

(watu wanawapongeza sana)

Edmond:(anamuita Raymond pembeni) Mond…embu njoo

Raymond:(anamfuata) vipi are you not happy for me Mond...?

Edmond: iam very happy for you Mond ubaya ni kwamba unajichanganya?

Raymond: kivipi?

Edmond: wewe ni mchumba wa Christina au umesahau?

Raymond: wewe ndo umesahau my friend…mimi na Christina tumeshaachana siku nyingi sana

Edmond: amekubali

Raymond: inabidi akubali hana ujanja hapo

Edmond:(kimya kidogo kama anawaza kitu) haya lakini kama umeamua hivyo…by the way mnapendezeana sana

Raymond: eti eeh(anacheka)asanteeeee

(wanarudi walipo wengine)

Pendo na Rachel :(wanaishangaa sana pete ya Angelina)

Glory: basi mtaishangaa…nimeichagua mimi hiyo

Pendo: hujaulizwa mama

Catherine:(anacheka) jamani kama amefanya hivyo asiseme?

Rachel :( anacheka) anajishaua tu…ila boss sasa hivi kajua kuchagua

Glory: Sana

Edmond:(anawaangalia huku anatabasamu) hatimaye mmefanikiwa na mipango yenu hongereni sana

(Watu wote waliopo pale wanaonekana ni wenye furaha mara baada ya tukio fupi lililotokea)

Rachel: harusi lini?

Raymond: hivi karibuni

(watu waliopo hapo wanashangilia)

Post a Comment

0 Comments