IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 5

 


SCENE 5: -

(Christina anafika nyumbani kwao akiwa anaonekana ana hasira sana juu ya kitu Fulani, anaingia ndani bila kuwasalimia mama na shangazi yake anaelekea moja kwa moja mpaka jikoni anafungua friji anatoa bia aina ya castle lite na kuanza kunywa huku akirudi sebuleni)

Mama: sasa shoga yetu mbona umepita hapa hata salamu kwani tumekukosea nini?

Christina: yaani acha tu mama yaani kichwa changu kimevurugwa achene tu...

Shangazi: tatizo nini?

Christina: Raymond...

Mama: huyu mumeo mtarajiwa?

Christina: ndio…huyu huyu…mshenzi Sana huyu mtoto…ananipa wakati mgumu

Shangazi: kafanyaje tena jamani mbona kelele Tu...

Christina :( anakaa maana muda huo wote alikuwa amesimama)

Shangazi: tatizo nini shoga yangu?

Christina: hivi mnaweza kuamini kuwa Raymond leo kanifanya nimpigie magoti…mimi Christina Damas ni wa kumnyenyekea mtu mimi…kanidharirisha sana na ni lazima atalipa (anakunywa bia yake ambayo wakati wote alikuwa ameishika mkononi)

Mama: umempigia magoti kisa nini…?

Christina: aliniambia kuwa tuachane

Shangazi: hivi huyo mumeo ana akili timamu? Miezi miwili imebaki mfunge ndoa anaanza kuleta ushenzi wake

Mama: hata iweje haitawezekana hata siku moja Raymond kumuacha Christina…yupo kiganjani mwetu hana ujanja acha tu ajipe moyo

(Wote wanacheka kimbea)

Shangazi: ila hizi hela zitatutoa roho haki ya Mungu loh!!

Mama: kwanza mama na baba yake hawawezi kukubali Raymond aoe mke mwingine hiyo aibu ataificha wapi?

Shangazi: anajipa moyo tu (kimya kidogo) hivi shosti ile dawa niliyokupa uliioga vizuri

Christina: hata sijaioga

Shangazi: ioge…

Mama: halafu Ili kumkomesha beba mimba yake

Christina: nyie mnajua kabisa kuwa nampenda Peter na kwa Raymond nachuna tu pesa nikale na Peter wangu

Shangazi: tunajua sana tu…ila njia ya kumkamata ni kubeba tu ujauzito wake basi mambo mengine yatajipa

Christina: ngoja nitafikiria…

Mama: shoga yangu fikiria haraka haraka maana miezi miwili sio mbali kesho kutwa tu mama

Christina: naelewa Sana tu na ondoa shaka kabisa kila kitu kitakuwa sawa wala usijali...

(Simu ya Christina inaita)

Christina :( Kwa sauti ya kimahaba) hello my love, nilikuwa nakufikiria, sasa hivi

Peter: kweli? (Anacheka kidogo) nimekumisi Christina, mbona huji kuniona mpenzi wangu

Christina: nitakuja tu, honey wewe ondoa shaka  

Peter: ok haina shida, uko wapi na unafanya nini sasa hivi…

Christina: nipo nyumbani nipo tu sina cha kufanya

Peter: njoo kwangu sasa hivi

Christina: no, baby, nitakuja baadae tufanye usiku nije nilale huko

Peter: ok hiyo iko vizuri Sana hapo sasa ndo umenena, poa nitakuona baadae…

Christina :( anakata simu yake)

Mama: mwenzangu umekufa umeoza kwa huyo Peter mtu mwenyewe hana hata hela

Christina: hivyohivyo tu mama, sijali ananifikisha napotaka

Shangazi: wacha weee…

(Wanacheka kimbea)

Christina: sio huyo fala, mwaka wa sita sijawahi hata kubeba mimba hata kwa bahati mbaya loh!!!

Shangazi :( anacheka) hivi Raymond alikubamba na Peter eeh…

Christina: ndo maana yake yaani siku hiyo walipigana kumbe na mimi mzuri ee yaani wanaume wawili tena wazuri wanapigana kwa ajili yangu (anacheka)

Shangazi: yaani we chizi kweli

Mama; shoga yangu hukutupa michapo nakwambia Raymond alikuja hapa kapaniki kuliko maelezo kweli ilimuuma

Christina: atajijua mwenyewe mi napenda tu anavyonipa hela yaani Raymond hanifikishi yaani mshamba huyo

Shangazi: tatizo ulokole kila saa Yesu, Kha!!Hata huyu Yesu jamani anachokwa kutajwa

(Wanacheka tena kimbea)

Shangazi: ila tuache utani Raymond, mzuri huyo mtoto duh!!Ningekuwa kijana ningejiweka hapo mazima…ana kifua unasemaje huwa hakufikishi?

Mama: mlokole yule (anacheka) si cha ajabu huwa anaona dhambi kuzini

(Wanacheka tena)

Christina: Kwa kifupi pamoja na uzuri, sijui utajiri yaani hajiwezi kabisa mjinga yule

Shangazi: basi usimtukane

Christina: yaani Raymond kanichosha basi tu, yaani hapa nataka anioe baada ya miezi kadhaa naenda kuomba talaka mahakamani

Mama: na umejipanga

Shangazi: kikubwa tu oga ile dawa miezi miwili ni mingi sana mambo mengi yanaweza kutokea hapa katikati anaweza akakomaa kuwa anataka kukuacha halafu ndoto zako zikaishia hapohapo kuwa makini sana

(Wakati huo wanaendelea na mazungumzo msichana wao wa kazi aliyekuwa anafanya kazi ndogondogo sebuleni anawasiliza maneno yao ya kebehi na umbea)

Mama :( Kwa msichana wa kazi) we mbwa unasikiliza nini yaani hiyo kazi umechukua masaa mia kuimaliza embu toka hapa nenda kapike huko tule

Msichana: sawa mama (anaondoka)

Mama: eti mama Mimi mama yako Mimi, sina mtoto maskini kama wewe

Shangazi: au sio!!!

Christina :( anacheka) wacha we

Mama: olewa mwanangu niishi Zaidi ya malkia maana hiyo familia (anaguna) wana pesa jamani loh…

Shangazi: hivi hili danga Christina alilipataje?

Mama: danga gani?

Shangazi: Raymond…

Christina: baba yake na baba yangu ni marafiki sana, sasa siku moja kulikuwa na sherehe nikawa nimeenda na baba nay eye akawa amekuja na wazazi wake hapo ndo tukaonana, baba zetu wakaanza kusema upumbavu kuwa tunaendana na ingefaa kama tungeoana basi na yeye sijui akanipenda ndo tukaanza urafiki mwisho tukawa wapenzi ndo leo hii tupo hapa

Shangazi: duh...

Christina: Na kipindi hicho Raymond alikuwa ananipenda balaa jamani loh…nilie nini…Mimi tayari Napata …leo hii kawa mshenzi sijui kaopoa mhindi huko...

(Wanacheka)

Mama: wewe hawezi kuchanganywa na mhindi wale huwa wanachanganyana wenyewe…tu

Christina: sasa nini jamani unajua amebadilika yaani kawa mkali (anaguna)

Mama: atajijua mwenyewe

Post a Comment

0 Comments