IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 39

 


SCENE 39: -

(Usiku mwingine, Raymond amejipumzisha katika bustani yake nzuri iliyopo mbele ya nyumba yake huku mchumba wake ambae alikuwa msichana wake wa kazi yupo jikoni anaandaa chakula cha usiku)

Raymond:(anachukua simu yake kisha anampigia Angelina aliopo jikoni)

(simu inaita)

Angelina:(anaipokea) dear...

Raymond: hujamaliza kupika tu jamani? mimi nimekaa peke yangu nasikia upweke…jamani

Angelina:(anacheka kidogo) nameshamaliza kupika nasubiri maziwa yachemke, nikuletee

(maziwa yanachemka)

Raymond: fanya haraka bwana nataka kukaa na wewe…bwana

Angelina: haya nakuja (anakata simu kisha anamimina maziwa katika vikombe viwili vikubwa kisha anatoka navyo na kuelekea alipo Raymond)

Raymond:(anamuona kisha anampokea kikombe kimoja) asante kwa kuja…dear

Angelina:(anakaa pembeni yake)

Raymond:(anamsogeza karibu yake na kumkumbatia)

Angelina:(anacheka) nini?

Raymond: kwani siruhisiwi kumkumbatia mchumba wangu?

Angelina:(anacheka sana) jamani…unaruhusiwa

Raymond: sijui ulikuwa wapi miaka yote…wewe ni kiboko yangu

Angelina: hata wewe ni kiboko yangu…

Raymond: nakupenda sana Angelina wangu

 Angelina: nakupenda pia Raymond…

Raymond: Mungu atusaidie tuzae watoto mapacha

Angelina:(anacheka) yaani wewe… unahisi nina mimba

Raymond:(huku anacheka) inamaana hujapata tu mimba…?

Angelina: hapana sijapata mimba

Raymond: bahati yangu mbaya mwenzenu…

Angelina: nitabeba tu tukishaoana

Raymond: nitakuoa uleule mwezi tuliopanga mara ya mwisho wakati nataka kumuoa Christina…nitabadilisha tu bibi harusi

(Wanacheka)

Angelina: yaani unajua siamini

Raymond: huamini nini?

Angelina: baba yako amekubali jamani

Raymond: ndo hivyo hata hivyo Mungu alipanga tu Mimi na wewe tuoane kwahiyo amini tu kwamba tunatarajia kuoana

Angaelina:(anacheka kidogo)

Raymond: hukujua tu

Angelina: kujua nini?

Raymond: ungenipa mapema sasa hivi ungekuwa umeshakuwa mke(anacheka)

Angelina: Ha!!kwa hiyo Raymond ile siku ndo imekufanya unichumbie?

Raymond: sasa je si nikapagawa?

Angelina:(anashangaa)

Raymond:(anacheka sana)

Angelina: makubwa basi…kwahiyo nisingelala na wewe usingefikiria kunioa?

Raymond: nakutania mke wangu…nilipanga kukuoa tangu kipindi naanza kukupenda wewe ni wa tofauti sana…una akili nikikuweka ndani tunajenga nyumba hizi Zaidi na Zaidi au unajifanya?

Angelina:(anaguna) kwahiyo nijifanye siku zote za maisha yangu?

Raymond: nakutania…una hasira wewe…

Angelina:(amenuna)

Raymond: basi mama…tema mate tumpige Ray…amekuchokoza ee…haya (anakinga mkono mdomo kwa Angelina) tema mate mama…tumchape

Angelina:(bado kanuna)

Raymond: tema usiogope urefu wake…tema tumkate makofi Raymond

Angelina:(anajikuta anacheka sana) yaani wewe

Raymond:(anacheka pia) sipendi kukuona unanuna wewe…kwakweli basi tu

Angelina: mbona unapenda kuniudhi?

Raymond:si kawaida…mimi unajua sasa hivi ndo mwanao eeh wa kwanza

Angelina: He!!! Yaani niwe na litoto likubwa hivi? lina mandevu makubwa hivi…

Raymond: ndo lizuri…linakuwa linakutetea hilo lenye mandevu mengi

Angelina:(anacheka kidogo)

Raymond:(anacheka sana halafu anaacha kucheka ghafla, anamuangalia Angelina kwa muda)

Angelina: nini?

Raymond: wewe Mrembo…sana, nina bahati kukupata wewe

Angelina: mimi ndo nimepata bahati ya kukupata wewe mpenzi wangu

Raymond: Edmond alichelewa sana kukuleta

Angelina:(anatabasamu) wakati wetu ulikuwa haujafika

Raymond: nina furahi kuwa muda wetu umefika mpenzi

Angelina: nina furahi kuwa na wewe

Raymond: mimi Zaidi Angelina wangu…

Angelina: hivi kwanini ulinipenda mimi?

Raymond: swali gumu sana maana hata mimi sijui kwanini nilikupenda mpenzi wangu, ilitokea tu mimi na wewe tukawa hivi, pamoja na kwamba nilijitahidi kuzuia hisia zangu kwako ila moyo ukalemewa

Angelina: naupenda sana moyo wako

Raymond :( anatabasamu)

Angelina: wewe kweli ni mume mwema

Raymond: hata wewe ni mke mwema

Angelina :( anacheka)

Raymond: weekend hii naomba tutoke nje ya mji

Angelina: tutaenda wapi?

Raymond: Serengeti mpenzi wangu

Angelina: kwenye mbuga za wanyama?

Raymond: ndio, au utakuwa na kazi

Angelina: nyingi sana

(wanacheka)

Raymond: twende bwana tukatulize mawazo bwana

Angelina: sawa tutaenda

Raymond: (anambusu)

Post a Comment

0 Comments