IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 42

 


SCENE 42: -

BAADA YA SIKU TATU: -

(jioni ya siku ya tatu, baada ya Raymond na mchumba wake (Angelina)kurudi kutoka Serengeti, Raymond anafika nyumbani kwa baba na mama yake, anawakuta wazazi wake wamekaa wametulia huku wakiburundishwa na runinga kubwa iliyopo sebuleni hapa)

Raymond:(anaingia ndani) shikamoo mama, shikamoo baba

(wanaitikia)

Mrs.Bembele: oh, my son…za Serengeti?

Raymond:(anashangaa) Serengeti tena mama?

Mr. Bembele:si uliondoka ukaenda Serengeti wewe na mchumba wako?

Raymond: nani Christina?

(wazazi wake wanaangaliana)

Mrs.Bembele: embu acha masihala…mchumba wako ni Christina? wewe si ulikuja kutuambia kuwa umemvalisha pete ya uchumba Angelina?

Raymond:(anaonekana haelewi kitu chochote) Angelina wa wapi?

Mrs.Bembele:ni msichana wako wa kazi ila umempenda kisha ukaamua kumvalisha pete ya uchumba na unataka kumuoa

Raymond: mimi? mama mimi naanza saa ngapi kuoa msichana wa kazi?

(wazazi wake wanashangaa sana)

Raymond: anyways…mimi nimechoka nilipokkuwa hata sipajui kwakweli mara watu waniite dokta mara sijui nini?

(wazazi wanashangaa)

Raymond: naenda kulala… (anaingia chumba ambacho alikuwa analala wakati anaishi katika jumba hilo la kifahari)

Mr. Bembele: Raymond…siku hizi una nyumba yako…hicho chumba siku hizi sio chako

Raymond: baba unanifukuza nyumbani kwako au?

Mrs.Bembele: umekuwaje? wewe Raymond umekuwaje mwanangu wamekufanya nini huko Serengeti mwanangu?

Raymond: sijawahi kwenda Serengeti na wala sijamvalisha pete ya uchumba mtu hata Christina bado sijamvalisha ila nitamvalisha mpenzi wangu nampenda

(wazazi wanashangaa sana)

Mrs.Bembele:(anachukua simu na kumpigia Angelina)

(simu ya Angelina inaita)

Angelina: (anapokea)hello mama, shikamoo mama yangu…

Mrs.Bembele: marahaba mtoto wangu hujambo?

Angelina: sijambo…

Mrs.Bembele: wewe unajua hatumuelewi huyu mwenzio

Angelina: kwanini mama yangu?

Mrs.Bembele: kaja hapa sijui kapoteza kumbukumbu…sijui kafanyaje…hakumbuki kuwa yeye sasa hivi ni dokta, hakumbuki kuwa sasa hivi ana nyumba yake mwenyewe, hakumbuki kama wewe ni mchumba wake na wala hakumbuki kuwa mlienda Serengeti

Angelina: yaani acha tu mama…mimi mwenyewe leo nimempigia simu yaani hanikumbuki nimejitambulisha hakumbuki wala nini…mimi nikajua masihara yake kumbe kaja na huko

Raymond: jamani…mimi kichwa kinaniuma sana…naomba nikalale

Mr. Bembele: baba…una kwako…twende nikupeleke

Raymond:(anatabasamu) umenipa surprise baba…nimependa hiyo…

Mrs.Bembele:(bado anaongea na Angelina) yaani sijui amekuwaje huyu mtoto…ngoja tunakuja nae huko akiamka maana anasema anataka kulala kichwa kinamuuma

Angelina: sawa mama

Mrs.Bembele: haya mwanangu (anakata simu kisha anamgeukia Raymond) haya nenda kalale mwanangu

Raymond: sawa mama (anaingia ndani)

Mr. Bembele: nini tena hiki jamani?

Mrs.Bembele: yaani sielewi nini kimemkuta mwanangu

(wanasikitika sana)

Mr. Bembele: sijui tu

(Upande wa kina Christina anamalizia kupokea simu ya Raymond)

Mama :( anakuja alipo Christina) unaonyesha furaha sana, una yapi mwenzetu

Christina: wala…nina raha zangu tu (ananyanyuka na kwenda chumbani kwa shangazi yake)

Shangazi :( hana uchangamfu wa kawaida)

Christina :( anacheka Sana)

Shangazi: mwenzetu vipi? Mbona una raha Sana?

Christina: yule mtaalamu noma…

Shangazi: kivipi?

Christina: Raymond yupo kwao

Shangazi: kwahiyo kama yupo kwao?

Christina:(anacheka sana) nilichomfanyia mpaka mimi binafsi nimejiogopa

Shangazi: umemfanyia nini mtoto wa watu?

Christina: nimeirudisha akili yake nyuma…hakumbuki chochote kilichotokea hivi karibuni

Shangazi :(anaguna) kwahiyo unaona ufahari? kuroga?

Christina: sana…katoka kunipigia simu ananiita jina alilokuwa ananiita…tena na sauti ya madeko… (anaiga sauti ya madeko) Darling (anacheka kwa nguvu)

Shangazi:(anacheka) nasikitika kuwa sisi wenyewe tulikuharibu halafu tumejikuta tu tumekushindwa…Christina hata iweje…Raymond hawezi kukuoa maana Mungu mwenyewe hajapanga wewe uolewe na Raymond...

Christina: muone…wewe mwanamke una wivu wewe

Shangazi: moyo wa Raymond…upo kwa huyo kijakazi wake…wewe umemchezea akili tu…ila amini nakwambia Raymond akimuona Angelina kwa macho yake moyo wake utapingana vikali sana na akili yake…utakuwa umepoteza muda na pesa kijinga

Christina: tutaona…

Shangazi: tutaona…Christina…Raymond anampenda sana Angelina

Christina: hapana…ananipenda mimi

Shangazi: umemroga…hata ungemrudisha kumbukumbu za miaka 30 iliyopita bado Raymond akimuona huyo binti moyo wake utamtamani sana huyu binti

Christina: tutaona… (kwa hasira) tutaona, kama Raymond hatanioa

Shangazi: unajua kwanini mimi nilianza kwenda kinyume na wewe kwasababu niliona mapenzi waliyonayo Raymond na Angelina ni mapenzi ya dhati na hakuna aliyewahi kuyatenganisha mapenzi ya dhati iwe uchawi au nini, Angelina anampenda kweli Raymond yaani hajali kwamba Raymond ana hela au lah

Christina :(anafyonza)

Shangazi: utafyonza sana Christina ila ukweli ndo huo hapo…ukubali, mchezee sana Raymond na akili yake maskini ila hakuoi…hawezi kukuoa, anampenda sana Angelina yaani hata wewe hakuwahi kukupenda kama anavyompenda Angelina

Christina :( machozi yanamlenga)

Shangazi: habari bure…

Christina: atanioa

Shangazi: sawa…toka chumbani kwangu nataka kupumzika…umefikia mpaka kuroga ili umpate mwanaume na sio kwamba unampenda unataka pesa zake…hivi unadhani Mungu haoni? Utaaibika vibaya na siku wala sio nyingi

Post a Comment

0 Comments