IAM IN LOVE WITH MY HOUSEGIRL 43

 


SCENE 43: -

(Asubuhi ya siku iliyofuata, wazazi wa Raymond na Raymond wanafika katika jumba la kifahari la Raymond, wanapofika Raymond anaonekana kushangaa mazingira hayo kama mtu ambae hajawahi kuliona hata siku moja, mama yake anamuangalia na kugundua kuwa mwanae anashangaa sana)

Mrs.Bembele: mtoto wetu amefanyaje mbona kama kapoteza kumbukumbu…yaani anakumbuka tu sisi ni wazazi wake ila hakumbuki kuwa ana nyumba yake na kazi yake

Mr. Bembele: tulia mke wangu hakuna kitakachoharibika tutulie na tujaribu kujua nini kimemsababishia kusahau kila kitu labda ameumia kichwa na kama ni hivyo tumuwaishe matibabu

Mrs.Bembele: kweli kabisa mume wangu…ngoja nimuulize mkwe wetu Angelina labda walipokuwa Serengeti labda mtoto wetu alipata jeraha kichwani tunatakiwa tujue

Raymond: mama, mbona baba kawa mpole hivi yaani hata hanigombezi tangu jana

Mrs.Bembele:ni baba yako mwanangu…anakupenda sana…

Raymond: anyway…tuachane na hayo… (anamuona Ramadhani) habari yako kaka?

Ramadhani:(anashangaa) He!!bosi

Raymond:(anashangaa) boss???boss yupi?

Ramadhani:si wewe…mimi Ramadhani

Raymond: wa wapi?

Ramadhani:(anashangaa sana) Ba!!!mazito haya jamani nyie

Mrs.Bembele: Ramadhani kaendelee na kazi zako

Ramadhani: mama mbona boss kasahau au anajifanyisha?

Mrs.Bembele: hapana…wewe nenda tu kila kitu kitakaa vizuri

(Angelina anakuja, Raymond anamuona lakini katika hali ya kushangaza anavutiwa nae)

Raymond: mama huyo dada ni nani?

Mrs.Bembele: ndo yule mchumba niliyekuwa nakwambia

Raymond: mmenichagulia?

Mr. Bembele: hapana mwanangu…ulimchagua mwenyewe...

Raymond: lini?

Mrs.Bembele: mna muda kidogo tangu mmependana…

Raymond: hata sikumbuki vizuri lakini wow…ni Mrembo sana, amenivutia sana

(Mr na Mrs. Bembele wanaangaliana)

Mrs.Bembele: amekuvutia?

Raymond: ndio…mpaka leo nilikuwa sijawahi kuona mwanamke Mrembo Zaidi ya Christina… (kimya kidogo huku anamuangalia Angelina anayekuja kwa mwendo wa kuvutia) kwani huyu dada anaitwa nani?

Mrs.Bembele: anaitwa Angelina…

Raymond: wow…Angel

Angelina:(anawafikia na kwa heshima anawasalimia wazazi wa Raymond kwa heshima kubwa sana) shikamoo mama, shikamoo baba (anapiga magoti)

(wazazi wanamuitikia)

Angelina:(kwa Raymond) dear…shikamoo

Raymond:(anatabasamu) marahaba…Angel hujambo? Ee wewe mzuri jamani

Angelina: sijambo… (kwa wote) karibuni sana (anawaongoza mpaka bustanini)

(wanafika bustanini wanaketi na Angelina anaenda jikoni kuleta vinjwaji)

Raymond: mama…huyu dada ana heshima Christina hana hata heshima si huwa mnamuona?

(wazazi wanaangaliana)

Raymond: mbona mnaangaliana? kwani nasema uongo?

Mrs, Bembele: hausemi uongo mwanangu

Raymond: sijui mlinichagulia au nilijichagulia mwenyewe nimempenda sana huyu dada na nitamuoa…kesho nitaenda kumwambia Christina kuwa sitaweza kumuoa…ila sijui atanielewa kweli?

Mr. Bembele: atakuelewa tu…

Raymond:(anamuangalia baba yake) baba…asante kwa nyumba…nzuri na kwa mchumba mzuri Angel…

Mr. Bembele: usijali mwanangu, ila Angel ulimchagua mwenyewe

Raymond: sawa, labda nimesahau kidogo(anacheka)hivi Edmond yupo wapi?

Mr. Bembele: atakuwa kwake

Raymond: anatakiwa awepo hapa kwenye ufunguzi wa nyumba yangu

(Angelina anarudi na vinywaji, anawatengea kisha anaenda jikoni, Raymond anamfuata)

Raymond: Angel…

Angelina: nambie dear, nini kimekupata? mbona jana asubuhi uliondoka vizuri kwenda kazini?

Raymond: kazini? kwani mimi kazini kwangu ni wapi?

Angelina:(anamshangaa) jamani umekuwaje leo? au unanitania?

Raymond: sikutanii Angel sema nini yaani nimekupenda kweli...wewe mtaratibu sana una heshima unafaa kweli kuwa mke wangu yaani wazazi wangu wamefanya vizuri sana kunichagulia mke na wenyewe wameona kuwa Christina hatanifaa kama mke, kwanza nimemfumania na yule hawara yake kama sio mara kumi basi mara kumi na mbili yaani…nampenda ndio ila hatanifaa kuwa mke wangu nitakufa siku sio zangu

Angelina:(anacheka) yaani wewe huo utani wako siupendi bwana baba na mama wanahofia sana bwana

Raymond: haki ya Mungu jamani mimi sikutanii…Angel

Angelina: inamaana hukumbuki kuwa tumetoka Serengeti siku sio nyingi?

Raymond: hapana sikumbuki yote hayo…inamaana kumbe tumeanza kuwa pamoja?

Angelina:(anamuangalia usoni kwa muda) ulifanyaje Raymond mpaka umesahau kila kitu…

Raymond: sio kwamba nimeshau kila kitu…ila nachoshangaa sijui kwanini Edmond hajaja kuniona muda Mrefu

Angelina: Edmond alikuja kabla hatujaenda Serengeti

Raymond: mimi sijawahi kwenda Serengeti Angel…

(Mrs.Bembele anakuja)

Mrs.Bembele: Angelina, naomba nikuulize kitu kama hutajali…

Angel: sawa mama

Mrs.Bembele: Raymond naomba utupishe kidogo

Raymond: sawa (kwa Angelina) nimekupenda kweli (anamshika shavu kisha anaondoka)

Mrs.Bembele:ni ajabu ila ni kweli…Raymond amesahau baadhi ya vitu ila moyo wake haujasahau kuwa anakupenda Angel

Angelina :( anatabasamu) mama kwani amefanya nini?

Mrs.Bembele: sijajua ila tunahisi labda ana jeraha, huko Serengeti hakujipigiza sehemu labda?

Angelina: hapana mama…hakujipigiza sehemu…

Mrs.Bembele: sijui amefanyaje…ila afadhali hiyo haijaathiri mahusiano yake na yako…yenu namaanisha

Angelina: yaani hilo ndo la kumshukuru Mungu mama

Mrs.Bembele: usijali mwanangu kila kitu kitarudi kama kilivyokuwa…na baada ya hili mipango ya harusi yenu itaanza

Angelina:(anacheka) asante mama…

Mrs.Bembele: haya andaa andaa kwa ajili ya mumeo…amesema amekupenda

Angelina:(anacheka)

Mrs.Bembele :( anacheka kisha anatoka) haya mie ngoja nikawakute huko sijui wanafanya nini

Angelina: haya mama…ngoja Mimi niandaeandae… (Anaendelea na shughuli zake)

Post a Comment

0 Comments