IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 40

 


SCENE 40: -

(Asubuhi nyingine ya siku nyingine tena, Ramadhani yupo chumba kidogo kilichowekwa kwa ajili ya mlinzi, anaonekana ana mawazo sana)

Ramadhani: yaani sina hela halafu boss yupo busy kweli hata hanisikilizi tena jamani…mara aniambie nimsubiri atanipa jioni…jioni penyewe mbali na mama yangu kijijini anaumwa sana wanataka kumpeleka hospitali nitafanyaje sasa (anachukua simu yake anapekua majina) ngoja niangalie mtu ambae anaweza kunikopesha kwa muda jioni boss akinipa nitamrudishia (anaona jina la Christina) sijui nahangaika nini huku bank hii hapa ngoja(anampigia)

(Simu inaita)

Christina :(bado amelala kwahiyo haisikii)

Ramadhani: ah hili nalo ndo maana halijaolewa si cha ajabu bado limelala, (anapiga tena)

(Simu inaita)

Christina :( anashtuka) nini? (anapokea)hello

Ramadhani: shemela langu la ukweli hilo

Christina: nini…asubuhi asubuhi

Ramadhani: nimekumisi mie jamani uko wapi?

Christina: bwana ee(anafyonza)sema shida yako haraka mimi nina usingizi bwana

Ramadhani: duh…shemela saa nne hii bado una usingizi wewe noma…ila nakukubali…mwana

Christina: unataka nini?

Ramadhani: mama anaumwa

Christina: kwahiyo?

Ramadhani: naomba unisaidie mwanangu

Christina: hapo nikusaidia utanipa nini Mimi?

Ramadhani :( anacheka kidogo) kama kawaida nitakupa yaliyojiri wiki hii…

Christina :( anakaa maana alikuwa amelala) unataka sh. ngapi?

Ram adhani: elfu hamsini tu

Christina: niambie kwanza

Ramadhani: Raymond kamvalisha Pete ya uchumba Angelina

Christina :( anashangaa sana) eti nini?

Ramadhani :( anashangaa) inamaana ulikuwa hujui au unajifanyisha?

Christina: hivi Raymond ana kichaa huyu mwanaume, si alitakiwa anioe mimi? yaani kanivalisha pete ya uchumba halafu kaniacha solemba kaenda kumvalisha pete ya uchumba huyu mwanamke ambae haeleweki…ngoja niongee na baba yake...

Ramadhani: umechelewa Sana mama…baba mtu amekubali…waoane na mipango ya kwenda nyumbani kwa kina Angelina imeanza kupangwa tena kwa siri wanataka kumpa surprise Angelina

Christina :( anasikitika sana) jamani huyu mwanamme ndo wakunifanyia mimi hivi?

Ramadhani: mapenzi mubashara nakwambia hapa tu kila jioni wanakaa bustanini watashikana weeeee mpaka sisi huku tunaomba po!!Yaani ndugu yangu na hapa analetwa mfanya kazi mwingine huyu keshakuwa maza hausi sijui upo? haya leta hamsini yangu

Christina: nakutumia

Ramadhani: nasubiri (anakata simu)

Christina:(huku anatetemeka, anaenda kwenye menyu ya mpesa na kuanza kutuma pesa kwenda namba ya Ramadhani) Mungu siamini mimi leo nimewakosa baba na mtoto nani tena atanipa pesa? pesa jamani ndo byebye loh!!!!Wamenikomesha jamani wanaume wanajua kukomoa hawa jamani (anamaliza kutuma)

(Meseji inaingia kwenye simu ya Ramadhani)

Ramadhani :( anaangalia) mpesa imethibitishwa… (Anacheka) kumbe umbea nao kazi eeh (anabusu simu yake) haya bwana…ngoja niwatumie mie, embu ngoja nimshukuru (anapiga simu ya Christina)

(Simu ya Christina inaita tena)

Christina :( anapokea) umepata?

Ramadhani: ndio Asante

Christina: utaendelea kuniambia

Ramadhani: poa (anakata simu)

Christina:(ananyanyuka kisha anaenda mbele ya kioo kikubwa kilichopo chumbani humo) kwani mimi nina kasoro gani mpaka Raymond asinipende mimi na kunioa? kaona nini kwa huyo msichana wa kazi za nyumbani ambacho hakuona kwangu?

(shangazi yake anakuja)

Shangazi: wee mtoto

Christina:(anashtuka)

Shangazi: vipi mbona unaongea peke yako?

Christina: sijui kwanini ila najiona nimeshindwa

Shangazi: umeshindwa na nini?

Christina: nimeshindwa maisha

Shangazi: kivipi?

Christina: baba na mtoto wote hawanitaki

Shangazi:(anashangaa kidogo) yamekuwa hayo tena?

Christina: acha tu shangazi…yaani huyo mzee hapokei hata simu zangu na mtoto mtu sasa nasikia kamvalisha pete ya uchumba yule kijakazi

Shangazi:(anashangaa sana) eh makubwa (anakaa kitandani)

Christina:(anaguna kisha anakaa kitandani pia) sijui huyo kinyago kampa nini Raymond mpaka kaamua maamuzi makubwa ndani ya muda mfupi hivi?

Shangazi:(anashangaa sana)

Christina:(machozi yanamlenga) yaani Raymond nimehangaika nae miaka mingi leo hii anakuja kuniacha mimi na kutaka kuoa mwanamke mwingine…nimemvumilia mangapi leo anakuja kuniacha na kutaka kuoa mwanamke mwingine…kwakweli (anafuta machozi) siwezi kukubali…Raymond ni mume wangu namtaka…na ninamtaka baba yake pia maana alikuwa ananipa pesa za kutosha aliuwa ananisaidia sana

Shangazi:(anavuta pumzi ndefu kidogo) Christina mimi naona sasa uwaache…kiukweli naona mambo yamegoma

Christina: hakuna kilichogoma hapa shangazi…nitafanya kila mbinu Raymond na baba yake warudi kwangu…mimi ndo mwenye mamlaka ya kuwa na Raymond na baba yake na sio kinyago mwingine…utaona nitakachofanya hutaamini

Shangazi: kila mara ukipanga jambo Fulani linakurudia vibaya kwanini mwanangu usiwe na Peter wako…? wenyewe mnapendana hadi raha

Christina: namtaka Raymond na Bembele

Shangazi: Raymond ni wa Angelina na Bembele ni wa Glory waache mwanangu…wewe ni wa Peter…

Christina:(anapandwa na hasira) sitaki sasa na usinilazimishe niache kufanya haya…yote na nahitaji msaada wako

Shangazi: wangu tena?

Christina: nipe namba ya yule mtu aliyetusaidia mara ya kwanza…namuaminia

Shangazi: wewe Christina…unataka kuroga si uache mwanangu jamani sio kwamba hauna mwanaume anayekupenda

Christina: taja namba huwezi usiniongeleshe tena

Shangazi:(anataja namba)

Christina:(anaziandika kisha anapiga)

Shangazi :( anaondoka zake)

Christina:(anaonekana amepandwa na hasira) sishindwi kitu mimi…mwisho wa mpambano mimi ndo nitakuwa mshindi… (anatupa simu pembeni kwa hasira) mbona huyu nae hapokei simu yangu (anapiga tena)

(Anaendelea kujaribu kupiga simu)

Post a Comment

0 Comments