IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 38

 


SCENE 38

 (Raymond anafika nyumbani kwa wazazi wake akiwa anaonekana ana furaha sana juu ya kitu Fulani)

Raymond:(anagonga mlango) hodi…

Mrs.Bembele:(anakuja kufungua mlango) karibu

Raymond:(anamkumbatia mama yake kwa furaha)

Mrs.Bembele: wewe nini? mbona sikuelewi?

Raymond: she said yes…

Mrs.Bembele: nani?

Raymond: Angelina mama…she is now my fiancée

Mrs.Bembele:(anamvutia sebuleni) wewe ongea taratibu baba yako akisikia atatunyonga au umesahau

Raymond: ah mama(anatembeatembea)sijali yeye anawaza nini…nachojua ni kwamba nimemvalisha pete ya uchumba mpenzi wangu na sasa ni mchumba wangu na ninampenda sana

Mrs.Bembele: hongera mwanangu yaani unaonekana una furaha wewe

Raymond: sana mama…yaani mpaka nahisi nataka kupaa kwa furaha hii mama, iam so happy mama

(Mr. Bembele anakuja)

Mrs.Bembele: baba yako huyo…

Mr. Bembele:(anamuangalia Raymond kwa aibu kubwa sana)

Raymond:(anaona amwambie hapohapo) nimemvalisha pete ya uchumba Angelina natarajia kumuoa

Mrs.Bembele:(anaziba mdomo kwa mikono yake miwili) wewe Raymond…

Mr. Bembele: sawa haina shida

Mrs.Bembele:(anapigwa butwaa) makubwa…leo imekuwaje baba Raymond umekubali

(Raymond na baba yake wanaangaliana chinichini)

Mrs.Bembele: yaani unajua sikuelewi kabisa

Raymond:(anamuangalia baba yake kwa jicho la hasira sana)

Mrs.Bembele: eti umekubali Raymond amuoe msichana wake wa kazi au mimi nimesikia vibaya

Mr. Bembele: sasa kama ameamua mimi ni nani kupinga

Mrs.Bembele: lakini si ulisema mwanao hatakiwi kuoa takataka leo amekuja kukuambia kuwa amechumbia umemjibu haraka na bila kupinga kuna nini hapo?

Mr. Bembele: kwani mke wangu wewe unataka kuwepo nini hapo?

Mrs.Bembele: ndo uniambie wewe…kuna nini mbona hizi siku mbili tatu sikuelewi umekuwa mpole unawahi kurudi nyumbani na zile simu zako za mpaka saa sita usiku umeacha yaani umekuwa mume mwema kweli

Mr. Bembele: Nimeona tu nifanye hivyo kama ni vibaya nitaacha na kuendelea jinsi nilivyokuwa nafanya

Mrs.Bembele: hapana sijamaanisha nataka uache mume wangu ila nashangaa anyways… (anamuangalia Raymond) hongera mwanangu kwa kuchumbia(anacheka)kwa mara ya pili

Raymond: asante mama

Mrs.Bembele: nilijua tu utapigana mpaka umuoe huyu mwanamke

Mr. Bembele: inamaana ulikuwa unajua kuwa Raymond anatembea na msichana wake wa kazi?

Mrs.Bembele:(huku anatabasamu) ndio aliniambia tangu hata bado hajamtamkia kuwa anamtaka

Mr. Bembele:(hatii neno)

Mrs.Bembele: unajua mume wangu kwa mara ya kwanza nilimuona mtoto wetu kuwa kweli amependa

Mr. Bembele: aisee…basi kakua

Raymond:(anatabasamu kinafki mbele ya mama yake)

Mrs.Bembele:(anaguna) unajua mimi nafurahi nini? leo hamjagombana

Mr. Bembele:(anatabasamu) hautaona tunagombana tena…sasa hivi tutaelewana...nitamsaidia hata ile ndoto yake ya kujenga nyumba kwa ajili ya watoto yatima…

Raymond:(anashangaa) unasema kweli au unanitania?

Mr. Bembele: nasema kweli kabisa...na unaweza kuwa na marafiki wowote unaowataka

Mrs.Bembele: maajabu haya leo mimi (anacheka huku anapiga makofi) eeh jamani niacheni niende nikapike leo mume na mwanangu wamekuwa marafiki jamani (anaenda jikoni)

Raymond:(anajitupa kwenye sofa kama mzigo)

Mr. Bembele: mwanangu naomba unisamehe kwa yote niliyowahi kukufanyia…

Raymond: nitakusamehe yote ila sitakusamehe hilo la kutembea na mwanamke aliyekuwa mchumba wangu

Mr. Bembele: ndo maana nakuomba msamaha mwanangu…usimwambie mama yako…haki ya Mungu tena nimeachana na Christina yaani siku hiyohiyo umetukuta mwanangu…nampenda sana mama yako mwanangu jamani

Raymond: uwe umeachana nae au hujaachana nae baba hilo mimi sijui na wala sijali na unajua hivyo

Mr. Bembele: basi fanya kwa ajili ya familia yetu mwanangu…tupo watatu tu…jamani tukiachana na kutengana unadhani itakuwaje?

Raymond:(anavuta pumzi ndefu) kwahiyo unataka kuniambiaje baba?

Mr. Bembele: mimi ni baba yako lakini je umeshawahi kuniona nakuomba msamaha kwa chochote?

Raymond: hapana

Mr. Bembele: sasa naomba uone kuwa ninajuta kosa langu ni kweli baba na mtoto kuchangia mwanamke au mwanaume ni laana na ndo maana nimetubu naomba unisamehe baba

Raymond:(anakaa kimya huku anaonekana kuna kitu anatafakari)

Mr. Bembele: usimwambie mama yako unajua nampenda mama yako sana na akija kujua kuwa nimewahi kuwa na Christina ataondoka na kudai talaka hata mpaka mahakamani…nampenda sana mke wangu na ndo maana nimeshaachana na Christina hata ukimuuliza leo hii atakuambia kuwa tuliachana siku ile ile

Raymond: nikikuuliza dad…kwanini ulifanya vile na unasema kuwa unatupenda sisi familia yako? je upendo ndo uko hivyo kusaliti wapendwa wako?

Mr. Bembele: hapana mwanangu unajua ile ilikuwa tu ni tamaa…kuna siku niligombana na mama yako sana tu nikaona kuondoa stress nitafute mwanamke mwingine

Raymond: ukaona utembee na Christina mwanamke ambae alikuwa analala na mimi

Mr. Bembele: baba ilikuwa tamaa tu mwanangu…kwa wakati huo Christina ndo alikuwepo hapo…alikuwa kama amenitegea tu...

Raymond: naelewa kuwa ilikuwa ni tamaa kwa mara moja kwanini uliendelea nae?

Mr. Bembele: ndo maana nakwambia ni ujinga wangu tu wala sio kwamba mke wangu ana kasoro yoyote maskini…mke wangu mwenyewe mzuri…yaani na hivi kazaa mara moja…Mrembo kweli mke wangu

Raymond:(anajikuta anacheka) sawa…sitamwambia mama kitu chochote…iwe siri yetu

Mr. Bembele: sawa…asante… (kimya kidogo) enhe!!tunaenda kutoa mahari lini kwa kina Angelina?

Raymond:(anashangaa) hivi ulikuwa upo serious uliposema kuwa ni sawa mimi kumuoa Angelina

Mr. Bembele: sikuwa nakudanganya mwanangu…nimechoka kugombana na wewe huku ndo ulivyo…una rafiki unampenda kweli ni maskini, sasa hivi umependa msichana wako wa kazi, wajukuu zangu watatoka kwa mama maskini (anacheka kidogo) sina ujanja mwanangu…nimekubaliana na wewe…kesho njoo ofisini kwangu na yule rafiki yangu nani vile Desmond?

Raymond: Edmond

Mr. Bembele: yes…njooni mnitembelee

Raymond: hadi raha…dad asante

Mr. Bembele: usijali mwanangu sitaki tugombane tena, kwanza malkia wetu hapendi anaumia kweli si huwa unamuona ee

Raymond: kweli

Mr. Bembele: tusimuudhi tumpe amani jamani

Raymond: haswaaa

(Wanaendelea kuongea wakati Mrs.Bembele anaendelea kuandaa chakula kwa ajili ya mwanae na mume wake)

Post a Comment

0 Comments