IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 41

 


SCENE 41: -

SAFARI YA KWENDA SERENGETI: -

(Mchana wa siku ya jumamosi, Angelina na Raymond wanashuka katika kiwanja kidogo cha ndege kilichopo Serengeti mbuga za wanyama)

Raymond: pole dear…ulikuwa unaogopa sana(anacheka)

Angelina: acha tu…unajua sijawahi kupanda ndege katika maisha yangu na wala sikudhani kama kuna siku nitawahi kupanda ndege

Raymond: yote yanawezekana na unajua hilo…

Angelina:(anashangaa) naweza kupiga picha?

Raymond: ndio…unaweza kuwa huru baby

Angelina:(anapiga picha)

Raymond:(anafurahia mazingira ya mbuga hiyo)

Mhudumu:(anakuja na kuwakaribisha) karibuni sana…

Raymond: Asante sana…

Mhudumu: mngependa kufanyaje?

Raymond: ningependa kila kitu, kula, kulala, kuangalia wanyama na kuwa na wakati mzuri mimi na mchumba wangu

Mhudumu: sawa…kuna vyumba vina elfu 40 na kuendelea kuna chakula cha asili na vya kizungu

Raymond:(anacheka)

Angelina:(bado anapiga picha kila kitu anachokiona)

Raymond: kwanza naomba ukatuonyeshe vyumba, baada ya hapo tukatembee na kisha tuje tumalizie na kula

Mhudumu: sawa karibuni (anawaongoza njia)

Raymond: malaika…twende

Angelina:(anamfuata)

Raymond:(anaangalia mazingira) wow jamani pazuri...

Angelina: sana

Raymond:(kwa Angelina) umepapenda baby?

Angelina: pazuri…

Raymond: leo utapapiga picha mpaka tuelewe somo

Angelina: yaani we acha tu

Raymond:(anambusu mdomoni) nakupenda sana

Angelina: hata mimi…ila (anamuangalia mhudumu) tusifanye ujinga mbele ya huyu dada

(wanacheka)

Raymond:(kwa mhudumu) eti anakuogopa

Mhudumu:(anatabasamu) wala asijali kabisa ndo maeneo yenu ya kujidai haya

Raymond:(kwa Angelina) nilikuambia sikukuambia?

Angelina: uliniambia ila mwenzio nasikia usingizi…hatufiki tu

Raymond:(anashangaa) yaani wewe una vituko sana tumekuja kuenjoy au kulala

Angelina: vyote

Raymond:(anacheka huku anamuangalia mhudumu)

Mhudumu: acha adeke jamani

Raymond:(anaguna) haya bwana…mimi naenda kukuacha halafu ukiwa peke yako chumbani simba huwa wanakuja kukutembelea (kwa mhudumu) si eti dada ee

Mhudumu:(anacheka) yaani nyie

Angelina: basi kama ni hivyo turudi nyumbani

Raymond: rudi peke yako…

Angelina: napajua basi hata huko tulipotoka

(wanacheka)

Mhudumu: yaani mna vituko kweli

Raymond: sio mimi ni (anamshika Angelina) ni huyu

Mhudumu:(anawafikisha kwenye chumba kimoja kizuri na kinaonekana ni cha gharama sana) enhe!!mnakionaje?

Raymond: wow…kizuri kweli

Angelina: embu nione changu

(mhudumu na Raymond wanaangaliana kisha wanaangua kicheko)

Raymond: chako???

Angelina: ndio

Mhudumu: mnalala wote si wachumba?

Angelina:(anakaa kimya)

Mhudumu: haya bwana mimi ngoja niwaache mtaenda kulipia pale mapokezi

Raymond: sawa

Mhudumu:(anatoka)

Raymond:(anamfuata Angelina na kumkumbatia kwa nyuma)

Angelina:(anaona aibu)

Raymond: najua unaogopa sana mke wangu…naomba usiogope mimi wala sitakudhuru na kama hutaki na hujisikii mimi nitakuelewa tu

Angelina: sawa nimekuelewa…

Raymond: okay dear…unataka kuoga kabla ya kwenda kuangalia wanyama au unatakaje?

Angelina: kuoga sawa nitaoga kwanza

Raymond:(anamuonyesha bafu) bafu ndo hili

Angelina:(anafungua begi lake na kutoa khanga kwa ajili ya kuoga)

Raymond:(anacheka) yaani unaniogopa wewe(anashangaa)sasa utamuogopaje mumeo?

Angelina:(anacheka)

Raymond: basi sawa ngoja nijipe adhabu naondoka naenda zangu nje wewe oga ukimaliza nitarudi(anatoka)

Angelina:(anaingia kuoga)

Raymond: (amekaa nje anachezea simu yake)

(Baada ya dakika kama kumi na tano, Angelina anatoka kuoga na Raymond anarudi ndani, anavua nguo kisha nay eye anaingia kuoga, nae ndani ya dakika kumi na tano anamaliza kuoga, anatoka bafuni anakuta Angelina tayari ameshavaa anamsubiri, anavaa mbele yake na anaonekana hajali, Angelina anaona aibu anatoka nje)

Raymond:(anacheka) yaani wewe sasa usiponizoea sasa hivi utanizoea lini?

Angelina:si bado (anatoka nje)

(baada ya dakika kadhaa Raymond nae anatoka nje)

Raymond: haya twende

Angelina: nishike mkono maana naogopa kweli

Raymond: usiogope nipo na wewe mpenzi wangu

Angelina: (anatabasamu)

(Wakiwa wameshikana mikono wanaelekea mbugani kuangalia wanyama, huko wanafurahia mandhari, wanapiga picha kwa kifupi wanaonekana wanafurahia mapumziko yale ya mwisho wa wiki)

Post a Comment

0 Comments